Bandari ya Mombasa Yatoa Ofa Kwa Mizigo ya Congo DRC na Kutishia Uhai wa Bandari ya Dar. TPA na Serikali mmejipangaje?

Bandari ya Mombasa Yatoa Ofa Kwa Mizigo ya Congo DRC na Kutishia Uhai wa Bandari ya Dar. TPA na Serikali mmejipangaje?

The Sunk Cost Fallacy

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2021
Posts
19,582
Reaction score
14,167
Nawasalimu kwa jina la JMT, bila shaka mnaendelea kuchapa Kazi..

Kama inavyosomeka kwenye kichwa cha habari, Bandari ya Mombasa imetoa Ofa kabambe na kedekede Kwa Mizigo ya Congo DRC kupitia kwao, Kifurishi cha Ofa kinahusisha mambo yafuatayo;

1. Kupunguza gharama za kuhifadhi mizigo.

2. Kufuta gharama na vikwazo visivyo vya kikodi barabarani.

3. Kuwapa eneo Ili wajenge Dryport yao Ili wawe wanahifadhia mizigo yao hapo.

4. Ofa zingine za ki institutions.

Naomba ikumbukwe kwamba Bandari ya Dar inategemea zaidi mizigo ya Congo DRC kwa mapato sasa kwa Ofa hizi ni wazi bandari ya Dar inaenda kuwa tembo mweupe.

Ni vyema serikali kupitia TPA nao wakaja na counter offensive za kukabili ushindani wa kibiashara na kuongeza competitiveness yetu kwenye biashara ya logistics.

Tanzania inaongoza kwa kuwa na utitiri wa Kodi na tozo kwenye biashara bila kusahau utitiri wa vikwazo visivyo vya Kodi NTBs kama mamizani kila sehemu,traffic kila sehemu,sijui parking za malori za Halmashauri na blaa blaa zingine kama hizo.

Tukiendelea hivi bandari yetu itakuwa tembo mweupe na ikumbukwe kwamba hakuna kosa Wakenya Wamefanya ila ni mbinu za kukuza biashara.


Source> Uchumi Forum👇

Screenshot_20220912-163840.png
Screenshot_20220802-205049.png
Screenshot_20220801-213547.png
 
Ndio tayari tutakuwa tumepoteza sasa,kwa hiyo unaona kupoteza ni sahihi?
Hizi Bandari mbili huwa ni shindani sana miaka yote, sio kwamba MSA huwa haipokei share yake ya mizigo ya DRC ya Mashariki sema wanataka kuwavutia Wafanyabiashara wengi zaidi wa Kikongomani.

Miaka yote DAR ikidorora MSA inachukua nafasi lakini naona sasa wameamua.

Hawa wa kwetu watachukua hatua gani zaidi ya kuongeza Tozo.
 
DRC wana Bandari moja ya Matadi ambayo inahudumia Kinshasa na maeneo jirani, na kutokana na sehemu zingine kuwa na miundimbinu hafifu au kutokuwepo kwa miundimbinu kabisa, na factor zungine ni umbali ni bora utoe mzigo DAR au MSA ni karibu kuliko Matadi hadi Bukavu Goma na Lubumbashi.

Kongo ni kubwa.
 
Back
Top Bottom