Bangi...

mimi nakushauri uhamie kingston jamaica! kule ndiko kuna free and fair selection.

but kama ni bongo, mi ntakuwa wa kwanza kuripoti abuse kwa invisible! teh!
 
mimi nakushauri uhamie kingston jamaica! kule ndiko kuna free and fair selection.

but kama ni bongo, mi ntakuwa wa kwanza kuripoti abuse kwa invisible! teh!

Hivi kwenda kule mpaka uwe na VISA???
 
Mie nahamia URUGUAY,kule wamehalalisha jana..
 
Pili, nilijifunza kuwa kuna hoja nzito na za kisayansi za kutetea matumizi ya bangi; na kwa upande mwingine wa shilingi, hoja nyingi za kupinga bangi hazina mashiko katika sayansi ya tiba.
Ndiyo maana sikushangaa pale Bunge (la chini) la Uruguay (Congress) lilipopitisha muswaada kuhalalisha bangi; na naamini Bunge la juu (Senate) pia litaafiki ifikapo Oktoba, mwaka huu.
Uruguay itakuwa imeungana na majimbo ya Washington na Colorado ya Marekani yaliyotangulia kuhalalisha bangi kama kiburudisho kwa watu wazima. Pia, majimbo 17 ya Marekani yamelegeza sheria dhidi ya bangi kwa kuruhusu kutumika kama dawa.
Msuba, hashish, hemp, marijuana, cannabis, reefer, hash, pot, sigara pori ni machache kati ya majina mbadala (a.k.a) ya mmea bangi, unaosadikika asili yake ni Asia ya Kati na umekuwa ukitumika kwa miaka kati ya 3,000 – 5,000 iliyopita.
[FONT=Verdana, Geneva, Arial, Bitstream Vera Sans, DejaVu Sans, Meiryo, Hiragino Kaku Gothic Pro, MS PGothic, Osaka, sans-serif]hii nime nukuu na kuja na hoja zangu[/FONT]
 
Makala ya KTN niliyoitaja inamnukuu daktari wa magonjwa ya akili, Dk. Lukoye Atwoli akisema utafiti unaonyesha kuwa bangi haitengenezi ‘utegemevu' (addiction), tofauti na sigara, pombe, na dawa nyingine haramu.Uzoefu wa Dk. Lukoye umethibitisha kuwa dhana kwamba bangi husababisha matatizo ya akili si sahihi na wagonjwa wengi waliofikishwa kwake wakidaiwa kuathirika na bangi walikuwa na maradhi ya akili muda mrefu, kabla ya kuanza kutumia bangi.
Dk. Lukoye ananukuu matokeo ya utafiti katika Kituo cha Waathirika wa Dawa cha Mathare kuwa theluthi-mbili ya wagonjwa walikuwa na maradhi ya akili kabla ya kuanza kutumia dawa za kulevya, na maradhi hayo yaliwachochea kutumia dawa na kujenga utegemezi.
Hata hivyo hakuna hata mgonjwa mmoja aliyekuwa na arosto au utegemezi (addiction) ya bangi, ila pombe, sigara, na dawa haramu aina nyingine.
 
ligalazi
 
Profesa Yenesew anasema mbali ya Tetrahydrocannabinol, kemikali nyingine karibu 500 zinatoa uwezekano wa matibabu ya maradhi mbalimbali. Profesa huyo anasema miti mingi ya dawa ina kemikali kati ya 5 – 10 tu, na hivyo kufanya bangi kuwa mti wenye thamani kubwa kitabibu.
 
mi najua ni hatari kwa afya ila hata sijui zinaharibu sehemu gani ya mwili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…