Uchaguzi 2020 Bango la Magufuli limenishangaza sana

Awe mnyenyekevu kwa kila kitu ili mpige dili vizuri.?

Haaaaa haaaaa,, nimecheka eti kwenye mkutano mmoja wa kampeni anasema hataki kusema uongo mbele ya viongozi wa dini, kwani anataka kwenda mbinguni. Anadhani hao viongozi wa dini kwakuwa hawamuambii ukweli basi hawajui kuwa yeye ni muongo na ibilisi mwenye madaraka. Na ni nani alimwambia mbinguni unapelekwa na viongozi wa dini?
 
Asante. Umetukumbusha na yale ambayo sikuyaweka lakini ni halisia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Awe mnyenyekevu kwa kila kitu ili mpige dili vizuri.?
Hakuna anayemlazimisha awe mnyenyekevu. Kama ni sifa asiyoipenda, na wala haiishi. Tatizo, kwa nini awadanganye watu?

Mpiga kura humpa kura mgombea kwa vigezo anavyoviona ni muhimu. Kuna watu wanapenda kiongozi katili. Ikiwekwa sifa ya ukatili, atapata kura za wanaomtaka kiongozi katili lakini atazikosa kura za wanaomtaka kiongozi mwenye huruma.

Kuna watu wanamtaka kiongozi mfitini, ikiwekwa hiyo sifa, mgombea mwenye sifa hiyo atapata kura za wanaomtaka kiongozi mfitini lakini atakosa kura za watu wanaomtaka kiongozi mpatanishi

Ndiyo maana ni muhimu sana kwa wapinzani wa Rais Maguguli, kuwaeleza wapiga kura kuwa bango la mgombea Maguguli ni la uwongo, kwa sababu Rais Magufuli siyo mnyenyekevu. Na wafafanue kwa uthibitisho ili kuwaokoa wale wanaomtaka kiongozi mnyenyekevu.

Japo mgombea unapenda kupata kura za watu wengi kadiri inavyowezekana lakini siyo lazima upate kura za watu wote kwa sababu wapiga kura wana matakwa yanayokinzana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nyie watu nyoko sana
 
Kuna bango moja la mgombea wa kiti cha Urais, Mh. Magufuli linasema eti Magufuli ni mnyenyekevu!

Nilipoliona bango hili, nikashtuka sana. Nikajiuliza maswali mengi:

1) Ni Magufuli mwenyewe amehiari kuwepo kwa bango la namna hiyo?...

Bila shaka umeusemea moyo wangu. Kwa nyongeza tu, huyu mtu ni muovu toka moyoni na hajawahi kuwa na upendo kwa yeyote isipokuwa yeye mwenyewe na ni mnafiki kupindukia.

Kumuita huyu mtu kuwa “ni mnyeyekevu” ni unafiki na harakati za kupotosha ukweli kwa matarajio ya kupata uDC au cheo chochote cha upambe!

Anachoonesha huyu mtu ni kinyume kabisa cha unyenyekevu!
 
Hizo ni namna tu za wapambe wa chama kupamba pamba mtu wao,sasa hapo huwa kuna sifa zauongo na kweli.Mabango ya mwaka 2015 waliweka na neno Muadilifu safari hii naona wamelitoa.itakua wameshtuka kwamba hili la uadilifu hapana aise.Namimi naona ata hili la unyenyekevu ni sifa isiyomstahili.
 
Kuna bango moja la mgombea wa kiti cha Urais, Mh. Magufuli linasema eti Magufuli ni mnyenyekevu!

Nilipoliona bango hili, nikashtuka sana. Nikajiuliza maswali mengi:

1) Ni Magufuli mwenyewe amehiari kuwepo kwa bango la namna hiyo?...
Anawachukia wazee na wastaafu kiasi ya kuwanyima pensheni zao! Labda Kwa sababu yeye hatazeeka au amejiwekea pensheni nono.
 
Kuna bango moja la mgombea wa kiti cha Urais, Mh. Magufuli linasema eti Magufuli ni mnyenyekevu!

Nilipoliona bango hili, nikashtuka sana. Nikajiuliza maswali mengi:

1) Ni Magufuli mwenyewe amehiari kuwepo kwa bango la namna hiyo?.....
Mkuu hizi sifa zinapaswa ziandiikwe Kwenye bango kubwa na litundikwe kila lango kuu la kuingia miji yote tz. Ni sifa za kweli
 
Kuna bango moja la mgombea wa kiti cha Urais, Mh. Magufuli linasema eti Magufuli ni mnyenyekevu!

Nilipoliona bango hili, nikashtuka sana. Nikajiuliza maswali mengi:

1) Ni Magufuli mwenyewe amehiari kuwepo kwa bango la namna hiyo?...
Na anavyomtajataja Mungu ipo siku atamlipa sawia Mungu hadhihakiwi. Magu anamdhihaki Mungu.
 
Kuna bango moja la mgombea wa kiti cha Urais, Mh. Magufuli linasema eti Magufuli ni mnyenyekevu!

Nilipoliona bango hili, nikashtuka sana. Nikajiuliza maswali mengi:

1) Ni Magufuli mwenyewe amehiari kuwepo kwa bango la namna hiyo?...

Mhe. LISU soma hiyo kisha iweke kwenye hotuba zako.
 
Ndugu yangu Bams, naona umesahau kuorodhesha sifa zake hizi...
  1. Ni kiongozi katili
  2. Ni kiongozi anayekurupuka
  3. Ni kiongozi asiye na hekima
Kiongozi mpenda sifa zisizo na tija.
 
Unahubiri amani na upendo huku unateka na kuwahonga wapinzani wako ili washindwe kurudisha fomu halafu unasema madiwani wako wamepita bila kupingwa huku ni kumdhihaki Mungu.Mnamtumia Mungu kisiasa subirini mapigo yake atawajibu tu Nina hakika.
 
Mh Rais anatisha aisee ile siku anacheza singeli Singida alivyonyanyukaa tuu high table wotee mbiooo naoo wakanyanyukaa kwa spidi ya umeme na kucheza nae.

Nikasema duhh hii shughuli pevuu
 

Madikteta na makomunist wote upenda kuabudiwa thus wao maendeleo ya watu sio vipaumbele vyao. Huwasomesha namba watu ili waabudiwe
 
Mh Rais anatisha aisee ile siku anacheza singeli Singida alivyonyanyukaa tuu high table wotee mbiooo naoo wakanyanyukaa kwa spidi ya umeme na kucheza nae.,
Nikasema duhh hii shughuli pevuu
Ila wakikosa maslai yao kusifu na kuabudu kunakomea hapo baada ya kukosa ubunge si musiba,kange, nkamia, bashite wakiziimba Tena zile tenzi za rohoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…