Bank gani inatoa mikopo mpaka milioni 100?

Bank gani inatoa mikopo mpaka milioni 100?

Alvin Slain

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
6,375
Reaction score
3,663
Habari za majukum wakuu?
Naomba kufahamishwa ni taasisi zipi au Bank zipi zinatoa mikopo, hadi milioni mia moja,
Karibuni kwa michango yenu.
 
Bank zote za kibiashara just uwe ma mahitaji muhimu ya kupata mkopo, sio mbaya ukafanya research we mwenyewe kwa kutembelea mabank mbalimbali yaliyopo karibu nawe, kama una uwezo wa kuwa na biashara ya M100 ni kitu cha ajabu sana kushindwa kutembelea bank mbalimbali kuuliza maswali muhimu juu ya mahitaji yako.
 
Mwenye kiti chake leo kabanwa na foleni
 
Habari za majukum wakuu?
Naomba kufahamishwa ni taasisi zipi au Bank zipi zinatoa mikopo, hadi milioni mia moja,
Karibuni kwa michango yenu.
Benki zote kubwa na ndogo zinatoa hiyo 100M. Inategemea na wewe ikiwa unakopesheka.
Nasema kwamba unakopesheka kwa maana hii.
1. Unataka kuifanyia nini na una nini mpaka sasa kitakachowashwashi wakupatie hiyo mia.
2. Uzoefu wako katika kile kinachokusukuma kukopa
3. Haujwahi kukwepa kulipa deni katika taasisi za fedha
4. Una dhamana ya kudhamini huo mkopo ukishindwa kulipa inauzwa kufidia deni. Unaweza pia kuwa na mdhamini akaweka mali zake.
5. Anuani ya kazi yako na ya makazi pia.

Kwa kuanzia hakikisha hivo vigezo unavyo.

Sasa tembelea FINCA, NMB, CRDB, BARCLAYS, EXIM, KCB, AKIBA na benki zingine nyingi utapata huduma na gharama zao za mikopo (riba) zinatofautiana. Wapo wanakusubiri tu kukipatia hizo pesa ukikidhi vigezo.

ONYO: PESA YA MKOPO SI YA KUFANYIA STAREHE, UTADUWAZWA
 
Vyuma vimekaza Mkuu, benki zinazingua kutoa pesa ,
 
Sio kweli ...kuna mtu wiki iliyopita kachukua mkopo wa milioni 20 ...msiishi kwa nadharia za mitandaoni watu wanapiga mishe na kupata pesa ..vile vile ukiwa na kila kinachohitajika mkopo unaupata ..
OK sawa mkuu
 
BENKI ZINATOA MIKOPO MPK BILIONI!
SWALI NI JE UNAKOPESHEKA?
AKAUNTI YAKO INA UWEZO WA KUWEKEWA MILIONI 100
UNA MZUNGUKO WA HELA UNAORUHUSU KUKOPESHWA MILIONI 100
UNAWEZA KUGENERATE PATO LINALOWEZA KUREJESHA HIYO MILIONI 100 KWA KILA MWEZI!

SO MILIONI 100 SIO ISSUE!
ISSUE NI UKOMO WAKO WA KUKOPESHEKA!
KUNA WATU WAKIENDA BANK WAKIAMBIWA BANK INAWEZA KUWAPA MILIONI 100,WANAACHA PROCESS ZA KUKOPA HUO MKOPO !
MAANA HAZIWATOSHI!
 
Habari ndugu zangu.
Nina wazo la Biashara ambayo inahitaji Fedha kwa ajili ya uwekezaji. Benk Zilizo nyingi Zinataka Uwe na biashara ambayo imedumu zaidi ya miezi sita, Lakini Mimi s nina nyumba sina Biashara ambayo benki wanataka iwe imedumu zaidi ya miezi sita,naweza kuchukulia mkopo kutokana na hio nyumba. kama kuna taasisi binafsi hata Bank ambazo bado wanakubali kuchukua nyaraka za Nyumba ili nipate Mikopo nakuombeni Ushirikiano wenu wa hali na mali.

Asanteni .
 
Back
Top Bottom