Banki sio rafiki kwa Mfanyakazi/mtu wa kipato Kidogo

Naomba kuuliza vip benki ya NMB ni nzuri kwa ajili ya kutunza hela na makato yake kwa mwezi ni sh ngapi?
 
Motivation speaker katika ubora wako [emoji23]
 
Hesabu za kwenye daftari hizo mkuu acha kumdanganya mtoa mada na kudanganya watu. hizo hesabu za weka hii utapata hii ni hesabu chonganishi. Hamtofautiani na wapiga ramli nyie. Hizo hesabu zako hujazungumzia utapata wapi soko la mahindi, changamoto za serikal kufunga mipaka ya mazao, ushuru wa mazao katika mageti, msimu mbovu wa mvua, gharama za uendeshaji wa biashara hiyo kwa ujumla. We umekuja umepiga paah pah weka hii toa ile acheni dhambi nyie jamaa utashawishi watu wakakope wafanye kwa plan yako uliyo weka halafu kesho tukakuta watu wote andika uzi wa malalamiko mambo yamegoma tuwasaidie.
 
Bank gani hiyo inakopesha miaka 20?

👇👇👇👇👇
Benki ya CRDB ni Benki in ayoongoza hapa nchini kwa ubunifu wa huduma na bidhaa bora sokoni. Pia benki ya CRDB inatambulika kama kinara wa uanzishaji wa huduma na bidhaa mpya sokoni ambazo hukidhi matakwa ya mteja.

Katika kudhihirisha hilo, sambamba na kuzingatia uhitaji mkubwa wa makazi bora hapa nchini, Benki ya CRDB sasa imeleta bidhaa mpya sokoni ijulikanayo kwa jila la Jijenge. Jijenge ni mkopo wa nyumba ambao unakuwezesha wewe mteja wa Benki kumiliki nyumba ya ndoto yako kwa kununua, kujenga au kuboresha nyumba ya zamani. Mkopo huu ni sawa na kuwa kwenye nyumba ya kupanga huku ukiinuunua taratibu kila ufanyapo marejesho ya kila mwezi. Huu ni mkopo wa muda mrefu wenye kipindi cha marejesho cha hadi miaka 20 ambao dhamana yake ni nyumba hiyo hiyo ijegwayo , nunuliwa au kukarabatiwa.

Kupitia mkopo wa Jijenge, wewe mteja wetu unaweza kupata hadi shilingi milioni 500 na kurejesha kidogo kidogo kila mwezi au kwa agizo maalumu kwa Benki (standing order) au kwa mkupuo na tena kwa riba nafuu ambayo ni chini ya riba ya soko. Kwa kuwa mkopo huo ni wa kutosheleza, unakupa fursa wewe mteja kuweza kumiliki nyumba ya ndoto yako katika kipindi kfupii pasipo kusubiri kuweka akiba yako kwa muda mrefu.

Mkopo huu hutolewa kwa watanzania walioajiriwa na waliojiajiri ndani na nje ya nchi (kwa walio nje ya nchi wanapaswa kuwa na akaunti ya Tanzanite kutoka Benki ya CRDB ) na wenye umri kati ya miaka 21 hadi 60. Sambamba na hilo mkopo huu una bima ya mkopo (credit insurance) kwa mteja kama atapatwa na kifo au ulemavu wa kudumu ambao utamfanya ashindwe kuendelea na shughuli za kumpatia kipato na pia nyumba ijengwayo, inunuliwayo au kukarabatiwa huwekewa bima (property insurance) endapo itakumbwa na majanga kama vile moto na mengineyo.

Kwa maelekezo zaidi kuhusu Jijenge, au huduma/bidhdha yoyote ya Benki au ushauri tafadhari wasiliana nasi kupitia:

Simu:+255(22)2 19 77 00, 0714 19 77 00, 0755 19 77 00, 0789 197700,

Barua pepe: customer-hotline@crdbbank.com, Facebook:
http://www.facebook.com/crdbbank pia angalia tovuti yetu ku pitia www.crdbbank.com 👇👇👇
 
Na Hakuna Mfanyabiashara Mkubwa Makini Anaetumia Pesa Yake Kufanyia Biashara. They Use Other People's Money.

Mfano: Mtu Kama "Mo" Anaweza Kusoma Mchezo Akachukua Mkopo Wa Tsh 200M Bank Au Overdraft Akaagiza Boxer 200 Kwa Tsh 1M Kiwandani.

Then Anauza 2M Kila Pikipiki Halafu Anarudisha Mkopo wao.
 
Mwaka 2004 walimu wa shule ya msingi walikuwa wanalipwa 60000
Na huku shule za secondary za serikali za kutwa ada ikiwa elfu 20 kwa mwaka na bado watu wakawa wanarudishwa nyumbani mbaya kabisa kisa wazazi hawana pesa.
 
Kweli mkuu mikopo haina mwisho mzuri hata siku moja, nikisikia mtu anataka kukopa huwa namuonea huruma tu!
Sijawahi kuona alie kopa akafanikiwa siku ya mwisho lazima ile kwake tu,hakuna jambo zuri kama ukisave mwenyewe
 
Mkuu biashara haiko hivo usiweke hesabu as if utakuwa unakula wewe unga. Kuna kodi hapo kibao tu TRA, TFDA, Mazingira plus plus hali ya soko, kupanda kwa bei ya mahindi, wafanya kazi n. k hio Bil 1 ni hesabu za ndotoni.
Sijakataaa kuwa kuna utitiri wa mambo kama tra na tfda Ila muhimu ni lengo rasmi na uchaguz wa eneo sahihi la biashara. Kinachokufanya wengi wetu ni kufanya biashara Kwa kuigana na kukosa lengo rasmi.
Kama umenisoma vizuri kwenye bandiko langu no kuwa kila ntakapo nunua mzigo wa 5mil nipate wastan wa faida ya 300k Sawa na 6%, katikati Hali halisi inazid Sana no karibia 800k Kwa sasa.
Kwa kila mzigo 5mil utatoa pumba walau 3000kg au pungufu. Kiroba kimoja cha kilo 100 kinaenda 16000tsh. Kwa mzigo wa 5mil utapata pumba ya dhaman 480000. Kumbuka hapo huu sikuweza pumba.
Kwa ujumla faida IPO Sana Tu. Ni mzoefu wa hii KAZI mitaji ya kuanzia ndo sumbufu jaman
Ok sio kuwa motivation speaker hapana Ila nikazi ambayo nimekuwa naifanya Kwa muda mrefu Sana.
Kwanza niwekee wazi nimezungumza hivo kulingana na mazingira niliyotukana nafanyaje Mimi.
Kingine ieleweke sio kila biashara lazima jifanye dar au Tanzania ambako Ile ki Hali halisi kupiga hiyo pesa itakuwa ngumu.
Tukija kwenye selection ya eneo ambako ndo Kwanza ntaweza pendekeza Kwa MTU yoyote mwenyewe mtaji WA kiwango hicho ni either aende Mozambique na hasa mkoa kama nampula au kigoma Kwa upande wa Tanzania.
Tukija kwanini kigoma na wala sio dar.
Kigoma kama kigoma(kigoma mjini) kuna uhaba Sana wa chakula inafikia hatua unga WA sembe unafika mpaka 40k na Kwa wasiojua tu, hapa dar es salaam ni ngumu kupata unga WA sembe wa Azam tokana na ushindan mkubwa lakini Azam anauza kigoma sana. Na pia tukumbuke kilichozuiwa ni kusafirisha Mahind sio unga.
Kuna challenge umezungumzia ushuru wa mazao. Kama unafungua kiwanda na ukategemea kuwa utakuwa unafuata Mahind mwenyewe shamban jua ndo anguko lako kama huna mtaji. Siri iliyoko ni wewe kusubiria wanunue wa vijijin wa
Nadhani niliposimamia na wewe ulipoelekea ni tofaut. Mimi sijazungumzia kufuata mahindi vijijini bali nimezungumzia kuwekeza katikati uzalishaji. Katika uzalishaji wowote lazima utegemee kuwa na suppliers wa mzigo au Kwa lugha nyingine Mali ghafi. Kwa hapa bongo ni madalali. Na hawa kuna wengine wanaweza kukuletea mzigo mpaka Kwa mkopo na wewe ukapigana kuuuza bidhaa zako uliyotengeneza.
Kwa hiyo wewe utadili na tfda,tra, tanesco, na vipimo.
Tukija kwenye gharama za uendeshaji.
Karibia kila gharama itaendana na uzalishaji wako.
Mara nyingi huwa hatuajiri Kwa mishahara Bali tunategemea vibarua kuanzia kukoboa,kusaga na hata kuuanika na kuuza pumba( ndo maana ukienda nunua pumba au ukienda mbagala kununua mchele au unga unakutana na gharama ya ubebaji au kupimiwa.
Challenge kubwa ni ni soko ambalo wengi wetu tunafanya kimazoea ni wachache Sana ambao wamebadilika na wanaenda kisasa kuendana na soko lakini Siri kubwa chakula hatuaez Acha Kula. Tena mahindi yanapopotea kwetu n neema.
Gharama ambazo kwangu naona ndo ngumu ni zile za mwanzo kama ununuzi wa mashine, usajiri was kampuni, ujenzi uingizaji wa umeme.
Tukija upande wa pili kinachowashinda wengi ni pale mwanzon unataka uwaachie watu wakufanyie weww uletewe mauzo hutayapata sio dalala hiyo.

Naongelea kitu ambacho nalijua kama unapesa njoo nikupe location usajiri kila kitu Kwa jina lako nipe mwaka mmoja nikupe hela yako
 

Attachments

  • IMG_20190829_080622.jpg
    188 KB · Views: 20
  • IMG_20190829_080625.jpg
    158.9 KB · Views: 18
  • IMG_20170316_140109.jpg
    234 KB · Views: 19
Mimi wakati mimi nilikua nahitaji mkopo wa 2.5 mil nikakosa Daaaahhh...!
Kwa ujumla benk za Tanzania pamoja na mengine hawajakaa kibiashara. Imekuwa kupewa mkopo ni kama msaada. Matokeo yake wanajikuta hakuna jipya wanalofanya, wamebaki wanategemea wafanyakazi. Walau Kwa sasa Mimi naona equity bank wanajitahid kusaidia Kwa watu wa Hali ya chini.
 
Equity nina Account kule ila sijui kama watanikopesha maana nataka niepukane na utumwa huu
 
Equity nina Account kule ila sijui kama watanikopesha maana nataka niepukane na utumwa huu
Ili mradi use kajibiashara hata kama ni genge pia ujitahid kuweka kamzunguko hata muda wa miezi mitatu. Ukifanikiwa hapo utapata tu. Ila kama ndo unaanza nakushauri tafuta watu muunde kajikundi muende mkakope kama kikundi ingawa Kwa hicho kiasi unachotaka itakuwa ngumu.
 
Tatizo mwajiri wetu nae roho mbaya, hataki kitudhamini kwenye hizi Bank ili tukope yaani yeye naweza sema anapenda kuona tukiwa watumwa wake tu

Hivi hawa NSSF huwa hawatoi mikopo?
 
Mimi wakati mimi nilikua nahitaji mkopo wa 2.5 mil nikakosa Daaaahhh...!
Huo mkopo sio wa kwenda Bank. Ndugu zako 2 tu wanaweza kupa hio na ukarudisha bila riba. Shida wengi hamuaminiki. Nilimpa jamaa bodaboda aendeshe arudishe tu nusu ya hela (mdogo wangu) hadi leo sijamsikia nimeamua kukaa kimya.
 
Una uelewa kiasi gani kuhusu biashara?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…