Bar punguzeni volume ya mziki, mnafukuza wateja

Upo sahihi mkuu. Kuna kipindi nilianza kwenda bar za hotelini, huwa tulivu sana mnaongea mziki wa chini.

Sasa unaenda bar ukiamka sauti inakwaruza kisa kuongea kwa sauti. Ila siku hizi niko likizo isiyo na kikomo ya kunywa.
Sawa kabisa Mkuu. Bar za Hotelini poa sana. Ingawa bei ya bia inakuwa juu kidogo. Safi sana pale
 
Ukienda Bar zinazopiga mziki wa band utaweza kweli?
Bar raha yake mziki ndio shangwe linanoga!Kama una maongezi nyeti,nenda lounge!
Bar kama ina live band inajulikana na kueleweka ukubwa wa kelele. Sasa bar hiz hata kwa mziki wa kusukumia kinywaj huku mkibadilishana mawazo hapo ndo naona wanazid. Yan hata mech live tu masauti kama yote. Unalazimika kutengeneza undugu na simu tu!
 
Ni changalamkaa kwa kweli maana lazima utaongea kwa kupayuka ili msikizane na kuwasiliana kwa simu ndio balaa.
 
We tatizo unaenda kufanya vikao bar ndio maana inakuwa ngumu kusikilizana
 
Ukiwa unapata moja baridi moja moto na pembeni kuna kale kanyama ketu lazima usindikizwe na kamziki fulani hivi sasa wewe mleta mada ukitaka mziki mduchu nafikir sehemu nzuri ni lodge mnafanya mambo yenu kimyakimya
 
Mimi nadhani watanzania tunapenda kelele,

Kuna baadhi ya ofisi unakutana na kelele, kila mtu anazungumza na simu yake na wengine wanataniana tu , mara stori za simba au yanga, au Man u au Arsenal.

Ukienda kwenye nyumba za ibada nako vile vile, si misikitini wala makanisani.

Ukienda kwenye stand za mabasi, kule unakutana na balaa jingine la wakatisha tiketi.

Ukiwa kwenye usafiri wa Uma nako kelele ya ama radio, mazungumzo ya watu au Tv.

Hii nchi kiufupi hakuna mahali unaweza sema you can have a piece of mind it is chaos every where.

Tubadilike.
 
Ukiwa unapata moja baridi moja moto na pembeni kuna kale kanyama ketu lazima usindikizwe na kamziki fulani hivi sasa wewe mleta mada ukitaka mziki mduchu nafikir sehemu nzuri ni lodge mnafanya mambo yenu kimyakimyahoja hapa sio

Ukiwa unapata moja baridi moja moto na pembeni kuna kale kanyama ketu lazima usindikizwe na kamziki fulani hivi sasa wewe mleta mada ukitaka mziki mduchu nafikir sehemu nzuri ni lodge mnafanya mambo yenu kimyakimya
Sina tatzo na uwepo wa mziki. Hoja yang ni mziki aina ya kelele na vurugu kias kwamba hamwez kusikilzana wakat si club pale. Au hali ilivyo hujichanganyi bar zetu tena ziko nje pa waz. Mziki mtam ni uendane na mazingira yake. Mzik wa club unajulikana na wa bar unajulikana. Mbaya zaid hata kama mnaangalia mechi saut ni vile vile juu. Kila ukahamia bar ingine unakuta ni tabia ile ile.
 
Kwakweli mimi nilishazoea,na hii ni kwasababu huwa napenda kwenda kwenye live band karibu kila weekend!
So hata nikienda bar za kawaida,naona kawaida tu!
 
Mimi bar za kelele siendagi kabisa , nikienda nimealikwa company naweka earphone maana hatusikilizani ni kunywa tu na kuimba
 
Sheria zipo sema tu wazee wa mitano Tena hawashtukia waanze kukusanya pesa.
 
Hahahah miziki mingi ya bar ni nyenze. Kuna bar moja tu ndio nimewahi kukuta mziki wake uko balanced sio wa kukera masikioni. Hio bar iko Changanyikeni.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] mzee umenichekesha sana eti nyenze duh hatar sana iyo midudu nyenze ina mikerere mtaa mzima amsikilizani sema amna jinsi bar nyingi makerere ndio maala pake so tuvumilie tu
 
Mkuu unachokisema upo sahihi juzi kati nilikuwa nacheki mpira bar fulani yan dar kerere kama zote hakuna chochote tunachosikia kwenye mpira so bar nyingi ndo zipo ivyoo
 
Wewe utakuwa unakunywa maji, maana wazee wa kugonga vyombo hizo kelele huwa hawazisikii kadri muda unavyoenda. Sana sana huwa zinawasaidia kutunza siri maana huwa hawawezi tena kunong'ona siri bali huwa wanaongea kwa sauti za juu vitu vikishapanda kichwani.
 
Mimi bar za kelele siendagi kabisa , nikienda nimealikwa company naweka earphone maana hatusikilizani ni kunywa tu na kuimba
Ukivaa headphones kweli unapunguza vistereo vyao. Tatzo ni huu ubunifu wa kuweka ma dj na hata kareoke ni kama wako ki ulimbuken. Kuonyesha wanafaa hata studio au production au wao kuwa wasanii pia. wameangalia upande mmoja tu bila kujua bar ni zaid ya kunywa na mziki. Ndo sehem ya miaka nenda rud kwa watu wazima kubadilishana mawazo chanya na kufahamiana. Asiyeenda bar akubar anapunguza chances za connections muhim sana.
 
Natumia mvinyo kaka. Natii kanuni ..in vinus veritas. Labda Tofaut kubwa kat yang na wewe ni kuwa mimi nakunywa responsibly!
 

Nilidhani jambo hili litasimamiwa na NEMC, lakini na wao ni kama hamnazo vile, kelele kila mahali kwenye maeneo ya makazi ya watu na wao wanaishi maeneo hayohayo lakini hawaoni wala hawaguswi na adha hizo, huwa sielewi kwanini wanalipwa mishahara bila kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…