KERO Barabara Bariadi kwenda Itilima ni hatari, wananchi tunateseka, TANROADS - Simiyu hamuioni?

KERO Barabara Bariadi kwenda Itilima ni hatari, wananchi tunateseka, TANROADS - Simiyu hamuioni?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150
1000029900.jpg

Huu ndiyo mwonekano wa Barabara kutoka Wilayani Bariadi kwenda Wilayani Itilima Mkoa wa Simiyu, hii Barabara ni hatari Kwa Sasa imekuwa kero kubwa kwetu wananchi.

Barabara imejaa mashimo kuanzia Bariadi hadi Itilima, Kwa Sasa tunasafiri Kwa muda wa saa mbili wakati ni mwendo wa Dakika 30 Kwa gari.

Kwa hali ilivyo mbaya, akibebwa mjamzito akapitishwa kwneye hii Barabara lazima ajifungulie njiani, kama ni mgonjwa mahututi hawezi kufika akiwa hai.
1000029894.jpg


Barabara inakera sana hii, inatesa ukipanda gari, hatujui kama wahusika wanaiona, tumezoea imekuwa ikifanyiwa ukarabati kila inapoharibika lkn Kwa Sasa muda mrefu imefanyiwa.

Tunajiuliza kwani sisi wananchi wa Simiyu hatulipi Kodi kwenye hii inchi? Au huku kwetu hakuna viongozi wa Serikali, au hakuna wahusika ambao ni Tanrods?
1000029910.jpg


Toka kiangazi Barabara imekuwa mbaya sana mpaka Leo masika yameanza haipitiki hata kidogo, wakati ni barabara ya kiuchumi kabisa.

Barabara imeharibika vibaya sana, tunawaomba wahusika kutengeneza, ni barabara muhimu sana lakini inatutesa wananchi.
1000029907.jpg


Kuona matengenezo bofya hapa ~ Barabara ya Bariadi - Itilima Mkoani Simiyu iliyolalamikiwa na Mdau yafanyiwa maboresho
 
Back
Top Bottom