Barabara ya 12, Tanga: Inadaiwa Polisi na Zimamoto wamempiga mtu mmoja aliyesaidia kuzima moto

Mkuu samahani yaani ukae nyumbani kwako askari wakufate wakupe kichapo bila sababu ndio imetokea hivyo au ni tofauti kidogo.
Kwa Askari wetu huu utaratibu ni wa Kawaida sana Mkuu.. Hata kama umelala kitandani na Mkeo, wakiamua wanaweza wakakuamsha na Mateke..

Na wakakupeleka kituoni na wakiamua wanakubambikia kesi kwamba wamekukamata kwenye Tukio la Ujambazi.. Na wataonyesha silaha ambazo watadai wamekukamata nazo..
 
Kwa muktadha wa tukio hilo. Ninachoona ni kuwa huyo muhusika amepigwa kwa kuwa ametoa msaada wa haraka kwa kuokoa mali na uhai wa jirani yake, kwa kuwa ndio mwenye kisima cha maji.

Sasa baada ya wao Zimamoto kuchelewa na kukuta tukio limeisha, wananchi walipoanza kuwapopoa, ndipo wao wakamsaka muhusika ambaye amesababisha wao kuonekana sio weledi.

Ndo wakampiga na kumjeruhi hivyo, hii yote kwa kuwa amefanya kazi nzuri iliyopaswa wafanye wao, na kuwa amewaonesha kuwa wao ni wazembe na kuwatia doa ktk uweledi wa kazi yao.

Wema huponza. [emoji25][emoji25][emoji25]

Hapo zimamoto wachukuliwe hatua kali za kisheria.
 
Acha uongo ww kama Huna cha kuandika kaa kimya mmekalia kuchafua jeshi letu tu .
 
Kupopoa mawe jeshi la wazima moto ni sawa?
 
Kupopoa mawe jeshi la wazima moto ni sawa?
Si sawa kabisa,
Ila wao kupiga na kisha kutoa fidia ya ths 30,000/= ni sawa?
Usije ukasema walikuwa wanajihami,
Itakuwa ni sawa na waisraeli na wapalestina? Mawe kwa mizinga? 🤣
 
Nakazia
 
Wakati tupo Iyunga Polisi walimuua "MICHAEL SIKUPYA" wakati ndio alikuwa anawasaidia kutuliza mgomo wa wanafunzi.

Hivi vyombo, ovyo saaana!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…