Baraka da Prince kipaji kinachoangushwa na kiburi

Hemed nae nati imelegea
 
1:Nimekoma
2:siwezi
3:siachani nawe
4:Acha niende 5:Nisamehe
6:Sometimes
7:Nivumilie ft Ruby
8:Jichunge
9:Sina ft Madee
Chalii anakipaji kinyama,,sema kiburi na hasira za kimbanga zinam'cost mjamaa
Ongezea na Naogopa aliyoshirikishwa na Mirror,mule ndani dogo alitulia sana.
 
Huyo jamaa ni bonge la Talent, ila ana altitude kama za Nikki Mbishi, sasa kwa soko letu la muziki lilivyo bila kuwanyenyekea watu fulani huwezi kufanikiwa, jifanye bwege ufanikiwe
 
Ana nyimbo nzuri Nisamehe, siachi nae n.k na kuna alizoshirikishwa kafanya poa. Bora iwe na DJ RJ naipenda sana
 
Huyo jamaa ni bonge la Talent, ila ana altitude kama za Nikki Mbishi, sasa kwa soko letu la muziki lilivyo bila kuwanyenyekea watu fulani huwezi kufanikiwa, jifanye bwege ufanikiwe
Yeah nikki mbish ndo kabisa yule jamaa kila kitu kwake anajua yupo juu siku zote
 
Hakukuwa na haja tena ya kwenda kwa Ali ikiwa alikuwa anafanya vizuri sana na label ile ile ilikuwa inamgharamikia vizuri .

Istoshe alipata mafanikio zaidi akiwa label hiyo..
Mafahari wawili hawakai zizi moja..
Rejea mavoko na chibu
Maelezo Yako mbona hayaonyeshi hilo Kaburi? Baraka hakua chini ya kiba wala hakua kwenye label ya kiba..

Inshu ya mavoko kua chini ya Diamond ni tofauti kabisa na Kiba na Baraka,..
 
Maelezo Yako mbona hayaonyeshi hilo Kaburi? Baraka hakua chini ya kiba wala hakua kwenye label ya kiba..

Inshu ya mavoko kua chini ya Diamond ni tofauti kabisa na Kiba na Baraka,..
Baraka alikuwa chawa tu wa Kiba [emoji38][emoji38]
 
Maelezo Yako mbona hayaonyeshi hilo Kaburi? Baraka hakua chini ya kiba wala hakua kwenye label ya kiba..

Inshu ya mavoko kua chini ya Diamond ni tofauti kabisa na Kiba na Baraka,..
Sasa unataka nikuoneshe kaburi?? Lipo uko makaburini.
Baraka alikuwa rockstar 5000 ambayo alikiba ni moja ya viongozi pale huoni kuwa ni bosi hiyo..

Elezea ishu ya mondi na mavoko kama unajua ili nikikukamate vizuri hapa
 
Sasa unataka nikuoneshe kaburi?? Lipo uko makaburini.
Baraka alikuwa rockstar 5000 ambayo alikiba ni moja ya viongozi pale huoni kuwa ni bosi hiyo..

Elezea ishu ya mondi na mavoko kama unajua ili nikikukamate vizuri hapa
Unauelewa mdogo sana kuhusu haya mambo..

ndo ubaya wa ku-copy mada na kuja kupost huku, unashindwa kujenga na kutetea hoja...

Umesema Baraka alijichimbia kaburi baada ya kua chini ya kiba, Ndo uelezee alijichimbiaje kaburi? Au umeropoka tu kwa ushabiki wa kiteam..

Rich Mavoko alikua chini ya Wcb label na Boss alikua Diamond.

Baraka alikua Rockstar Ambayo alikiba hakua Boss Wake na wala kazi zake zilikua azisimamiwi na kiba,

ni Kama Dimpoz Yupo chini ya Rockstar ila kazi zake hazisimamiwi na kiba na mbona kufanya vizuri kwa Dimpoz mpaka kuchukua tuzo ya kimataifa mbele ya Mond hamkupongeza kiba? Kama mnaanza kumlaumu kiba kuhusu baraka msifieni kuhusu Dimpoz...
 
Baraka alikuwa chawa tu wa Kiba [emoji38][emoji38]
Kumbe unajua mkuu, sasa huo uchawa alitaka kuupeleka Wcb wakamtumia then Wakampotezea anakuja kustuka hana sapot kama aliyokua anaipata kwa team kiba,.


Wcb hawawezi kukupa sapot kama haupo chini ya label yao yani hawatoki kik hata ujipendekeze Vipi, Angali kabla mond hajawa na hawa mameneja alikua na msululu wa wasanii chawa na walikua wanapata sapot ya team mond na walikua wanapata corabo na jamaa kirahisi sana, sa hizi hiyo nafasi haipo

Baraka alichezea hiyo nafasi ya kupewa sapot na team kiba, Angalia Dimpoz alizingua kwa Mond anapata nafasi kwa team kiba maisha yanaenda
 
Nimegundua kitu kwamba sio kila MTU mzima ana akili wengine hawana wewe ni mfano wake..

Niko hapa toka wakati upo Instagram so hata kubishana. Na wewe ni kujishushia hadhi..

Kwanza onyesha sehemu niliposema kiba alikuwa anasimamia kazi za baraka .na alikuwa bosi wake ..nilisema kiba ni moja ya mabosi hapo rockstar najua hujui..
Na sio kwamba alikuwa anasimamia kazi za baraka.

Baraka alibweteka baada ya kutua apo rockstar tofaut na alipokuwepo royal nsyepa.lebel iliyomkuza ..na alipata tuzo ya msanii bora chipukizi akiwa hapo...

Alipoenda Rock star ni kama aliridhika na kuona kamaliza kazi..
Hii nayo ili apply kwa mavoko ni uvivu na kujiona umemaliza.kazi.

Lakini ukakimbilia eti " onyesha kiba alipohusika kuanguka kwa baraka"..

Kwani wapi nilisema kiba ndo alimuangusha baraka??

Walimu wako wana hasara sana kaka
 
πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…