Baraza Jipya La Mawaziri hili hapa

1. Nakubaliana nawe kwamba sitamani kuona huyu mama Simba kama waziri but I have nothing i can do.

Kasheshe,

Naskia watu wanasema Mzee hupumzika pale- hivyo hawezi kumwacha asimpe uwaziri kirahisi tu hivi2!
 
DR.Mwinyi na DR Nchimbi wizara ya ulinzi??hawa vijana wataweza kusimamia maswala ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama??
Sitaki kuamini sasa hivi kwamba kuna jipya,Time will tell

Baraza kwa ujumla wake naona bado, matarajio tuliyonayo ni makubwa zaidi, lakini naona hii ni hatua, ni bora kuliko la awali. Kama ni mwanafunzi alikuwa kwenye F sasa kasogea kwenye D (tunataka A au angalao hata B basi).

Lakini sikubaliani na suala la kumhukumu mtu kutokana na umri pekee. Kuna ushahidi gani kuwa mtu akiwa na umri mdogo hawezi kuwa waziri wa ulinzi? Salim Ahmed Salim alipoteuliwa kuwa waziri wa ulinzi mwaka 1985 alikuwa na umri wa miaka 40, je huu ni umri mkubwa? Umri wa Dr Hussein Mwinyi ni miaka 41. Sasa kwa nini wa miaka 41 aonekane "kijana" kwa hiyo ati "hawezi" wakati wa miaka 40 aliweza? Hata marehemu Edward Sokoine aliwahi kuwa Waziri wa Ulinzi miaka mwishoni ya 1970's akiwa kwenye early 30's, na alifanya kazi nzuri sana tu. Kwa nini Nchimbi mwenye late 30's ashindwe? Kumbukeni ninachopinga hapa ni hili wazo la kudai ati "vijana" hawawezi maswala ya majeshi yetu. Kuweza masuala ya majeshi hakutokani na umri, ni mengi zaidi ya hapo, tuyajadili hayo tusianze kubagua kwa msingi wa "ujana".
 


Is True kwamba Mathayo David ni mtoto wa nje wa Msuya?

Kwamba huyu jamaa PhD yake ni Fake nilisha wahi zipata sehemu lakini sikuwa na uhakika.

Kwa nini watu waliofoji Elimu Vihiyo wakubwa wankubalika serikalini?

Hii kweli ni serikali ya wasanii.

Huyu Mama mke wa mtu na adabu zake zote alikuwa akimvulia kaptula Rais mstaafu Ben Mkapa.

Halafu nikisema umalaya ni hatari kwa maendeleo ya taifa watu mnabisha na kwa uchungu mnataka hata kula nyembe mpya na sime za kimasai.

Umalaya wa viongozi wetu unatugharimu mamilioni.
Viongozi wetu wanatumia kuni zao vibaya matokeo yake wote tunabebeshwa gharama.
 

Nadhani hapa mnachanganya vitu viwili tofauti; ubora wa chuo kikuu cha Dar es Salaama na kiwango cha elimu ya juu kwa Watanzania.

Ukweli ni kuwa chuo kikuu cha Dar es Salaam ni chuo bora sana kuliko vyote katika eneo hili la Afrika ya Mashariki na ya kati. Kina waalimu wenye sifa na uwezo kwa viwango vya kimataifa na hata viwango vya mitaala yake ni vya kimataifa. Kuna vyuo vingi sana kwenye eneo letu hili vina waalimu wenye masters tu ambao hawawezi hata kujenga mada kwenye kongamano za kimataifa kwenye taaluma zao; kwa hiyo hawatambuliki kimataifa na hivyo kuathiri ubora wa chuo hata kama wanajua kufundisha mambo ya vitabuni.

Hata hivyo, lazima tukubali kuwa idadi ya watanzania wenye elimu ya juu kwa ubora huo wa UDSM siyo wengi sana. Kwa muda mrefu chuo kikuu cha Dar kilikuwa kinatoa wahitimu wapatao mia nane tu kwa mwaka, wakati majirani zetu walikuwa wakitoa wahitimu wapataio elfu tano kwa mwaka. Ukilinganisha wahitimu wa elimu ya juu na ubora wao kwa kila kaya, utaona kuwa Tanzania tunashika mkia katika eneo letu hili. Wataalam wetu wengi wamekuwa na digrii za kununua tu
 

Nungwi, good to see you back.
Kaswali kadogo tu,
Kwani hawa watoto wa prof vipi PhDs zao?
 
Kwanza napenda kutumia fursa hii kumpongeza Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Watanzania, kwa kutumia ujasiri wa nguvu wa kuleta mabadiliko haya, vilevile kuwapongeza Mawaziri wote waliochaguliwa kwenye safu hii ya kihistoria. Ni mategemeo ya wengi kuona kwamba safu hii italeta uadilifu na imani ya kweli, itadumisha uadilifu huo na imani zake.

Maoni: Kwa wana JF Shughuli bado ni pana-Tutafika, dhamana ambayo safu hii mpya inayo ni kubwa kuliko-unimaginable-Tuwape mda kwani wao wametusikiliza, wamesikia manung'uniko yetu, sasa huu ni mda wa kuipa safu hii Nguvu mpya ambayo haijawahi kutokea katika majukwaa ya siasa Afrika!

Asante.
 

Asante sana kwa maelezo mazuri. Wengine hapa naona wako kutukana na kutoa matusi kwa nchi yao bila kusifia hata vile vidogo vizuri tulivyonavyo.
 
Asante sana kwa maelezo mazuri. Wengine hapa naona wako kutukana na kutoa matusi kwa nchi yao bila kusifia hata vile vidogo vizuri tulivyonavyo.

Hivi kuna matusi zaidi ya kiongozi wa nchi kushiriki kikamilifu kuutafuta umasikini kwa undi na uvumba na kuusimika Tanzania?

Au kwako Matusi mpaka itajwe Kaptula?
 
Asante sana kwa maelezo mazuri. Wengine hapa naona wako kutukana na kutoa matusi kwa nchi yao bila kusifia hata vile vidogo vizuri tulivyonavyo.


...acha upuuzi wako hapa,unataka tusifie visivyosifika kwa sababu ni TZ tuu na ushaona watu kutafuta fact ni matusi kwa nchi yao au vipi?
 

Ndugu yangu Nungwi vipi, mbona unapatikana kwa nadra sana siku hizi? Usisahahu kijiwe chetu mzee; ndicho kinaibua mambo mpaka jamaa wanaona viti vyao vinawaka mioto.

Nimefurahi sana kwa observation yako hapo juu hasa kuhusu hao vihiyo wenye PhD feki.
 
...toa data la sivyo stop misleading people kwa sababu unachoongea ni contrary na data zinazotumika kupima ubora wa elimu ya juu!

Koba, unachobisha ni kipi hasa? Mfano mdogo ameshakupa YN, sasa unataka nini tena? Evidence is always both qualitatively and quantitatively attribiutable! Sisi tuliopo katika career hii ya elimu ya juu tunajua na wenzetu wakenya na waganda wanajua hivyo kwamba sisi kwenye mambo ya academics tupo juu. Na hapa sisi tunaongelea ubora wa elimu, sio wingi. Kwa wingi ni sawa wametuzidi kama vile ambavyo wametuzidi kila kitu katika wingi isipokuwa idadi ya watu. Ukiacha hiyo data aliyokupa YN, sisi tuna PhD holders wengi kuliko wao, tuna academic journals nyingi kuliko wao, tupo cited zaidi kwenye international journals kuliko wao, our standing in intenational academic fora ipo juu kuliko wao, tuna mitaala bora kuliko wao, you mention every aspect of quality higher education tunawazidi. Unapokuja kwenye academics kupata kazi katika international scientific organisations sisi tupo juu, ndio hao akina Tibaijuka, Mgongo, Lipumba et al wanatuwakilisha. Isipokuwa inapokuja kwenye kazi za kupitia mlango wa nyuma tupo nyuma kwa sababu watanzania sio kasumba yetu kutafuta vitu ambavyo hatuna sifa nazo. Sasa wewe umeng'ang'ania idadi ya mavyuo, wenzako wanapopima ubora wa vyuo hawahesabu idadi ya vyuo wanaangalia quality, na quality inapimwa kwa knowledge production and intellectual contribution-na hivi vitu vinaangaliwa kwa vigezo kama vya hapo juu.

Ni kweli watz tu wanyonge katika mambo kibao, lakini sio hili la ubora wa elimu ya juu, hili hapana. Pale tunapofanya vizuri kidogo tusisite kusema na kujipongeza. Waswahili wanasema "You cannot be inferior unless you feel that you are inferior"!
 

Sawa. Ila, Mbona humsemi Che-Mkapa mume wa mtu na adabu zake kwanini alikuwa akimvulia kaputula mke wa mtu? Au ni kina mama tu huwa ndio wanaovuaga? Wanaume je, hawajuagi? Au tendo la namna hii ahukumiwaye ni mtu wa jinsi ya kike tu? Kazi ipo!
 

Kitila,

Kwa hali halisi Tz- tuangalie zaidi quality or quantity? Suppose you can not have both- je tuanze na kipi?
 
Kitila,

Kwa hali halisi Tz- tuangalie zaidi quality or quantity? Suppose you can not have both- je tuanze na kipi?

that was eazy...!! of course quality! kwa jinsi mambo yalivyo na mwamko wa vijana in ten yrs, will be on the mountain top!!.
 
Wenzangu wanaJF, kiasi napoteza mwelekeo, inaonekana pana mada mbili tofauti zinajadiliwa hapa. Ikiwezekana, hii ya ubora wa elimu/universities ifunguliwe sehemu nyingine, hapa tubaki na hii ya baraza jiya la mawaziri.
 

Uko sahihi kabisa, Mh. Rais ana imani kuwa aliowateua watatimiza wajibu wao kama ambavyo wanatakiwa kufanya.
Mimi binafsi nimefurahia baraza jipya na sina tatizo almost wote wana uwezo wa kufanya kazi vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…