Baraza Jipya La Mawaziri hili hapa

Baraza Jipya La Mawaziri hili hapa


"kwa sababu kufanya tofauti rais ilikuwa either achukue viongozi toka upinzani, au arudishe wazee kwa sababu kama ni ccm tu, aliowachagua ni almost all we got kwa mtizamo wangu",


Tatizo linaaanza kwa wananchi kwa nini wachague viongozi wasio na sifa kiasi cha kumpa Rais kazi hivyo ?
 
Kwangu although Waziri/Deputy anachangia sana katika ufanisi/utendaji wa Wizara, Katibu Mkuu ndiye ambaye amekamata mpini!!! Kwa mawazo yangu (I stand to be corrected on this) ni kwamba kwa kweli kwenye wizara nyingi ambazo zipo goigoi ni maPS ndio wanalete rongorongo..... Mifano ya haraka ni pale Fedha, Viwanda n Biashara, Energy, Afya, Miundombinu zamani, Elimu ya Juu etc..... Kwa muangalio wa haraka haraka nilichogundua ni kwamba most of these posts tumewapa "non-professionals in the field"... Hii imekuwa more political!!

Absolutely, Morani! Bila kuwa na makatibu wakuu walio competent, wenye msimamo usioangalia ideology na wenye uwezo wa kutoa ushauri bila woga na kusimamia principles tutakuwa tunampigia gitaa mbuzi! Tunahitaji watendaji ambao hawatakubali kuyumbishwa na wanasiasa.
 
Rais J.Kikwete hakufaulu kuunda baraza la mawaziri ambalo wananchi walilitaka. Wanachi walitaka sura mpya sio zile zile za zamani ambazo zimezungurushwa tu na kupewa wizara nyingine. Katika wizara ya afya ni wale wale.
Kitendo hiki cha rais j.Kikwete ni dharau kubwa sana kwa wananchi ambao walimchagua. Kuna wabunge chungu nzima wa CCM ambao hawana madowa ya ufisadi. Kuna wabunge pia wa upande wa wapinzani ambao hawana madowa ya ufisadi.

Wakai kama huu rais J.Kikwete alitakiwa kuunda serikali ya MSETO ili ikabili matatizo ya nchi kama UMASIKINI, UGONJWA(HIV), UBADHIRIFU,UJAMBAZI NA UFISADI.

Tukumbuke kwamba Mzee Nyerere pia alikuwa na serikali ya MSETO. Lile Baraza la Mawaziri katika serikali ya 1961 tulipopata uhuru (Tanganyika) lilikuwa ni la MSETO.

Hii inaonyesha wazi wazi kwamba rais J.Kikwete ameshindwa kuiongoza nchi yetu na wakati wake umefika kujiuzulu kama vile alivyojiuzulu PM. Lowasa. Ama sivyo ile tume yake ya MIKATABA YA MADINI itakuja kumangusha mwenyewe kwani yeye pia yumo katika ufisadi wa mikataba ya Madini. Alikuwa ni waziri wa Nishati na Madini hapo awali.
Wenzake wote wamejiuzulu bado yeye tu.

HILI NI BARAZA LA MAWAZIRI LA DHARURA TU. Tumuulizeni J.kikwete HAKUNA WATU WENGINE BALI NI HAO HAO TU TANZANIA ambao wanaweza kazi za uwaziri?
 
Time will tell,nasema tuwape muda wakati tukiendelea kumkoma nyani giladi na kuwafuatilia kwa karibu sana.
 
Time will tell,nasema tuwape muda wakati tukiendelea kumkoma nyani giladi na kuwafuatilia kwa karibu sana.

Kati ya picha zilizonifurahisha ni hii ya Mama Megji na Karamagi. Inasema mengi sana. Inata huruma mama kama vile anasema jamani mimi niliingizwa mkenge tuu na Balaa hili.

http://mpoki.blogspot.com/
 

Attachments

  • Why.jpg
    Why.jpg
    22.2 KB · Views: 125
..te Teh Namimi Niliona Alipomgusa Yule Binti Begani..kila Mtu Na Hobby Yake Si Mnajua Rais Wetu Anawapenda Warembo[na Mama Yupo Safarini Korea]...teh Teh..

Ehee Vipi Pale Alipowaambia Wambadilishie Kiti......machale Yalimcheza Nini...wasije Wabaya Wakawa Walimwendea ...kunako ..mngeshangaa Mnasikia Mara Sauti Inakauka Ghafla ...ukizingatia Alishaahirisha Kutangaza Mara Mbili..angeahirisha Tena...uzuri Aliona Kabisa Kiti Kilikuwa Hakifai...kaaga Bwana!!! Yupo Fit!!! Teh Teh...
 
Naomba nichukue nafasi hii kumponda rais JK kwa baraza mbovu na ya kiushikaji aliyouweka.
Siwezi amini kwamba wana_JF mnasema tuwape muda? wa nini?
- Ni sura ngapi mpya zilizoongezwa kwenye baraza? 3 au 4
- Wengine waliobaki wote walikuwa kwenye cabinet iliyopita, je walitenda kazi ipasavyo, waliboronga au they just lived through another day? Watendaji wazuri walikuwa 2 au 3 by anyone's estimate kama vile Magufuli. Wengine walilala tu au kusimama kusema ujinga. Kati ya waborongaji wa kubwa waliobaki ni Chiligati (labor market is a chaos!), Wassira (wakulima wa korosho watamlaaani milele) etc
- Sura mpya zinasemaje? Dkt Mwinyi mnayemsifia eti mchapakazi,mmh, na hiyo digrii yake feki hata madaktari enzake Muhimbili hawakumkubali. Nchimbi ndo huniambi kitu! Eti mnataka kuwalinganisha Moringe Sokione and Salim Ahmed Salim na hawa? PLZZZZ
- Kaendeleza ule ushikaji wa kulipa fadhila. Malima? Kalipwa fadhila kwa ajili ya kuwa 'attack dog' against Mengi? Na alidhihirika kusema uwongo bungeni! Integrity : 0!
- Kupunguza cabinet haikuwa mjadala, he just went back to the good old days, alicho'tunga' ukubwa wa cabinet in 2006 kwa ajili ya ushikaji, kairudisha katika hali yake ya Mkapa era. Nothing creative about it. Na elimu kazidi kuboronga eti kaunganisha Elimu ya Juu na Elimu ya msingi+sekondari+ufundi. Alafu kaongeza District Education Officers wawe wawili kila wilaya, sasa hii si kuongeza gharama!? Kapunguza nini?
- Yaani simalizi list yangu

Kusema eti tumpe muda, wa nini? Tunarudi palepale, kwa miaka 2 waandishi na baadhi ya watu pamoja na upinzani wamepiga kelele kwamba nyumba inaungua, tukajibu wapeni muda, sasa after billions of loss and poor infrastrucure and all the crap, tunashangaa how did we get there! Ni hii 'tuwape muda!"
Hii cabinet ni mbovu na ya kushikaji. Na it will not last more than 1 year!
Tuache unfaiki na ushabiki usio wa maana na tufuate aliyosema Anna Kilango, hapa si muhimu chama bali uzalendo!
 
Hapa mkuu tuko pamoja ila nina haya machache ya kuongeza:

-Kuwaweka watu kama Nchimbi na Husein Mwinyi kwenye wizara muhimu ya Jeshi letu la Ulinzi na kujenga Taifa ni kulidharau jeshi hilo ambalo ni chombo muhimu sana kwa Taifa letu hasa katika kipindi hiki ambacho karibu majirani zetu wote wapo kwenye vita au machafuko ya kisiasa.
-Inaelekea JK bado hajaona umuhimu wa kupunguza timu yake pamoja na ushauri wote aliopewa.Nchi kama Tanzania kweli haipaswi kuwa na wizara zaidi ya 15!!kuwa na wizara zaidi ya 25 ni mzigo mkubwa sana kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

-Naona mawaziri wengi wamewekwa si kutokana na uchapakazi au ufanisi au uwajibikaji au usafi bali ni sera zilezile za ushikaji,urafiki,kusoma pamoja,kuoneana haya na bila kuzingatia zile sera za ari mpya,nguvu mpya na kasi mpya!.Hebu tuchukulie mfano wa Prof.Kapuya kweli huyu mtu anatufaa?? je kweli uchapakazi wake unaridhisha? mtu huyu kila kukicha anawaza kununua vipanya ili apeleke kule ISAKA-Shinyanga mpaka sasa ni mtu mwenye vipanya vingi kule ISAKA sasa swali linakuja kavipatapataje?????

-Kumpeleka Prof.Mwandosya wizara ya maji badala ya wizara ya Sayansi na Technologia ambako ndiyo mtaalam huko ni kukoroga mambo tu! Sijui ni kigezo gani kimetumika hapo..hebu nielimisheni.

-Kumuondoa pombe magufuli wizara ya ardhi ambapo alionekana kupamudu kabisa na kuweka mtu mwingine nikukaribisha lile wimbi la wageni kujitwalia tena ardhi yetu huku watanzania tukiendelea kunyanyasika.

Wembe Mkali
NI WAZI UNAJENGA HOJA ZAKO KTK MSINGI WA CHUKI NA WALA UNA VIGEZO VYA KIHISTORIA WALA UELEWA MPANA WA WAJIBU WA WAZIRI KTK WIZARA,KWA UELEWA WAKO TN INAPASWA KUWA NA WIZARA 15,UMEFANYA UTAFITI GANI KUJUA HILO!UNALOPOKA TU MTU MZIMA.UNASHANGAA MARK KWENDA WIZARA YA MAJI NA UNADHANI ANGEPELEKWA TEKNOLOJIA,KWA TAARIFA YAKO MARK AMEPATA KUWA KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI KWA MIAKA KADHAA NA WAZIRI WAKE ALIKUWA NI JK,HUVYO JK ANAMJUA KULIKO WEWE UNAONGEA BILA MPANGILIO.HAYA NIAMBIE KWA DATA TATIZO LA MWINYI NI NINI WIZARA YA ULINZI?UNA MAANA KAPUYA ALIKUWA NI BORA KULUKO MWINYI?
 
Jamani, mbona mna challenge sana this cabinet? JK angemchagua nani katika pupulation aliyokuwa nayo ya wana CCM ambao kwenye uchaguzi wa 2005 wote walipita kwa Rushwa?

Mimi naomba mnapo challenge mjaribu kutoa mapendekezo yenu ambayo mnaona ni bora, sio just critising without supportings!

Yes, JK angeweza kuwaacha watu fulani fulani km Chenge, Mkullo ambao tuna skendo zao, lakini inawezekena kwa mtazamo wake hao alio chagua ni bora kati ya taka taka zilizo bakia??
 
Mkullo kuwa Waziri wa Fedha imeni dissapoint kweli?

Inasikitisha sana kwa mtu kama Mkullo kuwa waziri wa fedha!hivi huyu rais kweli ana nia nzuri nchi. Angalia maskendo yake pale NSSF ni mdini sana jamaa kama aliyeko sasa (Dau). Uchumi utadidimia kuzimu,jk hajua nani wa kumteua. Kweli kweliii mkuloo,jk isnt serious as always. Mkulo ana kashfa kibao za ubadhirifu na ndio uliomtua NSSF!!Unajua tofauti ya mkapa na jk ni ndogo sana nayo ni: Mkapa aliwatimua mafisadi wote wa enzi za mwinyi (Mkullo,Mataka,etc)na kuunda mafisadi wapya na JK yeye anaua mafisadi wa kundi lake na kufufua wale waliouawa na Mkapa. Ngoma droo. Ni bora kuanziasha wapya kuliko kufufua wafu......
 
Halafu mmepaonaje pale David Mathayo anakuwa naibu wa mwalimu wake Prof Msola? Wakikutana ofisini anaamkia kwanza "shikamoo mwalimu!" ndipo wanaendelea na kazi! Raha, kitu?
 
Nashangazwa sana nauteuzi wa Chenge.

Nasikitishwa sana na uteuzi wa Shamsa Mwangunga kupewa wizara ya utalii na maliasili hivi huyu mama anaweza kweli? ama ni kiupeana vyeo tuu bila kujali uwezo wa huyo anayepewa hicho cheo.

Sioni mwanga nazidi kuona kiza nene mbele yangu na mbele ya taifa langu.

Tanzania bila mafisadi inawezekana ,timiza wajibu wako.
 
mie nashangaa,au Jk amerogwa?kurudi kwa chenge ni kama jinamizi limemtokea Muungwana.
 
Inasikitisha sana kwa mtu kama Mkullo kuwa waziri wa fedha!hivi huyu rais kweli ana nia nzuri nchi. Angalia maskendo yake pale NSSF ni mdini sana jamaa kama aliyeko sasa (Dau). Uchumi utadidimia kuzimu,jk hajua nani wa kumteua. Kweli kweliii mkuloo,jk isnt serious as always. Mkulo ana kashfa kibao za ubadhirifu na ndio uliomtua NSSF!!Unajua tofauti ya mkapa na jk ni ndogo sana nayo ni: Mkapa aliwatimua mafisadi wote wa enzi za mwinyi (Mkullo,Mataka,etc)na kuunda mafisadi wapya na JK yeye anaua mafisadi wa kundi lake na kufufua wale waliouawa na Mkapa. Ngoma droo. Ni bora kuanziasha wapya kuliko kufufua wafu......
Wewe KIFO na ufe na kauli zako za uchochezi. Wewe ndio mdini..tabu yako ni kuona jina la muislamu tu. Wewe kwako kila muislamu ni mdini tu. Labda utupe tafsiri ya udini. Huyu Mkullo hakuna mtu mlevi kama huyu haya tuambie ni udini gani aliufanya akiwa NSSF au pengine. wacha zako Mgala mkubwa wewe.Nyie ndo watu mnaotaka kila wizara ashike JOHN na JESEPH tu sijakusikia ukimtaja Chenge kama hafai au kwa kuwa ni Andrew! baradhuli mkubwa wewe.
 
Inasikitisha sana kwa mtu kama Mkullo kuwa waziri wa fedha!hivi huyu rais kweli ana nia nzuri nchi. Angalia maskendo yake pale NSSF ni mdini sana jamaa kama aliyeko sasa (Dau). Uchumi utadidimia kuzimu,jk hajua nani wa kumteua. Kweli kweliii mkuloo,jk isnt serious as always. Mkulo ana kashfa kibao za ubadhirifu na ndio uliomtua NSSF!!Unajua tofauti ya mkapa na jk ni ndogo sana nayo ni: Mkapa aliwatimua mafisadi wote wa enzi za mwinyi (Mkullo,Mataka,etc)na kuunda mafisadi wapya na JK yeye anaua mafisadi wa kundi lake na kufufua wale waliouawa na Mkapa. Ngoma droo. Ni bora kuanziasha wapya kuliko kufufua wafu......

Hii ndiyo Tanzania bwana... Mkullo akiwa Naibu waziri wa fedha, hapakuwa na Tatizo... Mkullo amekuwa Waziri wa Fedha kamili ... matatizo yapo...

Sikubalini na wengi:

kwamba kama system inafanya kazi vizuri kwa maana utendaji serikalini through makatibu wakuu... kweli waziri anaweza badilisha mambo mengi? (yawe mazuri au mabaya?)... I simply say NO.

Why tunapenda kuongelewa watu na si hoja!!! hapa mkuu wa nchi alisema wakati mkuu akiongelea kuhusu kubadilisha mfumo wa utawala at least kwenye maeneo fulani fulani waandishi wahabari walikuwa hata hawaandiki...
 
Nashangazwa sana nauteuzi wa Chenge.

Nasikitishwa sana na uteuzi wa Shamsa Mwangunga kupewa wizara ya utalii na maliasili hivi huyu mama anaweza kweli? ama ni kiupeana vyeo tuu bila kujali uwezo wa huyo anayepewa hicho cheo.

Sioni mwanga nazidi kuona kiza nene mbele yangu na mbele ya taifa langu.

Tanzania bila mafisadi inawezekana ,timiza wajibu wako.


Uhakika ni kwamba haiwezekani kumfurahisha kila mtu!!! Hivyo nakuomba ukubali tu kwamba CCM ndio wamepewa madaraka na walisha ahidi kupitia kwenye ilani yao... noa kisu subiri 2010...

Hata hivyo mimi nimemwona huyu mama kama miongoni mwa manaibu wachapa kazi sana!!!
 
Baraza la sasa hivi linaonekana kuwa ni dogo ukilinganisha na lililopita. Hivi kweli huyu JK yuko slow namna hiyo na hakuliona hilo tokea mwanzo?
 
a 100% right.......

kwa mtu yeyote ambaye kasoma bongo mpaka 'versity level hasa sisi watu wa science, tunakubali kwamba elimu ya bongo mwisho ktk afrika!!! hata hao nigeria na SA wanatuzidi namba tu ya vyuo, lakini ktk kushusha nyanga tumewaacha flani(forget desa/mkoba...naongelea "ngunju" lenyewe)..tatizo ni kiingereza ndio kinapiga njenga!! wakenya na waganda wanatuogopa sana.

Wakuu,

Lakini hapa mbona ni kitu cha kutegemea? Tanzania tulikuwa na chuo kikuu kimoja kwa muda mrefu sana, kikiwa na wanafunzi chini ya 10,000 kati ya Watanzania milioni karibu 40. Kwa vyovyote wanaosoma hapo watakuwa katika wale best na pia hata walimu watakuwa katika wale best.

Ni rahisi UD kuwa na wanafunzi na walimu wazuri maana wana pool kubwa ya kuchagua. Wakati mwingine kulinganisha nchi na nchi kwa kutumia UD inaweza kuleta picha ambayo sio sahihi sana. Labda kama mnalinganisha chuo na chuo.

Angalia hata shule za secondary, zilipokuwepo chache zile za serikali, viwango vyao vilikuwa juu mno, maana walimu na wanafunzi hawakuwa na sehemu nyingine ya kwenda. Lakini sasa pool ambayo shule wanawezakutumia kuchagua wanafunzi na walimu linazidi kupiganiwa na shule nyingi hivyo kuwa mchezo wa mwenye kupata apate.

Kwenye kulinganisha inabidi tuwe waangalifu, maana kuna factors nyingi zinazoingia katikati, hivyo kufanya mlinganisho huo usiwe fair. Waliosema ili kulinganisha unatakiwa kulinganisha egg for egg hawakukosea.
 
Back
Top Bottom