Baraza la Mawaziri lasema liko tayari kujiuzulu huko Korea Kusini baada ya kushindwa kwa Amri ya Utawala wa Kijeshi

Baraza la Mawaziri lasema liko tayari kujiuzulu huko Korea Kusini baada ya kushindwa kwa Amri ya Utawala wa Kijeshi

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Rais Yoon Suk Yeol ameondoa Utawala wa Kijeshi nchini humo baada ya maandamano ya wananchi na wabunge kupiga kura za kufuta amri yake

Aidha, Msemaji wa chama cha Upinzani cha 'Democratic' amedai uamuzi wa Rais Yoon Suk Yeol wa kutangaza Utawala wa Kijeshi Desemba 3, 2024 ni kitendo cha Kihaini na vyombo vya Sheria vinapaswa kuanza uchunguzi wa kitendo hicho na hivyo kupanga kumuondoa madarakani

Aidha, chama hicho kimepanga kuwashtaki Waziri wa Ulinzi Kim Yong- hyun, Waziri wa Mambo ya Ndani Lee Sang-min na baadhi ya maafisa kwa kumshauri Rais kutangaza Utawala wa Kijeshi

Baraza la Mawaziri limesema liko tayari kujiuzulu baada ya Kushindwa kwa Utawala wa Amri ya Kijeshi nchini humo. Hatua hiyo inafuata baada ya baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais kujiuzulu, leo Desemba 4, 2024 Baraza la Mawaziri limesema liko tayari kujiuzulu
 
Korea Kusini rahaa sana, Intern Doctors walipogoma mwaka huu kushinikiza serikali kufuta sheria ya kupunguza idadi ya wanafunzi wanaodailiwa kwenye kozi ya MD walifutiwa leseni.
Kilichofuata ni Madokta wakufunzi na specialists wote wakagoma na kurudisha leseni zao na kuweka sahili ili serikali kuwarudishia leseni wale intern alafu pia kufuta sheria ya kupunguza idadi ya wanafuzlnzi wanaodailiwa kujiunga na kozi ya udaktari.
Elimu kitu muhimu sana hapa duniani
 
Back
Top Bottom