Baraza la sanaa(BASATA) lasitisha usajili wa Msanii Dudubaya

Baraza la sanaa(BASATA) lasitisha usajili wa Msanii Dudubaya

Sheria zote duniani zinalazimika kufuata na kuzingatia misingi ya 'Haki Asili za binadamu' (Principles of Natural Justice), moja ya misingi mikubwa ya sheria hizi ni haki ya kusikilizwa.

Haupaswi na hauwezi kutoa hukumu ya upande mmoja tu, ni lazima uusikilize na upande mwingine, ni lazima usikilize nini chanzo vile vile.

Basata wameendeleza kuhamua mambo kwa hisia tu pasipo kufuata sheria, kwakua wana uwezo wa kumfutia mtu leseni basi hawaangalii huo utaratibu wao wanajifutia tu, hii sio haki na hapa lazima lifanyike jambo kukomesha upuuzi huu.

Hakuna sheria inayotambua mambo ya hisia, mtu kuumiza hisia zako sio kosa kisheria, dudubaya kaumiza hisia za basata na hili sio kosa la kisheria.
 
Nisaidie kushangaa. Yaani kwa vile ni msanii basi akifanya kosa hata kama halihusiani na sanaa basi wao ni kufungia tu! Kama kuna jinai si polisi na mahakama zipo. Au mie ndo sielewi na akili zangu za usiku?😴
Hahahahaaa ni shida
 
Siku atakayo kufa mpinzani wa kisiasa, wa vyama vya upinzani atakejeriwa, kutukanwa na kuundiwa vikatuni na watakaofanya hivyo watasifiwa hata kupewa nishani.
Hii ndiyo nchi yangu iliyotekwa, na wanasiasa kila nyanja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetangaza kusitisha usajili wa Msanii Godfrey Tumaini (Dudubaya) kuanzia leo tarehe 28/02/2019.

Faida na hasara yake ni nini.
 
Hivi kwa nini ukifungiwa na BASATA hamna kukata rufaa au hao Basata ni malaika maamuzi yao yapo sawa kila wakati hayatakiwi kupingwa.Sasa Dudu kisheria hana kosa ,ila kimaadili sawa sasa kwa nini unamfungia kavunja sheria gani ya BASATA.Ila aisee hii nchi yetu hii mihemko mingi sana.
Unaweza unaenda kuomba judicial review na jamaa akiende anatoka vizuri tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
.
Nimeona tamko, na ningependa kufanya comment mstari baada ya msitari kama ifutavyo:

Mosi, BASATA wanasema:
View attachment 1034718

Aya hii ni taarifa, na haina lolote la kujadili kwani mamlaka hayo yako ndani ya uwezo wa kisheria wa BASATA.

Pili, BASATA wanasema:

View attachment 1034719

Hapa kuna kuna tatizo. Kukamatwa na Jeshi la Polisi ni kutuhumiwa. Kutuhumiwa sio kuhukumuiwa. Katiba ya nchi inasema kila mtu anayo haki ya kuhesabiwa mwenye haki mpaka mahakama inapomtia hatiani. Dudubaya hajatiwa hatiani na mahakama. Kwa hiyo, uamuzi wa BASATA unaweza, na unapaswa kufanyika, baada ya hukumu ya mahakama na sio kabla yake. Kwa hiyo, aya hii inamaanisha kuwa BASATA wamefanya maamuzi yanayokiuka Katiba ya nchi.

Tatu, BASATA wanasema:

View attachment 1034720
Aya hii inaendeleza kosa lililofanyika aya ya hapo juu. Kwamba Dudubaya ni "raia mwema" au kinyume chake ni suala la kuamuliwa na mahakama na sio vingnevyo. BASATA walipaswa kusbiri maamuzi ya mahakama ili wachukue hatua hii. Lakini wameitangulia mahakama. Wamekosea.

Na nne, BASATA wanasema,

View attachment 1034721

Aya hii imekaa kiswahili kweli kweli. Kwamba kuna Watanzania wengi "waliojitokeza kukemea kitendo cha Msanii Dudubaya" kwa sababu wanaona "hakifai," haimaanishi kwamba mahakama imetoa hukumu ya kisheria. Kisheria tunasema "plausibility does not imply validity." Kwa hiyo, BASATA wametumia sheria za mitaani kana kwamba ni sheria za kimahakama. Wamekosea.

Hivyo, naona kwamba, BASATA wanaendeleza utamaduni mpya wa baadhi ya vyombo vya serikali "kufanya kazi kwa mujibu wa matamko ya wakubwa" badala ya kuangalia sheria inasema nini. Utamaduni huu haukubaliki kwa Watanzania wanaojua na kuheshimu kanuni za utawala bora.

Kanuni moja ya utawala bora ni kanuni ya usawa mbele ya sheria.
Yaani, "the same law should apply to like persons in like circumstances."
BASATA wamezingatia kigezo hiki ? Hapana

Na bahati nzuri ni kwamba, Waziri wa Michezo, Dr. Harrison Mwakyembe, ni Mwanasheria Nguli. Nimesoma PHD Thesis yake yote. Yuko safi kichwani. Pia ni mlokole mzuri. Wengi tuliona alivyousindikiza mwili wa hayati Samwel Sitta kwa mbwembwe tosha za machozi ya Kilokole. Tunataka imani yenye vibwagizo vya matendo.

Ama sivyo, tutahitimisha kwamba ulokole ule ulikuwa ni usanii, na usanii sio taji lenye heshima kwa mtu mwenye umri kama wa Dr. Harrison Mwakyemba.

Mama Amon.
Unaweza tuhumiwa na Polisi ila ukawa umefanya kosa kwenye mamlaka husika..mfano sianond alifungiwa na basata lakini hatushtakiwa na polisi
 
Ni upuuzi kulazimishwa kufikiri sawa nchi nzima. Rais alitweet kuhuzunishwa na kifo cha Ruge, Lakini dudubaya yeye hakuona huzuni,bali akaona ndio muda wa yeye kutoa nyongo yake dhidi ya Marehemu. Hilo likawaudhi Serikali ya CCM kwa sababu aliyefariki ni wa kwao.
Kila mtu anakichwa chake na kila mtu yuko huru kufikiria na kusema akili yake inachoona kinafaa kusemwa hata kama hakiwapendezi. Uhuru wa mawazo uko wapi? Hao BASATA wamefuata kanuni na sharia gani au ndio wametumwa na Mwakyembe wamfungie?! Mwakyembe katumwa na mkubwa, nchi hii ni yetu sote jamani achene ubaguzi wa kifikra.
 
serikali ina viongozi wajinga sana hii! kwani ruge ndio nani hadi akidhihakiwa ipelekee ku end someone's career!? ujinga mtupu umewajaa viongozi wa nchi hii hasa yule jamaa wa BASATA anaitwa Mungereza nahisi hana ubongo hua anafikiri kwa kutumia bandama.
 
Dudubaya kaja na stail mpya[emoji38]
Kaona akitukana au akitoa kashfa mitandaoni eti ndio anapata jina[emoji38]
Alijua na hii nayo atapata jina kam ileee,!!!ishu ya mashoga[emoji38]
Duh,!!!kapewa Ban ya Nguvu[emoji38]na hivi hana hata hela ya chips[emoji38]huyo ndio Buriani naaga masela[emoji1321]‍♂️
 
Chukulia wewe baba yako kafa, harafu Kuna fala anatokea na kuanza kuitukana maiti ya baba yako, we ungemchukulia hatua gani, nahisi ungeenda kumfanya chochote ili ulidhike, sasa serikali kuona hivyo ndo ikaona umuhifadhi ili asidhurike
serikali ina viongozi wajinga sana hii! kwani ruge ndio nani hadi akidhihakiwa ipelekee ku end someone's career!? ujinga mtupu umewajaa viongozi wa nchi hii hasa yule jamaa wa BASATA anaitwa Mungereza nahisi hana ubongo hua anafikiri kwa kutumia bandama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetangaza kusitisha usajili wa Msanii Godfrey Tumaini (Dudubaya) kuanzia leo tarehe 28/02/2019.

Faida na hasara yake ni nini.
kwani kishatoka jela?
 
Back
Top Bottom