Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 6,067
- 10,938
Watu 7 wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa kutokana na ajali iliyohusisha lori aina ya Scania lenye namba za usajili T172 AUP, ambalo liligongana na Bajaj yenye namba za usajili MC 426 CFQ.
Watu saba wamefariki dunia na wengine nane wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha Lori kugonga pikipiki ya matairi matatu (Bajaji) jana Jumapili March 27, 2022 katika eneo la mtaa wa Kidulya nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
Akizungumza na Mwananchi Digital Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Simiyu, Faustine Mtitu amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa dereva wa lori uliosababisha kugonga bajaji.
"Baada ya lori hilo kuigonga bajaji inayokisiwa kuwa ilikuwa imebeba abiria sita na lori likiwa na watu takribani 12, bajaji iliwaka moto na lori kupinduka," amesema Mtitu.
Chanzo: Mwananchi
Watu saba wamefariki dunia na wengine nane wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha Lori kugonga pikipiki ya matairi matatu (Bajaji) jana Jumapili March 27, 2022 katika eneo la mtaa wa Kidulya nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
Akizungumza na Mwananchi Digital Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Simiyu, Faustine Mtitu amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa dereva wa lori uliosababisha kugonga bajaji.
"Baada ya lori hilo kuigonga bajaji inayokisiwa kuwa ilikuwa imebeba abiria sita na lori likiwa na watu takribani 12, bajaji iliwaka moto na lori kupinduka," amesema Mtitu.
Chanzo: Mwananchi