Barua Kutoka Ughaibuni - Kwanini Katiba Mpya na Si Kubadilisha ile Iliyopo

Barua Kutoka Ughaibuni - Kwanini Katiba Mpya na Si Kubadilisha ile Iliyopo

JC:

Nakubaliana katika ufafanuzi wako. Na kwa kutumia ufafanuzi wako, serikali ya majimbo ni muhimu kwa nchi kama Tanzania ambayo ina diversity ya ethnic groups.

Kuna study inayoonyesha kuwa nchi masikini kama Tanzania, zinatumia sehemu kubwa ya mapato yao ku-pacify ethnic tensions. Kwa mfano wilaya za Tanzania zimegawanywa kimakabila. Wakati wa Nyerere kulikuwa na wilaya kati ya 120 na hiyo ni sawa na idadi ya makabila. Vilevile majimbo ya ubunge yamefuata makabila.

Baraza la mawaziri la kwanza la Kikwete lilikuwa na mawaziri karibu 60. Na wengi walikuwa kama wawakilishi wa maeneo fulani au dini fulani.
Matokeo ni gharama kubwa ya uendeshaji wa serikali.

Wabunge wengi wa sasa ni wakazi wa DSM, wanagombe ubunge kwa sababu ya uhusiano wa kikabila na sio kuwa na ukazi au interests katika maeneo hayo. Na matokeo yake ni kuwa na wabunge wenye kuhitaji VX, kwa sababu atakuwa na uhakika wa kwenda kwenye jimbo lake, Dodoma kwenye vikao na kurudi nyumbani DSM.

Uzembe unaouona kwa viongozi wetu unatokana na kuwa hawawajibiki kwa wale wanaowatawala. Njia moja ya kuwafanya wawajibike ni kuzipa local authority madaraka makubwa. Viongozi wachanguliwe na locals.

Mkuu wa mkoa anayeteuliwa na Rais, interests zake ni kumsikiliza rais na sio wananchi. Na hicho cheo anaweza kupewa kama zawadi na sio sifa za kiutendaji.
 
Kaka George,

separation of power aina maana mwingine ana nguvu kushinda mwingine isipokuwa kama kuna mahala katiba imesema hivyo, naelewa kuna veto ambazo raisi anaweza pewa kwenye masuala nyeti. Hila kila mhimili unapewa, majukumu yake hili kuweka checks sawa. Mahakama aitungi katiba, wala executive gov aitungi katiba, the parliament has to vote for it kama wanaikubali ikishatungwa.

Na kama ulivyosema yes katiba itakuwa juu ya organs nyingi za serikali kwa sababu katiba ni kanuni za muongozo , lakini katiba kama ina utata lazima ibadilishwe na mahala pa kuutambua utata si ni mahakamani au?

The role of judicial review ni hizi zifuatavyo
(i)mahakama inaweza sema kama sheria fulani inafuata au aifuati katiba:
Kwa maana hiyo ingawa hawatungi sheria hila bunge likitunga sheria inayosema 'tume ya uchaguzi ndio yenye sauti ya mwisho kwenye matokeo". Mahakama inaweza sema kipengele fulani cha katiba labda tusema kipengele kinachosema 'kuhakikisha uchaguzi unakuwa wa haki na wa uwazi' kimevunjwa.
Kwa sababu hii sheria inasema tume haiwezi wajibishwa hivyo the openness ya kwenye uchaguzi according to 'katiba' inaweza vunjwa kupitia kipengele cha sheria hiyo na jamaa walivunja kweli. Matokeo yake Mahakama inaweza amuru sheria irekebishwe kulingana na katiba inavyosema. Kitakachoangaliwa ni nini katiba inasema kuhusu hicho kipengele kikatiba kwenye uchaguzi na hiyo sheria kurekebishwa uwazi wake hii ndio checks ya mahakama (you know im beggining to think the problem might be with the lawyers kuliko katiba).

(ii) judicial review inaweza resolve conflicts baina ya uongozi na wananchi kama masuala ya ubabe ambayo Za10 ameyaongelea ambayo hayako kwenye katiba hila CCM inafanya ki ubabe. Sasa suala si kujua katiba bali sheria ya nchi, ndio unawezajua umeonewa lakini kuna watu wanaenda shule kujifunza masuala ya kuweza kutetea.

(iii) judicial review ndio inayoweza amua masuala kama mahakama ya kadhi, au kesi za kisiasa kitaifa kwa kuangalia mistari ya katiba iliyopo.

Suala la UK separation of power lina utata sana kwa kuwa kuna fusion of power between the three main bodies, na 'bungeni' wabunge siku hizi hawana sauti, MPs just play within party lines and vote the same hata kama policy hawaikubali thats how things work right here. To sum up unaweza sema decision executive watakazo amua pembeni kwenye vikao vyao au mchakato wao wa kutunga policy, bungeni itapita tu based on their majority number.

Kuelezea hii issue ya UK ni kitabu ina mambo mengi ya politicians na how people are promoted to from back to front benches. Hivyo tamaa na party descipline imeua sana nguvu ya bunge na mahakama aipati challenges za hivyo kwa kuwa hawa watu wana respect democracy. political dramas zipo kwa akina Za10, huko ndiko kwenye separation of powers za ukweli na party descipline kuiweka ni ngumu kiasi.

Suala la mgombea binafsi kwangu ali make sense na wanasema if you got nothing nice to say about something best not say anything.
 
Kaka Za10,

In short hiyo namna aijenga taifa hila inabomoa, kuna uzembe tu wa kuwajibishana lakini matatizo si ya kusema tujenge namna nyingine ya kuliongoza taifa. Kwa maana huko ni kuwafanya watu wazidi kujitambulisha kiukabila kuliko utanzania especially taifa ambalo ignorance is still a problem.

Hiwapo kuna mijitu mpaka leo ulaya ina matatizo na jina tu socialism bila ya hata kuelewa the concept despite all the mass media, I cant imagine watanzania wote wakianza kujitambua kikabila kwanza. You do not need Einstein's IQ to know that is trouble in waiting.

nachukua break kidogo.
 
Kaka Juma nakubaliana na uchambuzi wako wa kazi za Judicial Review. Nionavyo mimi, katiba ya jamuhuri ya muungano kama ilivyo sasa inatoa nafasi na uhuru kwa mahakama kufanya kazi hii. Ndio maana kifungu katika sheria ya uchaguzi kilichokuwa kinahalalisha rushwa kwa mtindo wa takrima kilitangazwa na Mahakama kuwa haramu kwa kusigana na katiba. Tatizo lilipo katika kupinga matokeo ya Uraisi kama ilivyo kwa mgombea binafsi ni la kikatiba. Hata kama ingekuwa katiba ya Marekani ina kipengele kama hicho Mahakama ya Marekani ingebaki bila mamlaka ya kusikiliza kesi za kupinga matokeo ya uraisi. Kinachosema matokeo ya uraisi yasipingwe mahakamani ni Katiba sio sheria ya kawaida ya Bunge. Kama ingekuwa ni sheria ya kawaida ya Bunge mtu angeweza kufungua kesi mahakama kuu na kuipinga sheria hiyo kwa kukinzana na haki ya access to justice.


Katiba yetu licha ya mapungufu iliyonayo imeweka misingi mizuri ya separation of power, parliamentary supremacy na rule of law. Tatizo kubwa kwa kipindi kirefu ilikuwa ni kiwango kidogo cha uelewa wa sheria na uraia na kuwa na idadi chache ya wanasheria na wanaharakati wa haki za binaadamu. Kadili muda unavyokwenda matatizo mbali mbali ya ukiukwaji wa haki za binaadamu na utungwaji wa sheria haramu yanajitokeza na kupingwa mahakamani kwa mafanikio. Utakumbuka masuala kama ya dhamna ya gharama katika kesi ya uchaguzi, takrima, mgombea binafsi yalivyopingwa mahakamani na mahakama ikatamka bila kujiumauma kwamba sheria hizo za Bunge ni haramu kwa kusigana na katiba.

Tatizo ambalo lilianza kujitokeza ni msuguano kati ya mihimili mitatu ya dola. Bunge (bila shaka kutokana na uchanga wa mfumo wa utawala wa sheria na constitutionalism) Tanzania walianza kuhisi kwamba kwa mahakama kuzibatilisha sheria zilizotungwa na Bunge walikuwa wanaingilia mamlaka ya Bunge ya kutunga sheria. Pakajitokeza mjadala mkubwa ndani na nje ya Bunge kama Tanzania tuna Parliamentary Sovereingity kama ilivyokuwa Uingereza au Constitutional Supremacy? Mahakama ilivyotamka kuzuia mgombea binafsi ni batili kwa kukiuka haki ya kuchagua na kuchaguliwa, Bunge liliwazidi Mahakama ujanja kwa kuweka kifungu katika katiba kinachotaka mgombea kuwa mwanachama. Walifanya kitu karibu kama hicho hicho kuhusiana na dhamana ya gharama katika kesi za uchaguzi. Misuguano huu kati ya mihimili mikuu ya dola imesaidia kufichua mapungufu katika utaratibu wa kurekebisha katiba. Mamlaka ya Bunge la Katiba kurekebisha katiba yamekuwa makubwa mno kiasi kwamba yanatishia uhuru wa Mahakama. Suluhisho, vifungu vinavyojenga msingi wa katiba yetu kama vile haki za binaadamu, muungano, usekula wa dola, mfumo wa vyama vingi, ukomo wa bunge na uraisi nk vilirekebishwe bila kuwepo referandum.
 
Kaka Za10,

In short hiyo namna aijenga taifa hila inabomoa, kuna uzembe tu wa kuwajibishana lakini matatizo si ya kusema tujenge namna nyingine ya kuliongoza taifa. Kwa maana huko ni kuwafanya watu wazidi kujitambulisha kiukabila kuliko utanzania especially taifa ambalo ignorance is still a problem.

Hiwapo kuna mijitu mpaka leo ulaya ina matatizo na jina tu socialism bila ya hata kuelewa the concept despite all the mass media, I cant imagine watanzania wote wakianza kujitambua kikabila kwanza. You do not need Einstein's IQ to know that is trouble in waiting.

nachukua break kidogo.

JC:

Unajua miaka ya 60, 70, 80, watanzania walikuwa wanajivunia kuwa wana lugha moja na mataifa mengine ya kiAfrika hayana lugha. Tumekalia kujivunia wakati hatufanyi kitu chochote cha kuonyesha kuwa kuna advantage ya kuwa na lugha moja na makabila yanayofanana.

Kwa sasa hivi nchi nyingi za kiAfrika zimeanza kuwa na identity zao. Lugha alizoacha mkoloni zimeshasambaa na kutumika kama lugha ya taifa. Na zile tofauti zao za kikabila zinaondolewa kwa kuwa na local governments kusikiliza matatizo ya wananchi.

Sisi tunaendelea kutumia fomula hilehile ya 60 ambayo ina-breed mediocrity. Huwezi kupata viongozi wenye kuwajibika ukiwa unaendelea ku-recycle baraza la mawaziri. Vilevile huwezi kupata viongozi wa kujibika iwepo wengi wanaoongoza nchi wanateuliwa na mtu mmoja.

Tukirudi kwenye vipengere vyako vya mwanzo. Mfumo wa sasa wa utawala wa Tanzania unaiga wa Marekani. Mfumo huu wa Republic wa rais mwenye nguvu unataka wananchi wapewa madaraka makubwa ya kuchagua viongozi mbalimbali. Na vilevile unatakiwa uwe na bunge na judiacial zenye uhuru.

Na kama utaona kuwa wanaishi wakipewa nguvu wataleta ukabila, basi turudi kwenye mfumo wa Mwingereza. Serikali iundwe na wabunge na wao wachague waziri mkuu ambaye akiboronga, abaki madarakani kwa kupigiwa kura ya imani. Na kama tukirudi kwenye mfumo huo, basi rais abaki kwenye cheo cha kisherehe.
 
Kwamba Tanzania kuna tatizo la ethinicity kiasi cha kuhalalisha serikali za majimbo mimi nitakuwa wa mwisho kukubali. Tanzania niionavyo mimi ukabila sio tatizo kabisa. Kama ukabila lingekuwa ni tatizo tusingetegemea hata siku moja kuwa na Raisi mkwele au mzanaki wanaotoka katika vikabila vyenye watu wachache kabisa. Tusingetarajia mtu anayemfuatia Raisi katika jumla ya kura za Uraisi kutoka katika kabila la wambulu ambalo pia ni miongoni mwa makabila madogo hapa nchini. Tungetegemea Raisi msukuma, mnyakyusa au muhaya. Tusingetegemea msukuma kuwa mbunge Dar Es Salaam au Pwani na mchaga kuwa mbunge Mwanza au Shinyanga kama ilivyojitokeza katika uchaguzi mkuu. Kutokuwepo ukabila Tanzania ni suala la kihistoria lilichangiwa kwa kiasi kikubwa na mfumo wa maisha watanganyika tuliokuwa nao kabla ya ukoloni, mfumo wa ukoloni na harakati za kupingania uhuru bila kusahau juhudi za makusudi zilizofanywa na waasisi wa Taifa hili kujenga umoja na upendo miongoni mwa watanzania.


Tatizo la ukabila au umajombo ni tatizo Tanzania Zanzibar na ndio lililolazimisha kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa.


Matatizo madogomadogo yanayojitokeza kati ya wafugaji na wakulima na mgawanyiko na misuguano ya kikoo huko msoma haviwezi kuhalalisha serikali ya majimbo.

Nakubaliana na kaka Juma kwamba kuruhusu serikali ya majimbo ni kutoa mianya ya ubaguzi wa kikabila na kimajimbo Tanzania.
 
Kwamba Tanzania kuna tatizo la ethinicity kiasi cha kuhalalisha serikali za majimbo mimi nitakuwa wa mwisho kukubali. Tanzania niionavyo mimi ukabila sio tatizo kabisa. Kama ukabila lingekuwa ni tatizo tusingetegemea hata siku moja kuwa na Raisi mkwele au mzanaki wanaotoka katika vikabila vyenye watu wachache kabisa. Tusingetarajia mtu anayemfuatia Raisi katika jumla ya kura za Uraisi kutoka katika kabila la wambulu ambalo pia ni miongoni mwa makabila madogo hapa nchini. Tungetegemea Raisi msukuma, mnyakyusa au muhaya. Tusingetegemea msukuma kuwa mbunge Dar Es Salaam au Pwani na mchaga kuwa mbunge Mwanza au Shinyanga kama ilivyojitokeza katika uchaguzi mkuu. Kutokuwepo ukabila Tanzania ni suala la kihistoria lilichangiwa kwa kiasi kikubwa na mfumo wa maisha watanganyika tuliokuwa nao kabla ya ukoloni, mfumo wa ukoloni na harakati za kupingania uhuru bila kusahau juhudi za makusudi zilizofanywa na waasisi wa Taifa hili kujenga umoja na upendo miongoni mwa watanzania.


Tatizo la ukabila au umajombo ni tatizo Tanzania Zanzibar na ndio lililolazimisha kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa.


Matatizo madogomadogo yanayojitokeza kati ya wafugaji na wakulima na mgawanyiko na misuguano ya kikoo huko msoma haviwezi kuhalalisha serikali ya majimbo.

Nakubaliana na kaka Juma kwamba kuruhusu serikali ya majimbo ni kutoa mianya ya ukabila
Zakumi na George,

Tatizo huwa wengine wanazani hivyo vitu muhimu ulivyoweka mpaka kufikia hapa tolerance yetu ilipo vimetokea natural tuu, bila ya kuangalia kuwa mfumo wa sasa ndio ume-promote kuweza kufikia hapa tulipo na bado tunakazi.

Sasa wasubiri labda katiba ibadilishwe kama wanavyotaka wao alafu makabila yenye utamaduni wa kutafuta kimaisha waingie maeneo ambayo watu wanakalia mali na waanze kushamiri waone mapanga yatakavyoanza kurushwa.

Dini mbili kuu tu zinawashinda kudhibiti, itakuwa makabila yote baada ya miaka 30 ijayo. Wengine wanaona hivi vitu as a 'way of life and values' na wengine wanaona in 'terms of ideology and lines of reasoning' only, by understanding the latter utajua hatari zake.

Somali na Northern Ireland ni watu wa dini moja na almost of the same ethnicity lakini simple line changes on looking at religion watu wanaishi na chuki za ajabu wenyewe kwa wenyewe, hii ndio hatari ya ideology kwa kuwa ina form part of human reasoning and his/her identity.

Kuna mfano mmoja nilikuwa naangalia documentary wakati wa 'Obama' ana angaika na his 'health reform bill', kuna some sourthern state huko ambako kuna core conservative values na wazungu njaa. Yule reporter alienda clinic or something ambayo ina hudumuia watu wasiokuwa na health insurance. Akawa hana wa-interview watu pale clinic, watu wanasema sema hawamataki Obama kwa sababu ni 'socialist' he wants to make America a socialism country.

At the end of the programme nilijua kwanini yule reporter alichagua a southern state and a deprived neighbourhood, to question the sort of people Obama aimed to reach. Watu hao hao ndio wanasema he is a socialist they dont need him and do not support his reforms, yule reporter aka muuliza mama mmoja mwenye mdomo mrefu 'do you pay for this service' jibu lake 'no'. Yule reporter akaendelea 'what would have happened if there was no free clinic', mama 'i dont know'. Haya akaulizwa who funds the clinic, akajibu kanisa gani sijui huko.

Point aliyokuwa akitaka kuitoa reporter hapo ni kwamba hawa wamarekani wengine wapo too brain washed na ideologies zao kiasi kwamba they are not willing to be open minded au hata kuelewa kiasi kitu before making a decision. Watu wapo clinic ambayo inaendeshwa na Kanisa, madokta ni volunteer hawalipwi, watumiaji maskini lakini hawataki Obama reforms kwa kuwa Obama ni socialists. Yaani inabidi uangalie na kusema amna kitu kibaya kama kumpa mtu ideology bila ya kumfundisha ku question.

Sasa tazama huko marekani mpaka leo kuna states ambazo ni core Republic au Democrat, mwingine unaweza sema ndivyo ilivyo. Mwingine anauliza do these people look at any policies on offer or they just vote on ideologues of the party. Si ajabu most Americans (particulary the poor supporters of republicans) bado kujua most strong economies today are of mixed economies.

Kwa sababu kubwa America ni nchi ambayo bado inatumia media propaganda kuwauzia pumba na ideology ambazo wanazitambua zinaeleweka katika jamii iliyozoea kusikiliza one sided.

Ukija Europe huwezi kuta maskini hata siku moja akipigia kura Conservative. Yaani ni simple party affiliation is based on policies on offer, the poor labour (because it stands on strong values of equality), the rich (conservartives kwa sababu it protects the status quo) and the middle class are the swinging people (dependending on whos got the best policy for them coming election time). Unlike America were media plays a huge role based on ideologies and the wall st. can dictate the elcetion by pumping money.

Point ni kwamba with a fixed ideology or ways of running a state that promotes social groups identifiying themselves first than a state si nzuri. Sisi tumeshapita huko na kurudi si busara, ni sawa na kusema California leo ijigawe tena.
 
Kaka George,

Mimi sijaisoma katiba nzima ya Tanzania wala siijui inapopatikana sasa siwezi kuja na kusema kipi kimevunjwa au la. Ninachoweza zungumzia ni mgawanyo wa majukumu na kusema vipi intervention inawezekana. Kama katiba yetu aina kipengele chenye kusema uchaguzi 'huwe wenye uwazi na kufuata demokrasia' (or anything along those lines) then sheria si batili. Lakini kama kuna kitu chochote kinacho gusia fareness kwenye election hiyo sheria inaweza pingwa kwanza kabla ya kusubiri katiba. Hila kama katiba inasema matokeo ya uchaguzi wa raisi yasipingwe then katiba yenyewe inazua utata na masuala ya uchaguzi. Sasa hata mtu akichukua mtutu akaikamata tume ya Uchaguzi na kusema imtambulishe kama yeye raisi inakuwaje? tutaweza kumshitaki kwa namna aliyojipa muongozo au?.

Point ni kwamba kuna vitu ni just commonsense katiba kama inasema matokeo hayawezi pingwa au hata kutakiwa kuhalalishwa kama kuna utata, then it is a problem lakini still mahakama inaweza bado kutumika kama chama cha siasa kiki-file a claim against ruling party kukataa kurekebisha matatizo au?

Mwisho niseme parliamentary sovereignty doesnt mean parliament can behave as it wishes without questioned. Ndio katiba inasema parliamentry ndio chombo kikuu ikamaniisha kwamba bunge ndio lenye uwezo wa wakutunga, badili au rekebisha sheria. Lakini mahakama inaweza challenge sheria ambazo azipo in line na katiba. Na katiba yao ina mambo mengi sasa apart from human rights amendements bado kuna EU amendments. Hivyo now and then laws are challenged and changed kutokana na civil law suits along the lines of human rights, equality, employment tribunals. Huwezi sikia kesi kama za kwetu kwa sababu political democracy is respected na sheria aitungwi na watu tu, both political parties reps are present at the process, scholars, and experienced people of the branch of law hiyo sheria inapolenga. Kwa hiyo rarely utasikia malalamiko ya kisiasa na vitu kama hivi upita bungeni mara nyingi bila ya kelele. Bali malalamiko ya human rights and other civil liberties are not uncommon kwenye ku-challenge baadhi ya sheria.
 
JC:

Naelewa unayozungumza. Nimejaribu kuipitia historia ya Tanzania kwa makini sana wakati wa uhuru. Nyerere alipochukua uongozi wa TAA alikuwa kijana mdogo na kutoka mbali na DSM. Hivyo katika kipindi kile suala la ukabila au udini halikuwepo. Hivyo basi watu wanapokuwa na common interests ambazo zinawapa faida, wanakubaliana na kuachana na tofauti zao.

WaMareakani wana tofauti kubwa sana katika itikadi, kirangi na kiimani. Lakini kuna common interests ambazo zinawafanya wao wawe pamoja. Miongoni mwa vitu hivyo ni abstract concepts zilizopo kwenye tangazo la uhuru (Declaration of Independence) na katiba (Constitution).

Tangazo la uhuru linasema: We hold these truths to be self-evident, that all men are created equal, that they are endowed by their Creator with certain unalienable Rights, that among these are Life, Liberty and the pursuit of Happiness.



Katiba ina Bill of rights yenye vipengere:
  1. Free Exercise Clause; freedom of speech, of the press, and of assembly; right to petition: Congress shall make no law respecting an establishment of religion, or prohibiting the free exercise thereof; or abridging the freedom of speech, or of the press; or the right of the people peaceably to assemble, and to petition the Government for a redress of grievances.
  2. Militia (United States), Sovereign state, Right to keep and bear arms: A well regulated Militia being necessary to the security of a free State, the right of the people to keep and bear arms shall not be infringed.
  3. Protection from quartering of troops: No Soldier shall, in time of peace be quartered in any house, without the consent of the Owner, nor in time of war, but in a manner to be prescribed by law.
  4. Protection from unreasonable search and seizure: The right of the people to be secure in their persons, houses, papers, and effects, against unreasonable searches and seizures, shall not be violated, and no Warrants shall issue, but upon probable cause, supported by Oath or affirmation, and particularly describing the place to be searched, and the persons or things to be seized.
  5. due process, double jeopardy, self-incrimination, eminent domain: No person shall be held to answer for any capital, or otherwise infamous crime, unless on a presentment or indictment of a Grand Jury, except in cases arising in the land or naval forces, or in the Militia, when in actual service in time of War or public danger; nor shall any person be subject for the same offence to be twice put in jeopardy of life or limb; nor shall be compelled in any criminal case to be a witness against himself, nor be deprived of life, liberty, or property, without due process of law; nor shall private property be taken for public use, without just compensation.
  6. Trial by jury and rights of the accused: Confrontation Clause, speedy trial, public trial, right to counsel
    In all criminal prosecutions, the accused shall enjoy the right to a speedy and public trial, by an impartial jury of the State and district where in the crime shall have been committed, which district shall have been previously ascertained by law, and to be informed of the nature and cause of the accusation; to be confronted with the witnesses against him; to have compulsory process for obtaining witnesses in his favor, and to have the Assistance of Counsel for his defense.
  7. Civil trial by jury: In suits at common law, where the value in controversy shall exceed twenty dollars, the right of trial by jury shall be preserved, and no fact tried by a jury, shall be otherwise re-examined in any court of the United States, than according to the rules of the common law.
  8. Prohibition of excessive bail and cruel and unusual punishment: Excessive bail shall not be required, nor excessive fines imposed, nor cruel and unusual punishments inflicted.
  9. Protection of rights not specifically enumerated in the Constitution: The enumeration in the Constitution, of certain rights, shall not be construed to deny or disparage others retained by the people.
  10. Powers of States and people: The powers not delegated to the United States by the Constitution, nor prohibited by it to the States, are reserved to the States respectively, or to the people.
Ukichukua vipengere hivi, utaona kuwa waMarekani wengi wanavielewa na kukubaliana navyo japokuwa wanakuwa na backgrounds tofauti. Hakuna Mmarekani atakayekubaliana na wewe kuwa umpe shule au matibabu bure halafu umnyime haki za kikatiba.

Marekani huwezi kuanzisha kijiji cha Ujamaa kitakachotoa elimu bure, matibabu na huduma zingine bure lakini ukakiuka haki za wananchi za kumiliki au kutoa mawazo.

Kwa upande wa Tanzania, tunatumia muda mwingi kuwafanya watanzania wawe sawa. Hakuna mtanzania aliyechagua kuzaliwa katika kabila fulani. Hivyo mila na desturi za makabila ambazo hazivunji sheria au makubaliano ya kikatiba hazina ubaya wowote. Na watu wa makabila mengine ni lazima tujifunze kuheshimu wenzentu.
 
Kaka Zakumi,

Kwenda kumlazimisha mtu aende shule ya serikali kama hataki si sawa. Lakini mtu huyo huyo kwenda kutumia shule ambayo wasamalia wema imewajengea watu ambao hawana makaratasi ya kutumia shule za serikali ndio uwenda wazimu.

Halafu mtu huyo huyo aitukane serikali kwa kujenga shule za bure kwa raia. Wakati huo huo anaenda kutumia services ambazo wasamalia wema wamejitolea kujenga au kuziendesha kusaidia ambao serikali imewatupa. Halafu mtu huyu ndie anauliza kwa nini serikali ijenge shule za bure. Angekuwa mtu ambae analipia private sawa lakini ni mtu anaeenda kutumia service ambayo its meant for those at the bottom of the social. Huu ni ujinga as a product of ideology rather than being a realistic individual, kwa sababu in reality you need the service but your mind is telling you different things based on ideology. (huyo ndio mmarekani)

Ndio nasema amna kitu kibaya kama watu wakianza kupewa nafasi za kuanza kujiangalia through ideologies au hata kuacha hivi vitu vikuwe na namna moja wapo ni kuanza kusema watu wawe responsible na local wealth, especially were society is not of mixed cultures. Aina maana it is a aproblem at first lakini future implications watu wanaweza jiona hivi vitu ni mali yao kwanza na si ya Tanzania especially wale, watakao zaliwa baada ya katiba mpya. Ideologgy is not inborn it is learned, leo tunalalamika mali ya wizi wa taifa kutokana na uongozi ulipo (mfumo), hiyo namna ya federal watu watasema sisi ndio tunaonewa kwa sababu umeshawafunza kujitawala na kujiona kama kundi. Shinyanga leo wangedia more kwa madai almasi ndio mali inayotakiwa kuinua shinyanga.

Hivi vitu Za10 watu wanajifunza kutokana na hali na mfumo uliopo, amani yaleo ni mtaji mkubwa wa busara za mwalimu kuunganisha jamii. Lakini kamwe hivi sivyo inavyokuwa in all cases au vinginevyo the world would have been a better place.
 
Kaka Juma,

Tuko pamoja juu ya maana ya parliamentary supremacy. Parliament inakuwa supreme katika law making and unmaking in as long as hizo sheria hazipingani na katiba. Na hilo kwa Tanzania kikatiba halina matatizo.

Katiba ya Tanzania inazungumzia vya kutosha juu ya fairness katika uchaguzi. Ki msingi katiba imetoa haki nyingi za binaadamu na kiraia. Tatizo ni kwamba haki nyingi, kama sio zote sio absolute. Mbali ya vipengele vinavyotoa haki, vipo vingine vinavyotoa utaratibu na masharti ya namna haki zinavyoweza kutumika. Haki ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa na tumia mahakamani ipo isipokuwa tu kwa upande wa uchaguzi wa Raisi. Wajibu wa Tume ya Uchaguzi kuendesha uchaguzi kwa kuzingatia haki, usawa na sheria imeelezwa pia kwa unagaubaga. Haihitaji utafiti zaidi kuhitimisha kwamba uchaguzi ulioendeshwa kwa kukiuka misingi ya haki na uadilifu ni batili. Wakati huo huo katiba inasema matokeo ya uraisi yakitangazwa yanabaki kuwa sahihi. Hoja kubwa inayotolewa hapa ni kwamba haki ya kupinga matokeo ya uraisi mahakamani imeondolewa kwaajili ya maslahi ya umma. Watunzi wa Katiba waliona uwezekano mkubwa wa kutokea vulugu na uvunjifu wa amani kama kila mtu asieridhika na matokeo ya uchaguzi atakuwa na haki ya kwenda mahakamani. Kama wasiwasi huu kwa sasa haupo au hauna msingi ni suala la wananchi kuamua.

Mara nyingi kuondolewa kwa haki fulani ya msingi huwa kunakuja kama suala la necissity. Wafasilina wa katiba huwa wana kigezo kimoja katika tafsiri ya sheria kininachojulikana kama proportionality. Katika hili huwa pamoja na mambo mengine wanaangalia kama kuondolewa kwa haki fulani kulikuwa ni mhimu kwaajili ya kulinda haki ya watu wengine pengine wengi zaidi au haki kubwa zaidi.
 
Kaka George

Sasa huko unako kwenda unahitaji wataalamu wa kutunga sheria, mahakama, na watu wanaojau sheria vizuri. Mi naelewa siasa kiasi lakini si sheria.
 
hamna maana yoyote kuwa wanafiki. hivi hamuooni jinsi hawa viongozi wanavyojifanyia mambo bora liende kisa wako na power inawalinda ya katiba kutoshtakiwa au tutafute smg za Burindi tuwatungue ili wajue tunataka katiba inayo toa mamlaka kwa wananchi na sio watu baadhi 2
 
Kaka George,

Mimi sijaisoma katiba nzima ya Tanzania wala siijui inapopatikana sasa siwezi kuja na kusema kipi kimevunjwa au la. Ninachoweza zungumzia ni mgawanyo wa majukumu na kusema vipi intervention inawezekana. Kama katiba yetu aina kipengele chenye kusema uchaguzi 'huwe wenye uwazi na kufuata demokrasia' (or anything along those lines) then sheria si batili. Lakini kama kuna kitu chochote kinacho gusia fareness kwenye election hiyo sheria inaweza pingwa kwanza kabla ya kusubiri katiba. Hila kama katiba inasema matokeo ya uchaguzi wa raisi yasipingwe then katiba yenyewe inazua utata na masuala ya uchaguzi. Sasa hata mtu akichukua mtutu akaikamata tume ya Uchaguzi na kusema imtambulishe kama yeye raisi inakuwaje? tutaweza kumshitaki kwa namna aliyojipa muongozo au?.

Point ni kwamba kuna vitu ni just commonsense katiba kama inasema matokeo hayawezi pingwa au hata kutakiwa kuhalalishwa kama kuna utata, then it is a problem lakini still mahakama inaweza bado kutumika kama chama cha siasa kiki-file a claim against ruling party kukataa kurekebisha matatizo au?

Mwisho niseme parliamentary sovereignty doesnt mean parliament can behave as it wishes without questioned. Ndio katiba inasema parliamentry ndio chombo kikuu ikamaniisha kwamba bunge ndio lenye uwezo wa wakutunga, badili au rekebisha sheria. Lakini mahakama inaweza challenge sheria ambazo azipo in line na katiba. Na katiba yao ina mambo mengi sasa apart from human rights amendements bado kuna EU amendments. Hivyo now and then laws are challenged and changed kutokana na civil law suits along the lines of human rights, equality, employment tribunals. Huwezi sikia kesi kama za kwetu kwa sababu political democracy is respected na sheria aitungwi na watu tu both political parties reps are present at the process, scholars, and experienced people of the branch of law hiyo sheria inapolenga. Kwa hiyo rarely utasikia malalamiko ya kisiasa. Bali malalamiko ya human rights and other civil liberties are not uncommon.

JC:

Nimeisoma katiba ya Tanzania. Ina mambo mengi mazuri tu pamoja na kasoro zake. Lakini haina mtiririko mzuri unaowapa wananchi nguvu za kisheria.

Kwa mfano uingereza haina katiba ya kuandikwa. Lakini Magna Carta iliyoandikwa 1215 na kubadilishwa baadaye ilitoa haki za kiraia. Hivyo sheria za nchi zilizofuatia hazikuvunja haki za binadamu zilizotolewa kwenye Magna Carta.

Kwa Marekani Tangazo la uhuru na bill of rights zimeweka utangulizi kuwa hakuna sheria za nchi au mabadiliko ya katiba yatakayokiu haki zilizotangazwa mwanzo.

Ukisoma katiba ya Tanzania, inaonyesha kuwa vipengere vya haki za binadamu vimeingia kwenye katiba mwaka 1984. Wakati huo tayari viongozi wa nchi na mahakama walishajijengea mazoea ya kutoa amri. Kwa mfano, kuna kipengere kinachosema:

13.(6)(c) ni marufuku kwa mtu kuadhibiwa kwa sababu ya kitendo chochote ambacho alipokitenda hakikuwa ni kosa chini ya sheria, na pia kwamba ni marufuku kwa adhabu kutolewa ambayo ni kubwa kuliko adhabu iliyokuwapo wakati kosa linalohusika lilipotendwa.

Kwa Tanzania ni kitu cha kawaida kwa kiongozi kusema mweke ndani. Anafanya hivyo kwa sababu hajui katiba na haki za mwananchi. Sokoine kipenzi cha watu wengi hapa, alikamata watu kwenye ulanguzi na baadaye bunge likatunga sheria za makosa yao.



 
Zakumi bana,

si afadhali huyo sokoine, aliweza sema wahujumu uchumi leo hii mkwere nasikia anafunga watu for life wakipitia mizoga yake tu. Halafu hao majaji umewaona sijui law wame practise lini na ujaji wameupata lini. Tuna majaji tele hata 35 yrs of age hawana, kuna cha kupingwa hapo cha maana, iwapo majaji wenyewe hata hawaja practice hiyo law kwa muda mrefu.

Bongo mjomba usijifanye mjuaji ama likizo utaiona chungu mjomba.

Laterz.
 
Kaka Zakumi,

Kwenda kumlazimisha mtu aende shule ya serikali kama hataki si sawa. Lakini mtu huyo huyo kwenda kutumia shule ambayo wasamalia wema imewajengea watu ambao hawana makaratasi ya kutumia shule za serikali ndio uwenda wazimu.

Halafu mtu huyo huyo aitukane serikali kwa kujenga shule za bure kwa raia. Wakati huo huo anaenda kutumia services ambazo wasamalia wema wamejitolea kujenga au kuziendesha kusaidia ambao serikali imewatupa. Halafu mtu huyu ndie anauliza kwa nini serikali ijenge shule za bure. Angekuwa mtu ambae analipia private sawa lakini ni mtu anaeenda kutumia service ambayo its meant for those at the bottom of the social. Huu ni ujinga as a product of ideology rather than being a realistic individual, kwa sababu in reality you need the service but your mind is telling you different things based on ideology. (huyo ndio mmarekani)

Ndio nasema amna kitu kibaya kama watu wakianza kupewa nafasi za kuanza kujiangalia through ideologies au hata kuacha hivi vitu vikuwe na namna moja wapo ni kuanza kusema watu wawe responsible na local wealth, especially were society is not of mixed cultures. Aina maana it is a aproblem at first lakini future implications watu wanaweza jiona hivi vitu ni mali yao kwanza na si ya Tanzania especially wale, watakao zaliwa baada ya katiba mpya. Ideologgy is not inborn it is learned, leo tunalalamika mali ya wizi wa taifa kutokana na uongozi ulipo (mfumo), hiyo namna ya federal watu watasema sisi ndio tunaonewa kwa sababu umeshawafunza kujitawala na kujiona kama kundi. Shinyanga leo wangedia more kwa madai almasi ndio mali inayotakiwa kuinua shinyanga.

Hivi vitu Za10 watu wanajifunza kutokana na hali na mfumo uliopo, amani yaleo ni mtaji mkubwa wa busara za mwalimu kuunganisha jamii. Lakini kamwe hivi sivyo inavyokuwa in all cases au vinginevyo the world would have been a better place.

JC:

Mimi najaribu kukita kwenye mambo ya uchumi na maendeleo ya jamii. Almasi ya Mwadui ikibaki Shinyanga haitamfanya Mzaramo alale njaa. Hizi concepts za kuwa serikali kuu ipate revenues na baadaye i-distribute wealth hili amani ipatikane ni myth.

Kwa mfano wakati wa Nyerere kulikuwa na bodi za kahawa. Na matokeo yake serikali kuu ilipata sehemu kubwa ya mapato kuliko wakulima. Kipindi cha Mwinyi, wabunge wa mikoa yenye uzalishaji mkubwa wakataka mapato. Wakulima wakalipwa kutokana na bei ya dunia. Matokeo yake, watu wa mikoa hiyo wakawa na pesa zaidi ambazo wamezifanyia kazi za maendeleo bila kutegemea sana serikali. Na watu wa mikoa isiyo na kahawa hawakuathirika.

Na kwa mtaji huu serikali inaweza kuacha sehemu kubwa ya mapato kwenye sehemu husika. Na hii haitafanya watu wa mikoa mingine washike mapanga au bunduki kupigani kisicho chao.

Watu wanaendesha shughuri za maisha yao kutokana na vitu vilivyopo kwenye mazingira yao. Lakini kuanzia miaka ya 50, ilitokea nadharia kuwa ukitaka kuondoa umasikini katika nchi za dunia ya tatu, basi tajirisha serikali. Hivyo kuanzia kipindi hicho kukawepo na interests kubwa za serikali za nchi hizo kukusanya mapato yanayotokana na natural resources. Lakini hii kwa nchi za kiafrika imekuwa a curse than a blessing. Na imechochea ethnic conflicts. Kwa mfano wananchi wa mikoa inayotoa dhahabu wanaachiwa mashimo na uchafuzi wa mazingira.
 
mpaka Sabasaba ndio watoe Katiba?

Nimetafuta ma bookstore yote hakuna Katiba mjini hapa, duka la Serikali Jamhuri street ndio wazembeeee wa kutupwa mtaroni

Duh, kama sio sabasaba wapi pengine watagawa katiba.

If one has 1,000,000/= and bets with someone at Kimara that for each bookshop seen from Kimara to town centre he will dish 100,000/=, at the end of that adventure the guy will be left with 700,000/=. And, mind you, the three bookshop seen will be selling cards for valentine, sendoff, weddings and those funny stuffs like vocha za simu etc.
 
Bwana CJ suala la watu wanaozunguka rasilimali fulani kunufaika na mapato ya rasilimali hiyo kwa mtizamo wangu halihitaji serikali za majimbo. Chini ya mfumo tulionao sasa, mbali ya serikali kuu tuna local goverments ambazo sipo katika mtindo wa majiji, manispaa, miji, mitaa na vijiji. Chini ya utaratibu huu inaweekana sheria ikawekwa kwamba asilimia fulani ya mapato yanayopatikana kwa mfano katika madini itumike kuboresha huduma za kijamii katika jamii inayozunguka rasilimali husika.
 
Zakumi bana,

si afadhali huyo sokoine, aliweza sema wahujumu uchumi leo hii mkwere nasikia anafunga watu for life wakipitia mizoga yake tu. Halafu hao majaji umewaona sijui law wame practise lini na ujaji wameupata lini. Tuna majaji tele hata 35 yrs of age hawana, kuna cha kupingwa hapo cha maana, iwapo majaji wenyewe hata hawaja practice hiyo law kwa muda mrefu.

Bongo mjomba usijifanye mjuaji ama likizo utaiona chungu mjomba.

Laterz.

JC:

Kwikwikwi, yalishanipata hayo. Nilikuwa likizo na kulikuwa na uchaguzi mdogo wa ubunge. Wakati wa kampeni, mjumbe wa tawi la CCM akaja kutugongea mlango kwenda kwenye mkutano wa kampeni. Nikamwambia kuwa kupiga kura ni haki yangu. Hivyo ni chaguo langu kusikiliza kampeni na sio lazima kwenda. Mjumbe akaanza kufoka kuwa mimi ni miongoni mwa vijana wanaoleta vurugu na kutishia amani.

Mijitu kama hii iliyojaa ignorance uwezi kubishana nayo na kujifanya mjuaji.
 
Duh, kama sio sabasaba wapi pengine watagawa katiba.

If one has 1,000,000/= and bets with someone at Kimara that for each bookshop seen from Kimara to town centre he will dish 100,000/=, at the end of that adventure the guy will be left with 700,000/=. And, mind you, the three bookshop seen will be selling cards for valentine, sendoff, weddings and those funny stuffs like vocha za simu etc.

Ngambo Ngali,

Wakati wa uchaguzi T-shirt zinawafikia watu majumbani. Nchi za Magharibi zinatoa nafasi kwa wajumbe mbalimbali wa vyama vya siasa kutembelea nchi zao na kuona jinsi vyama vya kisiasa katika nchi hizo zinavyoendeshwa. Ruzuku ya vyama vya siasa ni nyingi mno kuliko kutoa machapisho ya katiba ya bure kwa watanzania.

Kwa ujumla gharama zinazotumika katika mambo ya kisiasa Tanzania ni kubwa sana kuliko faida inayopatikana. Kikazo kikubwa katiba sio priority ya Watanzania au serikali.
 
Back
Top Bottom