Barua ya Diamond ! Duh noma!

Barua ya Diamond ! Duh noma!

Wasanii wetu wanatia aibu,baada ya kutumia muda mwingi kujifunza vitu vya msingi katika maisha yao.Wao umaarufu na ufuska ndio kipaumbele katika maisha yao.Sasa hii barua sijui kaandika Babu Tale au Domo mwenyewe?
Ukiondoa makosa ya kiuandishi hata format yenyewe ya official letter ni ya hovyo.Anuani zote zipo upande mmoja (kushoto),WCB haina logo wala headed paper.Haya ni matusi kwa mara nyengine kwa jeshi letu.Diamond rudi shule kwani elimu haina mwisho.
 
kama kweli hii barua ni copy of the original one, kutakuwa na tatizo, kuwa daimond hana uelewa wa kutosha on how to draft an official letter jambo ambalo mimi halinishangazi tho' otherwise kuna mtu kuamua kumtengenezea headlines tena.

hivi kazi ya mameneja ni nini jamani?
 
Huu ni ujinga tuu hii barua haiwezi ikawa imeandikwa na watu wenye akili timamu kabisa!

Yani haijulikani ni JKT au JWTZ!
Huu ujinga hauwezi kuwa umepelekwa JWTZ ni watu tuu wana furahishana kwenye mitandao tuu!

Kinachokufanya uwaze diamond hawezi kuandika huo ujinga ni nini?
Juzi ulianzishwa Uzi kuhusu diamond kuzomewa na mashabiki wa kiba, nilipo comment kuwa anatakiwa aangalie nyendo zake kuhusu tabia na dharau, walijitokeza watu wakanambia nina wivu sana, ila nikawaambia kwa macho makavu SIWEZI ONA WIVU kwa mtu asiyejua hata kuandika jina lake vizuri. Sasa unaona ujinga ulioandikwa kwenye hiyo barua, na hapo wame edit sana hadi kujiridhisha itoke.
 
Kinachokufanya uwaze diamond hawezi kuandika huo ujinga ni nini?
Juzi ulianzishwa Uzi kuhusu diamond kuzomewa na mashabiki wa kiba, nilipo comment kuwa anatakiwa aangalie nyendo zake kuhusu tabia na dharau, walijitokeza watu wakanambia nina wivu sana, ila nikawaambia kwa macho makavu SIWEZI ONA WIVU kwa mtu asiyejua hata kuandika jina lake vizuri. Sasa unaona ujinga ulioandikwa kwenye hiyo barua, na hapo wame edit sana hadi kujiridhisha itoke.
Naomba unisome upya!

Nina cho maanisha kuwa haiwezekani management yote hile kuruhusu barua ya namna hii kupelekwa sehemu yeyote serious!

Barua hii haimgusi Diamond pekee bali ina gusa uongozi wake wote hata watu wake wa karibu!

Ndio maana nasema hii barua haijaandikwa kutoka kwa Diamond bali ni michezo tuu!
 
Kwenye hiyo barua hapo chini ya (JKT - JWTZ) alikua anaanza kwakuandika DEAR alikua anahisi anamuandikia WEMA nini!
 
hivi kazi ya mameneja ni nini jamani?

inategemea na meneja mwenyewe wangu, babu tale is he a meneja by professional??? i dont think so, anatakiwa awe amesoma leadership & administration, ila huu umeneja naona ni ile tuu ya kibongo bongo ili mradi liende.
 
Hiyo barua ameandikiwa na mama Ubaya akiwa China, si mnajua yule kwa kuwaza Mapenzi ndo akaandika dear...!
 
Kwenye hiyo barua hapo chini ya (JKT - JWTZ) alikua anaanza kwakuandika DEAR alikua anahisi anamuandikia WEMA nini!

Ha ha ha atakua ali mumiss bebe wake inabidi atafte proffesional wa kumsaidia aisee hadi namhurumia
 
SasA wakimpeleka mahakaman si barua itakua ushahidi au?
EMT kwa msaada wa kisheria
 
Last edited by a moderator:
Hiyo barua imeandikwa na vichwa vitatu babu Tale,mkubwa Fella na Almasi mwenyewe.Anwani imeandikwa na Babu Tale,mwanzo wa barua Mkuu Fella, dhumuni na mwisho wa barua imeandikwa na Almasi mwenyewe.
 
Hiyo barua imeandikwa na vichwa vitatu babu Tale,mkubwa Fella na Almasi mwenyewe.Anwani imeandikwa na Babu Tale,mwanzo wa barua Mkuu Fella, dhumuni na mwisho wa barua imeandikwa na Almasi mwenyewe.

Hahahaaaaaa
 
Jeshi la kujenga Taifa ndo JWTZ??? sidhani kama atapata msamaha!!!

ImageUploadedByJamiiForums1414168149.962947.jpg

ilo neno DEAR Kwenye barua ya Kiswahili nimelipenda!
 
Naomba unisome upya!

Nina cho maanisha kuwa haiwezekani management yote hile kuruhusu barua ya namna hii kupelekwa sehemu yeyote serious!

Barua hii haimgusi Diamond pekee bali ina gusa uongozi wake wote hata watu wake wa karibu!

Ndio maana nasema hii barua haijaandikwa kutoka kwa Diamond bali ni michezo tuu!

Ikizingatiwa ulikuwa unasizitiza kuwa

Diamond alikuwa na kibali cha kutumia nguo za jeshi la wananchi kwenye show yake na alipewa toka alhamisi!

......Diamond alipata kibali cha kutumia hayo mavazi!

Kwa hiyo hapo una maana kuwa hiyo barua siyo yake kwa sababu alikuwa na kibali cha kuvaa yale mavazi?

Maana mtu huwezi kuomba radhi kama ulikuwa na ruhusa ya kuvaa hayo mavazi.
 
Back
Top Bottom