Barua ya majibu ya Msekwa kuwajibu Kinana na Makamba hii hapa

Barua ya mzee Makamba na Kinana anaipeleka Nape?
 
Wewe ni mbuzi hujui hata taratibu zinaendaje akiliyako ni kutaka uvunjifu wa amani
 
Kwa hiyo unawatetea Kinana na Makamba? Siyo nyie mlikuwa mnasema Kinana ni msomali anayemaliza tembo wetu kwa kuwa kigogo wa biashara Haram ya pembe za ndovu?

Kiukweli hamuleweki!
Hao ni wajinga tuu nia yao ccm wavurugane
 
ukatorik tu ha
Huku bavichaa wako bize na audio feki za ccmView attachment 1156857
CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KUPITIA KICHAA WAKE JPM CHAWAZULUMU/ KUWAPORA WAKULIMA KOROSHO ZAO HUKO KUSINI.
chashindwa kulipa!
chasiingizia ujenzi wa mataaluma ya reli
Hovyo wewe
 
Neno "uoga" unautafsiri vipi? Kuna siku aliyekuwa kocha wa arsenal mzee arsene Wenger aliwahi kuulizwa....akistaafu atafanya shughuli gani? Alijibu hawezi kufanya chochote zaidi ya soka hii ni kwa sababu ameishi na kukulia kwenye soka...je Wenger ni muoga wa maisha nje ya soka?

The same applies to mzee Msekwa...amekuwa ameishi na amezeekea CCM tangu iikiwa Tanu...je huo ndo uoga?

Msekwa kumuoa Anna Abdallah toka UWT kuna tatizo gani? Mara Nyingi watu wa Kada Fulani wanaoana wao kwa wao sababu kuu ni kukutana Mara kwa Mara kwenye shughuli zao.....je tumlaumu mlevi akimuoa barmaid?

Kaka rudi tena darasani na utafute tafsiri sahihi ya neno uoga....maana unapotosha watu.

Humu JF kina Kinana wakati wameshika hatamu walishambuliwa sana kuwa ni majangiri na waua tembo wetu....je Leo baada ya kustaafu ndo wamekuwa mashujaa na ujangiri wameacha?

WaTanzania acheni unafiki na kusukumwa sukumwa na upepo.
 
Wajipange kisawasawa, ni vyema wakae kimya. wakati mwingine ukimya unasaidia kuonyesha hekima zao, wala siyo lazima ukituhumiwa ujibu kama ni kuchafuka walishachafuka sana na wala hawachafuliwi na Msiba, hata wakiweka mkwala ndani ya chama tuko tayari kumsimamisha kama mgombea pekee na atapata kura za kutosha. Makamba kama mwasisi wa rushwa ndani ya chama ambaye kwa kiasi kikubwa alikiweka pabaya chama hicho bora angekaa kimya vinginevyo anamharibia hata kijana wake January anayeonekana walau kuwa na hekima kidogo kuliko Baba yake. Niombe JPM awapuuze hao naona ugonjwa wa kusahau umewaanza mapema.
 
Nimeanza kumwogopa sana Musiba inaelekea anachosema anauhakika nacho na maneno yake yana kishindo kikuu. Musiba amesema Vodacom ilikuwa ya CCM wakagawana na wenye share ndio hawa wanaotoa majibu kwa akina Kinana hatari.
 
Msekwa anatoa majibu ya awali kama nani?? Hapo ni kama keshavunja katiba, je kikao kikaja kuamua vingine itakuwaje?
Kama umesoma between the lines,kikao cha Baraza hakitakuja na maamuzi tofauti na haya.They are thrown under the bus sababu wanes jamani was “wapambane na hali zao”!kwamba kutakua kikao kingine ni geresha kuwafanya waendelee kungoja/au kununua muda wakati majibu yako tayari.usishangae hata kikao cha hilo baraza hakitakaa
 
Kuchafuliwa ni kubambikiziwa mambo mabaya yasiyo kweli,sasa katika mazingira yao, kweli wamechafuliwa?Si kweli.Kama ni kweli wakanushe tuhuma za Mukama.
Na je,utendaji wa watuhumiwa ni mzuri kama wanavyodai?So far hakuna ushahidi huo.Kama nilivyosema wakanushe tuhuma za Mukama kama ni wasafi.Ila wawe makini,maana jamaa naona hazungumzi kutoka hewani,ana ushahidi wa kufa mtu.Naamini huyu bwana yuko ndani ya mfumo.Confidence aliyo nayo na taarifa alizonazo haiwezekani mtu wa kawaida kuzipata.
 
yaani wewe ndo unaakili saaan kupita wao
 

Asante Titicomb!
Majibu ya awali ya Msekwa yanaonyesha ukomavu na busara kubwa kushughulikia mambo mazito na ya msingi. Tufahamu kuwa hawa makatibu wastaafu, hususan Kinana kuwa ni watu wenye uelewa mpana sana. Kinana ndiye aliyeikoa CCM baada ya kuzama ikiwa chini ya Makamba na kukaribia kilindini chini ya Mukama. Ni vyema pia kukumbuka kuwa Kinana alihamua kujiuzulu nadhani kutoka kwenye sekretarieti ya wakati huo, kabla ya baadae JK kumuomba awe katibu mkuu. Walioona mbali, akiwemo Mhariri maarufu Kibanda, waliandika kuwa Kinana sio mtu wa kubeza baada tu ya kuchaguliwa kuwa katibu Mkuu. Itoshe tu kusema kuwa Kinana anayafahamu yote haya yaliyosemwa na Msekwa, lakini pia anayafahamu ambayo yangekuwa matokeo endapo barua yao ingewakilishwa kwenye sekretariati ya sasa.
Naamini, kwao hawakutegemea wala kuhitaji makubwa kuliko haya ya kuufahamisha umma juu yanayoendelea na pili, kutokubaliana kwao na sekretariati ya sasa kunyamazia watu kuchafuliwa na kutengeneza dhana inayoyofikiriwa kuwa wao wako nyuma ya huyu mpuliza mbiu.

Hii ni tathmini yangu kadri ya upeo wangu wa siasa za Tanzania.
 
Muoga kwakuwa hajatoa majibu sawa na matarajio yako?
Hekima huepusha mambo mengi sana wakati wote..
Mzee amejibu kihekima sio kimuhemko
Sio tuu kajibu kihekima bali pia ameonesha weledi katika kuilinda katiba na misingi ya chama. Mzee kichwa sana.
 
Tunapozungumzia sakata hili ni lazima tujikite ndani ya sakata lenyewe hasa , yote niliyoandika kuhusu Msekwa haikuwa lawama , bali nilikuwa naionyesha dunia kwamba Msekwa hana uwezo wa kuwa msuluhishi kwenye jambo ambalo anao upande wake , hayuko neutral , ndio maana nikaweka mifano iliyotukuka ! ili uelewe namaanisha nini , halikuwa lengo langu kumuonea Wivu Mzee Msekwa kwa kupata mke ndani ya jumuiya ya ccm
 
Haya ndio makosa ya kisarufi? [emoji23][emoji23][emoji23]Ok hiyo barua ni feki na mzee msekwa anawaunga mkono kina Kinana.

Haya furahi sasa
 
Uwiii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…