Barua ya wazi kwa Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi: Manung'uniko ya Waislamu lazima yafanyiwe kazi

Barua ya wazi kwa Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi: Manung'uniko ya Waislamu lazima yafanyiwe kazi

Kikubwa akikaa rais muislamu achague waislamu wenzake awape nafasi,
akitoka akija mkristo nae aweke wakristo wenzake wapate nafasi,
rais wa kubalance hayupo, na hatokaa awepo, cha muhimu tubadilishane tu pale juu,
akitoka mkristo akae muislamu, hivyo hivyo mpaka mwisho wa dunia.

Hili la mashekh lina ugaidi ndani yake, sasa ishu ya ugaidi bwana, achana nayo, sidhani kama kikwete hakutaka kujua kulikoni, ila alipojua chungu kinanini akaamua afunike kama kilivyo. Magu ni mkristo sio, hata rugemarila ni mkristo si ndio, au anawachanganya na ile kanzu yake, ruge mkristo yulee....mnanisikia au niongeze sauti.

Hii ishu ya udom hii, inasemekana wahusika hawajaonewa.

Kwenye maisha nimewahi kusaidiwa na wakristo na waislamu, nimewahi kukandamizwa na wakristo na waislamu. Binafsi udini si upi kipaumbele sana, bali utu wa mtu. Ukiwa mshenzi hata kama ni wa dini sawa na yangu, nakufyekelea mbali, nenda kashitaki.

Kama la masheikh lina ugaidi , kaisaidie polisi kupeleka kesi mahakamani labda mwenzetu unao ushahidi, ili hawa watu washitakiwe
 
Ndugu mtoa maada unapaswa kutambua kuwa Tanzania ni Nchi isiyoendeshwa kwa matakwa na utashi wa dini ila haizuii uhuru wa mtu kuwa muumini wa dini yoyote ilimradi havunji sheria za nchi. Kwa hivyo basi suala lako litakuwa na manufaa zaidi endapo ungebadili mlengwa na kutuma BAKWATA na nakala ukapeleka baraza la maulamaa.

Tanzania haina dini lakini Wakiristo ni wanufaika zaidi wa ajira na teuzi za serikali.
Kutokana na kunufaika huko wengi miongoni mwao wananufaika na mishahara iliyostable, Bima ya Afya nzuri, Pensheni za uzeeni, mikopo benki n. k
Matokeo yake wanao uwezo wa kusomesha watoto wao shule nzuri, kuwa na makazi stable.
Wakati huo Waislamu kutokana na kutonufaika ipasavyo na keki hiyo ya Taifa ya ajira za serikali , maisha yao yanakuwa siyo bora kama wakiristo, hawanufaiki na bima mzuri ya Afya, pensheni, na faida nyingi zitokanazo na mishahara ya serikali. Sasa katika hali kama hiyo Waislamu wanakuwa kama raia daraja la pili katika nchi yao. Hili halikubaliki, na lazima lifanyiwe kazi ili kuweka usawa na kuondoa manung'uniko ambayo kwa kweli ni madai ya msingi!. Hata mtu ujifanye vipi kuyapuuza, lakini ni madai halali na ya msingi sana!
 
Kama la masheikh lina ugaidi , kaisaidie polisi kupeleka kesi mahakamani labda mwenzetu unao ushahidi, ili hawa watu washitakiwe
Wewe ambae unaona wanaonewa nenda kawatoe tuishi nao uraiani.
 
Tanzania haina dini lakini Wakiristo ni wanufaika zaidi wa ajira na teuzi za serikali.
Kutokana na kunufaika huko wengi miongoni mwao wananufaika na mishahara iliyostable, Bima ya Afya nzuri, Pensheni za uzeeni, mikopo benki n. k
Matokeo yake wanao uwezo wa kusomesha watoto wao shule nzuri, kuwa na makazi stable.
Wakati huo Waislamu kutokana na kutonufaika ipasavyo na keki hiyo ya Taifa ya ajira za serikali , maisha yao yanakuwa siyo bora kama wakiristo, hawanufaiki na bima mzuri ya Afya, pensheni, na faida nyingi zitokanazo na mishahara ya serikali. Sasa katika hali kama hiyo Waislamu wanakuwa kama raia daraja la pili katika nchi yao. Hili halikubaliki, na lazima lifanyiwe kazi ili kuweka usawa na kuondoa manung'uniko ambayo kwa kweli ni madai ya msingi!. Hata mtu ujifanye vipi kuyapuuza, lakini ni madai halali na ya msingi sana!
Kama sababu ni hiyo kwanini usibadili dini ukaungana na unaodhani wanapata upendeleo ili nawe unufaike? Hii ni inferior complex ambayo mara nyingi insumbua sana makundi ama watu wasiojiamini!
Nenda kwa takwimu utueleze ni wapi ndani ya Jamhuri hii ya Muungano ambapo kundi fulani liliitwa kwenye usahili kwa nafasi fulani ila likabaguliwa kwa msingi wa dini.
 
Mimi ni mkristo ila nawaunga mkono kina shekh ponda kwasababu maaskofu wetu waliowengi wako kimya maboko kibao yanafanyika wao wako kimya wanasubiri rais mwislamu aingie madarakani ndio waanze kumsumbua.

Imagine polisi wanavyoonea chadema unreasonably.

Kupigwa risasi 32 kea lisu maaskofu wapo kimya .

Ben Saanane mpaka leo hatujui you mifupa au yupo safe house maaskofu kimya.

Azory kapotea maaskofu Aina ya pengo kimya .

Leo hii mtumishi wa uuma anaepaswa kuwa unbiased anachukua fomu kwa CCM maaskofu kimya.

Ikifika jumapili wanataka tuwapelekee our hard earned money kirahiiiiisiiii pumbav.

Nawapongeza wachache Aina ya bagonza hao Mungu awabariki .
 
Kama sababu ni hiyo kwanini usibadili dini ukaungana na unaodhani wanapata upendeleo ili nawe unufaike? Hii ni inferior complex ambayo mara nyingi insumbua sana makundi ama watu wasiojiamini!
Nenda kwa takwimu utueleze ni wapi ndani ya Jamhuri hii ya Muungano ambapo kundi fulani liliitwa kwenye usahili kwa nafasi fulani ila likabaguliwa kwa msingi wa dini.

Hakuna cha inferiority complex hapa. Huwezi kuteua 80% watu wa dini moja halafu ukaona hilo siyo tatizo!

Wote ni Watanzania, walipa kodi nchi hii, lazima keki ya Taifa igawanywe kwa haki.

Angekuwa rais Muislamu akateua 80% Waislamu nchi hii ingetawalika? , si mgechonga sana humu mitandaoni kama mlivyochonga kipindi kile JK alivyokuwa akiwapa vijinafasi waislamu angalauangalau hata kama kiujumla Wakiristo walikuwa bado ni wengi zaidi kwenye hizo nafasi?
 
Hahahahaaaaq!

Hv huu waraka mbna ww wakristo kule zanzibar tunapata tabu!

Jino kwa jino (mamamamamamamamamamamamamamaaaaaye)
 
Ndugu Bashiru Ally,
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi

Mimi ni mwananchi, raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nimeamua kuchukua wasaa huu kukuandikia haya yafuatayo, kwani kwa haya niyaandikayo naamini ni ya msingi sana katika kukuza umoja na mshikamano wa Taifa letu vitu ambavyo ni muhimu sana katika kuimarisha amani ya Taifa letu. Kwa muktadha huu kuna nukta chache ningependa kukueleza ili chama chako cha Mapinduzi ambacho wewe ni mfuatiliaji mkuu wa utekelezaji wa Ilani yake ni lazima uzielewe na uhakikishe chama chako kinazifanyia kazi.

Ndugu Ponda alisoma waraka mzito sana, waraka wenye mambo mengi yanayohusu Taifa letu kiujumla na mengine exclusively yanayowahusu waislamu. kwa hiyo mimi nitakijikita katika yale yanayowahusu Waislamu.

1. Mosi kuna malalamiko ya muda mrefu ya kuhusu Waislamu kufanywa raia daraja la pili nchini.
Kwa miaka mingi tangu uraisi wa Mwalimu Nyerere, kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa waislamu, kuwa kuna ubaguzi wa kimfumo dhidi yao, miaka ya zamani walikuwa wakitolea mifano kwenye nafasi za elimu ya juu, kuwa inakuwaje Wanaoanzishwa shule darasa la kwanza kuna mamilioni ya vijana wa kiislamu, lakini ukiangalia huko kwenye elimu ya juu vyuoni, waislamu ni wachache sana?

Madai haya ya waislamu yamekuwepo, wengi wamekuwa wakimrejea Kighoma Malima kuwa alisaidia kufanya reforms kadha wa kadha alipoteuliwa na Rais wa awamu ya pili kuwa waziri wa Elimu, Mimi sitaki kujadili ukweli au uongo wa haya madai, bali nataka nikueleze kuwa hizi sentiment zipo katika jamii, waislamu wamekuwa wakizizungumza hizi habari kwa muda mrefu kama sehemu ya historia yao katika harakati za kutafuta namna ya kunufaika na matunda ya uhuru. Ubaya wa historia ni kuwa historia haifi.

Ndugu katibu mkuu ipo haja ya Chama cha Mapinduzi kuja mbele, kuweka rekodi sawa kiwaeleze waislamu kuwa chenyewe kama chama ambacho kwa kauli ya muasisi mwenyewe wa chama hiki aliwahi kukiri waislamu kuwa nyuma kielimu wakati wa uhuru, kije kiwaambie Waislamu, sisi kama chama tumefanya kadha wa kadha juu yenu na sasa hivi tumepata mafanikio kadha wa kadha kwenye suala hili la Elimu. Kwanini hii hoja ya elimu ni muhimu sana? Kwa sababu Elimu inaambatana na ajira, na teuzi mbalimbali serikalini na katika utumishi wa umma. Kwa maana mara nyingi waislamu wanapouliza swali kuwa mbona proportion yetu kwenye teuzi na ajira haiakisi wingi wetu wamekuwa wajibiwa kuwa hamjasoma!

2. Chama cha Mapinduzi lazima kiitake serikali yake itende haki kwa makundi yote ya kijamii
Kwa mujibu wa waraka uliosomwa na Sheikh Ponda, unaoonyesha uwiano wa teuzi kati ya Watanzania wenye imani ya Kikiristo na Watanzania wenye Imani ya Kiislamu ni kwa uwiano wa asilimia 80% wakiristo, na 20%Waislamu.
Ndugu Katibu mkuu by all standards hii haijakaa sawa hata kidogo. Haiyumkiniki katika Taifa ambalo populationwise kila kundi kati ya hayo mawili ndani ya jamii lina idadi kubwa ya kutosha tu ya watu katika jamii lakini linapokuja katika utumishi wa umma na teuzi za serikali kundi moja liko overrepsented huku jingine likionekana likiwa na idadi finyu sana, Kwa namna zozote zile hii asilimia ya 80% kwa 20% haiakisi uhalisia wa demography ya wananchi kwa muktadha wa makundi ya imani zao.

Chama cha Mapinduzi kinapaswa kuja na kuwaangalia waislamu machoni kiwaambie, wao wana shida gani kwa nini ni wachache katika teuzi hizi za serikali, wao hawana nini ambacho wenzao wanacho kiasi kwamba kundi jingine likiwa jingi katika nafasi hizo za teuzi kuliko wao? Zimekuwepo hoja kuwa hateuliwi mtu kwa sababu ya dini yake bali vigezo vingine, Tunataka chama cha mapinduzi kiwaambie waislamu kuwa labda hawana elimu, siyo wazalendo, ni mafisadi, ni wavivu sana, Au kiwaeleze sababu zozote zenye mashiko kwa nini wingi wao katika jamii hauakisi uwepo wao katika utumishi wa serikali?

Ndugu katibu mkuu, Chama cha mapinduzi kinaweza kuamua kukaa kimya utadhani hili tatizo halipo, lakini mimi ningependa kukiambia kuwa, uwepo au kutokuwepo kwa tatizo hilo siyo hoja, hoja ni kuwa waislamu wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu na sisi tunaoitakia amani nchi hii, tunaona kuwa hili ni bomu linalosubiri kupasuka kama ama rekodi zisipowekwa sawa au kufanyiwa kazi na serikali.

Ndugu katibu mkuu, Chama chako cha mapinduzi au serikali zake kamwe zisidhani kuwa madai haya ya waislamu yataisha iwapo kila siku wanakaa wanaona teuzi za serikali moja baada ya nyingine anateuliwa mtu wa imani nyingine huku wao wakiambiwa eti watu hawateuliwi kwa dini zao bali vigezo vingine, kwa nini hivyo vigezo viwe kwa wingi kwa watu wa imani moja tu?

3. Udini ni ufa mkubwa sana wa jamii yetu na ni lazima wote tuungane kuupiga vita
Ndugu katibu mkuu, kama kuna ufa mkubwa zaidi katika nchi yetu basi ni suala la udini, hili ni tatizo ambalo hatupaswi kulipiga vita kwa maneno bali kwa vitendo, na katika kulipiga vita tatizo hilo lazima tulipige vita huku kila mtu akiona kabisa kuwa tuna dhati ya kufanya hivyo, vipo viashiria nchini kuwa watu wa imani moja wanawekwa kwenye mizania tofauti pindi wanapofanya mambo fulani yenye kuashiria udini, na mambo haya yanawafanya watu wa dini nyingine wajihisi kuwa ni kutokana na mfumo kuinua kundi fulani ndiyo maana kundi hilo linajihisi kufanya mambo with impunity.

Katibu mkuu nitakupa mfano, Mkuu wa mkoa wa mmoja nchini anatoa kauli kuwa Nchi hii iko chini ya kanisa, hasemi iko chini ya Mungu, anasema iko chini ya kanisa na wala hashughulikiwi na serikali ya chana chsko kwa uchochezi. Waziri mmoja mwandamizi anafanya kampeni katika kanisa kwa kutandika bendera ya chama ndani ya madhabahu, Viongozi wa imani moja wakikemea serikali kwa kauli na maandishi (Japo ni haki yao) hawakamatwi lakini kiongozi wa dini ya Kiislamu anaposimama na kutumia haki yake ya kutoa mapendekezo na maoni yake anakamatwa na kuswekwa ndani bila kufikishwa mahakamani ndani ya muda maalumu kinyume cha sheria.

Ndugu katibu mkuu, katika muktadha huu kwa nini Waislamu wasikiwekee chama chako na serikali yake alama ya kuuliza kuwa huenda vinalea na kuendekeza udini wa imani mmoja nchini?

4. Suala la kuhamisha wahadhiri na watumishi 11 wa Imani moja Chuo cha UDOM na kuleta wengine 11 wa imani nyingine linahitaji uchunguzi
Ndugu katibu mkuu, nilistushwa sana na hili suala kama ambavyo lilielezwa kwa kina kwenye waraka wa Sheikh Ponda.
Nimejiuliza kuwa iweje katika utumishi uhamishe watu kwa mkupuo halafu ionekane wote ni wa imani moja halafu waletwe wengine 11 na wote wawe wa imani moja, hili linatoa picha gani, limebeba ajenda gani, hao waliofanya uhamisho huo walitaka kuachieve kitu gani?

Wazungu wana msemo kuwa, ukiona inatweta kama bata, inatembea kama bata na inalia kama bata basi hiyo ni bata. Inawezekana vipi kwa kanuni zozote zile za nasibu uondoe watu 11 wenye kufuata mrengo wa dini moja sehemu halafu wakati huohuo ulete wengine 11 wa dini nyingine kama maamuzi ya kufanya hivyo hayakusukumwa na udini uliokubuhu katika kufanya maamuzi hayo basi ni kitu gani?. Cha kusikitisha zaidi waraka ukaenda mbele na kusema wazi kuwa wengine kstika wale waliohamishwa walirnda kupewa nafasi za chini kuliko hadhi yao.

Ndugu katibu mkuu, tunakitaka chama chako kifanye uchunguzi au kiilazimishe serikali yake ichunguze na iwaeleze Watanzania ni sababu gani za msingi hatua hiyo ilifikiwa na kwa nini ionekane watu wa dini moja ndiyo wanakumbwa na zoezi la kuondolewa mahali na wakaletwa wengine wote wa imani ya dini nyingine.

Hoja kuwa serikali inaweza kumhamisha yeyote na kumleta yeyote katika utumishi wa umma ni kweli lakini kwa muktadha huu haina mashiko maana inaonyesha kuwa kuna msukumo fulani wa maamuzi ambayo yameacha question marks na kwa kuwa kuna umma hususan wa kiislamu unadhani kuwa kuna nia isiyo njema imesukuma maamuzi hayo, tunakitaka chama cha Mapinduzi kitoe maelezo kwa nini uamuzi tata huo ulifikiwa ili kusafisha hali hii inayoweza kupelekea hisia hasi zinazoweza kupelekea kuvunjika kwa amani.

5. Chama cha mapinduzi na serikali yake kijifunze kwa maandamano yanayotokea marekani kupinga ubaguzi
Huko Marekani kulikuwepo na manung'uniko ya muda mrefu, watu weusi wakilslamika hadharani na sirini kuhusu ubaguzi wa kimfumo dhidi yao, walilamika kuhusu ubaguzi katika uchumi, katika mifumo ya utoaji haki nchini humo, walilamika hadi upataji wa ajira katika serikali ya Shirikisho na hata za majimbo.

Manung'uniko yao yalikuwa yakipuuzwa kwa madai kuwa marekani hakuna ubaguguzi wowote bali ni inferiority complex yao tu na uvivu wao wa kutofanya kazi. Ikawa inatolewa mifano michache kuwa mbona fulani na fulani ni weusi na matajiri, ni wacheza kikapu maarufu, ni wacheza sinema maarufu n. k. Hata hivyo pamoja na kauli hizi donge lilikuwa bado limo katika mioyo ya wamarekani weusi maana wanasema yule avaaye kiatu, yeye ndiye anayeona wapi kinambana. Leo Marekani hali imekuwa tete baada ya wamarekani weusi na wale wapenda haki kuingia mitaani kuonyesha ghadhabu yao juu ya matendo hayo baada ya kifo cha kikatili cha George Floyd kilichosababishwa na ukatili wenye dalili zote za ubaguzi wa rangi.

Ndugu Katibu Mkuu, madai haya ya Waislamu hapa nchini haijalishi ni ya kweli au siyo kweli lakini yapo, madai haya yanahitaji majibu au hatua ya kuyarekebisha ili yasije kuendelea kujenga ghadhabu ya kimya kimya ambayo siku moja ikitoka nje, sisi kama taifa tutakuja kuwa na wakati mgumu sana. Kamwe tusijenge Kiburi kuwa vyombo vya usalama vitawashughulikia wote hao wenye kuleta madai haya. Ndugu katibu mkuu hata katika hivyo vyombo vya usalama kunaweza kukawemo watu walioaminishwa dhana hizo iwapo zitaachwa bila kushughulikiwa na ikitokea hali hiyo Taifa liktakuwa katika sintofahamu kubwa. Wahenga walisema Kinga ni bora kuliko tiba, yatupasa kama Taifa kulitafutia ufumbuzi suala hili badala ya kujidai kuwa halipo.

6. Ni muda muafaka sasa Masheikh walioko jela waachiwe huru bila masharti yoyote
Ndugu katibu mkuu, ni mwaka takriban wa 8 sasa Masheikh wapo jela bila kuhukumiwa na mahakama yoyote, Makosa yao hayajathibitishwa mahakamani, kwa hiyo madai na hoja zilizosomwa na Sheikh Ponda zina. mashiko
Tunakitaka chama cha mapinduzi kiisimamie serikali yake izingatie utawala wa sheria.

Chama kiulize serikali yake, inaendelea kuwashikilia Masheikh hao kwa uhalali upi wa kisheria?. Kama uchunguzi haujakamilika, kama huo uchunguzi haujakamilika miaka 8 utakamilika lini? Je, haki inatendeka kwa hawa nasheikh au kuna namna yoyote ya kuamua kuwakomoa?

Ndugu katibu mkuu hawa Masheikh walikamatwa Zanzibar, kama lengo ni Justice au haki kwa nini ilazimishwe washitakiwe Tanzania bara na di hukohuko Zanzibar walipotenda kosa lolote inalodaiwa walitenda?

Hitimisho:
Ndugu katibu mkuu, yapo madai ambayo waislamu wamekuwa wakidai miaka nenda rudi, na kuna mambo wamekuwa wakiyawekea question mark kama vile teuzi katika awamu hii.

Sasa sisi kama raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaona kuwa haya madai yasipojibiwa huenda yakaitia nchi katika uwezekano wa kuvunja mshikamano wa kitaifa na kuvunja amani huko mbele.

Sasa kwa kuwa watu wa aina yangu tunaipenda nchi yetu, si busara kuacha kutoa mchango wa mawazo katika mambo kama haya hata kama ni tata kiasi gani(controversial). Ndiyo maana kwa muktadha huu tunakitaka chsma cha Mapinduzi kijibu hoja za waislamu ili kutunza huo mshikamano!

Ndugu Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi waislamu wana hoja zijibuni

Missile of the Nation (Kombora hatari kabisa la ulinzi wa Taifa)

Nakala kwa:
1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2. Waziri Mkuu
3. Mkurugenzi Usalama wa Taifa
Hii sio lazima ajibu Bashiru Ally

1. Kwani Udom hakuna wahadhiri waislamu kwa sasa? Mimi najua wapo wengi nawafahamu.
Kuhamishwa wahadhiri,kwani wamefukuzwa kazi? Acheni utoto ktk mambo ya maana.

2. Waislam hawajaweka Elimu dunia kama kipaumbele chao,nenda kilwa,Pwani yote na miji inayofanana na hiyo hawasomi elimu dunia,dhamira yao kubwa ni kwenda kwa mungu. Mkoa wa Lindi na Mtwara hasa elimu IPO chini sababu wengi ni waislamu(natokea huko)

3. Ukichukua takwimu za wasomi wa nchi hii,utakuta wakristo ni wengi kuliko waislamu,ukiondoa wachache wanaoibuka sasa hivi. Mfano nikiwa chuo kikuu tulikuwa wanafunzi 33 darasani ila waislamu ni 5 tu,nikiwa A level wanafunzi zaidi ya 18000,ila waislamu walikuwa 30% tu,
Kwa takwimu hizi unategemea nini.

4. Halafu Ponda amesahau kuleta na takwimu ya idadi ya waislamu against ya wakristo Tanzania,alichofanya ni kukurupuka tu.

5. Chuo kikuu cha waislamu kipo morogoro lakini ukiangalia udahili pale hukuti mkristo hata mmoja,vyuo vya kikristo wanasoma na waislamu,wakristo hawapigi kelele,ila ingekuwa viceversa ungeona maandamano ya waislamu.

6. Waislamu waache inferiority complex na wachape kazi, tunaishi nao,tunajua wanasisitiza nini zaidi ya elimu dunia.


Mwisho,niseme nimejibu sio kwa kufuata series ya maswali yake.
Ila Naomba yafuatayo:-

1. Idadi ya wakristo against waislamu

2. Idadi ya wasomi wakristo against waislamu.

3. Tuletee idadi ya wahadhiri/wafanyakaxi wa udom waislamu against wakristo.

Ahsante
Ni Mimi Stesheni
Mwananchi
 
Hahahahaaaaq!

Hv huu waraka mbna ww wakristo kule zanzibar tunapata tabu!

Jino kwa jino (mamamamamamamamamamamamamamaaaaaye)

Zanzibar ni nchi, wana serikali yao, wana bunge lao(baraza la wawakilishi), kuna kazi huko Zanzibar hata uwe muislamu wa Tanganyika huwezi pewa!, kwa hiyo wacha Wazanzibari wajisemee wenyewe kwenye mambo ya nchi yao, na sisi huku Tanganyika tujisemee yetu
 
Tujiulize kabla ya uhuru kulikuwa na Seminary za kikristo ngapi na sasa zipo ngapi na shule za umma kabla ya uhuru zilikuwa ngapi na sasa zipo ngapi? Je mitazamo ya dini zetu katika elimu ikoje? Wachina wameendelea sana sababu ya kufanya kazi na sio kuleta mambo ya dini kwenye taasisi za uma, hivi kweli kuna mtu anaweza kuwa na elimu ya kutosha na utaalam akaachwa kuajiriwa kwa ajili ya dini yake?

Binafsi huwa namshangaa sana binadamu anayekuwa na fikri za kikabila, ukanda, rangi na dini tunasahau ya kuwa binadamu wote ni sawa na tumezaliwa katika mfumo unaofanana na damu zetu wote ni nyekundu. Tukianza ubaguzi tutajikuta hata tunaojiona tunafanana hatufanani tena, tutaanza kujitenga wale wenye group O negative la damu nao wataanza kulalamika kwa nini wao ndio wanawajibika kuongezea damu kila mtu, wale wenye group zingine nao watahisi O anawasimanga.
 
Hii sio lazima ajibu Bashiru Ally

1. Kwani Udom hakuna wahadhiri waislamu kwa sasa? Mimi najua wapo wengi nawafahamu.
Kuhamishwa wahadhiri,kwani wamefukuzwa kazi? Acheni utoto ktk mambo ya maana.

2. Waislam hawajaweka Elimu dunia kama kipaumbele chao,nenda kilwa,Pwani yote na miji inayofanana na hiyo hawasomi elimu dunia,dhamira yao kubwa ni kwenda kwa mungu. Mkoa wa Lindi na Mtwara hasa elimu IPO chini sababu wengi ni waislamu(natokea huko)

3. Ukichukua takwimu za wasomi wa nchi hii,utakuta wakristo ni wengi kuliko waislamu,ukiondoa wachache wanaoibuka sasa hivi. Mfano nikiwa chuo kikuu tulikuwa wanafunzi 33 darasani ila waislamu ni 5 tu,nikiwa A level wanafunzi zaidi ya 18000,ila waislamu walikuwa 30% tu,
Kwa takwimu hizi unategemea nini.

4. Halafu Ponda amesahau kuleta na takwimu ya idadi ya waislamu against ya wakristo Tanzania,alichofanya ni kukurupuka tu.

5. Chuo kikuu cha waislamu kipo morogoro lakini ukiangalia udahili pale hukuti mkristo hata mmoja,vyuo vya kikristo wanasoma na waislamu,wakristo hawapigi kelele,ila ingekuwa viceversa ungeona maandamano ya waislamu.

6. Waislamu waache inferiority complex na wachape kazi, tunaishi nao,tunajua wanasisitiza nini zaidi ya elimu dunia.


Mwisho,niseme nimejibu sio kwa kufuata series ya maswali yake.
Ila Naomba yafuatayo:-

1. Idadi ya wakristo against waislamu

2. Idadi ya wasomi wakristo against waislamu.

3. Tuletee idadi ya wahadhiri/wafanyakaxi wa udom waislamu against wakristo.

Ahsante
Ni Mimi Stesheni
Mwananchi

Hayo ya Inferiority complex unayajua wewe lakini teuzi za 80% watu wa dini moja siyo jambo la kawaida hilo kuna harufu kali ya udini hapo!

Haiwezekani ubague watu kwa misingi ya dini kisha wakihoji uwape majibu ya nyodo, kuita madai yao ni "utoto", " inferiority complex", "hawajasoma" wala haisaidii.

Teuzi za serikalini hazihitaji watu mamilioni, zinahitaji mamia kadhaa na idadi hiyo Waislamu wanayo ya kutosha tu!.

Pia siku hizi waislamu waliosoma ni wengi, hata Nyerere mwaka 1985 kwenye hotuba yake ya kuaga pale diamond Jubilee ailikiri kuwa Waislamu waliosoma waliongezeka sana kulinganisha na mwaka 1961, Sasa kwa nini watu wa imani moja wawe overrepresented kuliko watu wa imani nyingine, kama siyo udini ni kitu gani?
 
Mkuu, hilo la uwiano ktk teuzi serikalini ni ukweli mtupu. Kwa jamii yenye makundi makubwa mawili ya kiimani, pale inapotokea kundi moja likionekana dhahiri likiwa na teuzi chache mno kulinganisha na lingine, kwa vyovyote vile huwezi kukwepa hisia kama hizi, kwa kuwa kundi kama hilo huku na likitemgwa na hata kukosa "ownership"

Waraka wa Ponda kimantiki ulipaswa kuchukuliwa kama kichocheo cha fikra ktk kutaka kujitathimini yenyewe ktk jambo hilo. Ponda hakutaka kuwa mnafiki bali kupaza sauti ili kile kinachozungumzwa mafichoni kikapate kusikika. Hii ni Tanzania iliyo makazi ya wananchi wote, ijapokuwa serikali yetu haina dini, bali ni lazima iyaangalie kwa umuhimu wa are na yake makundi mbalimbali ya kidini yenye watu wengi ndani ya mifumo yake.

Kundi kubwa la Waisilamu lina wasomi wengi mno, tena wa viwango tofauti. Visitafutwe visingizio ile kukwepa kulizungimzia suala hili kwa uzito wake. Mbona wakati wa utawala wa awamu ya nne, tulishuhudia nyaraka na malalamiko kama hayo kutoka kwa Wakristo ijapokuwa Mzee Kikwete alijitahidi mno kuzingatia uwiano huu?
 
Ujitambui kweli wewe inamana wewe ni muelewa Sana kuliko Samia Suluhu, Majaliwa,
 
Tanzania haina dini lakini Wakiristo ni wanufaika zaidi wa ajira na teuzi za serikali.
Kutokana na kunufaika huko wengi miongoni mwao wananufaika na mishahara iliyostable, Bima ya Afya nzuri, Pensheni za uzeeni, mikopo benki n. k
Matokeo yake wanao uwezo wa kusomesha watoto wao shule nzuri, kuwa na makazi stable.
Wakati huo Waislamu kutokana na kutonufaika ipasavyo na keki hiyo ya Taifa ya ajira za serikali , maisha yao yanakuwa siyo bora kama wakiristo, hawanufaiki na bima mzuri ya Afya, pensheni, na faida nyingi zitokanazo na mishahara ya serikali. Sasa katika hali kama hiyo Waislamu wanakuwa kama raia daraja la pili katika nchi yao. Hili halikubaliki, na lazima lifanyiwe kazi ili kuweka usawa na kuondoa manung'uniko ambayo kwa kweli ni madai ya msingi!. Hata mtu ujifanye vipi kuyapuuza, lakini ni madai halali na ya msingi sana!
Yes, ni vicious circle! Tatizo letu kubwa ni 'mfumo kristo' ambao kwa sehemu kubwa unatufanya tusione dhulma mbalimbali. Ni kama mfumo dume tu unavyofanya kazi. ...inahitaji tafakari kubwa kuweza kuziona dhulma mbalimbali. Ndio sababu hata kiongozi akiwa muislamu, mfumo huo unamfanya asione hizo dhulma. Ni kama ilivyo kwa mfumo dume, hata viongozi wanawake wanajikuta wakitenda kulingana na mfumo unavyotaka.

Sasa badala ya kuwafunga midomo watu wanaweza kutuonesha dhulma hizo na udhaifu wa mfumo uliopo, tungewaacha waseme ili kuweza kufanyia marekebisho. Hata kama hatukubaliani na wanayosema au kuyataka, lakini ni muhimu kusikiliza perspectives zao kwa sababu kuna kitu tutajifunza.

Bahati nzuri nchi yetu imechanganyika sana. Mimi ni mkristo, lakini ninao ndugu wa damu waislamu. Ninaamini watu wengi pia tupo hivyo.

Tuwasikilize wanachosema......kati yake zipo hoja zenye mashiko tu kama tukiamua kusikiliza objectively.
 
Ndugu Bashiru Ally,
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi

Mimi ni mwananchi, raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nimeamua kuchukua wasaa huu kukuandikia haya yafuatayo, kwani kwa haya niyaandikayo naamini ni ya msingi sana katika kukuza umoja na mshikamano wa Taifa letu vitu ambavyo ni muhimu sana katika kuimarisha amani ya Taifa letu. Kwa muktadha huu kuna nukta chache ningependa kukueleza ili chama chako cha Mapinduzi ambacho wewe ni mfuatiliaji mkuu wa utekelezaji wa Ilani yake ni lazima uzielewe na uhakikishe chama chako kinazifanyia kazi.

Ndugu Ponda alisoma waraka mzito sana, waraka wenye mambo mengi yanayohusu Taifa letu kiujumla na mengine exclusively yanayowahusu waislamu. kwa hiyo mimi nitakijikita katika yale yanayowahusu Waislamu.

1. Mosi kuna malalamiko ya muda mrefu ya kuhusu Waislamu kufanywa raia daraja la pili nchini.
Kwa miaka mingi tangu uraisi wa Mwalimu Nyerere, kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa waislamu, kuwa kuna ubaguzi wa kimfumo dhidi yao, miaka ya zamani walikuwa wakitolea mifano kwenye nafasi za elimu ya juu, kuwa inakuwaje Wanaoanzishwa shule darasa la kwanza kuna mamilioni ya vijana wa kiislamu, lakini ukiangalia huko kwenye elimu ya juu vyuoni, waislamu ni wachache sana?

Madai haya ya waislamu yamekuwepo, wengi wamekuwa wakimrejea Kighoma Malima kuwa alisaidia kufanya reforms kadha wa kadha alipoteuliwa na Rais wa awamu ya pili kuwa waziri wa Elimu, Mimi sitaki kujadili ukweli au uongo wa haya madai, bali nataka nikueleze kuwa hizi sentiment zipo katika jamii, waislamu wamekuwa wakizizungumza hizi habari kwa muda mrefu kama sehemu ya historia yao katika harakati za kutafuta namna ya kunufaika na matunda ya uhuru. Ubaya wa historia ni kuwa historia haifi.

Ndugu katibu mkuu ipo haja ya Chama cha Mapinduzi kuja mbele, kuweka rekodi sawa kiwaeleze waislamu kuwa chenyewe kama chama ambacho kwa kauli ya muasisi mwenyewe wa chama hiki aliwahi kukiri waislamu kuwa nyuma kielimu wakati wa uhuru, kije kiwaambie Waislamu, sisi kama chama tumefanya kadha wa kadha juu yenu na sasa hivi tumepata mafanikio kadha wa kadha kwenye suala hili la Elimu. Kwanini hii hoja ya elimu ni muhimu sana? Kwa sababu Elimu inaambatana na ajira, na teuzi mbalimbali serikalini na katika utumishi wa umma. Kwa maana mara nyingi waislamu wanapouliza swali kuwa mbona proportion yetu kwenye teuzi na ajira haiakisi wingi wetu wamekuwa wajibiwa kuwa hamjasoma!

2. Chama cha Mapinduzi lazima kiitake serikali yake itende haki kwa makundi yote ya kijamii
Kwa mujibu wa waraka uliosomwa na Sheikh Ponda, unaoonyesha uwiano wa teuzi kati ya Watanzania wenye imani ya Kikiristo na Watanzania wenye Imani ya Kiislamu ni kwa uwiano wa asilimia 80% wakiristo, na 20%Waislamu.
Ndugu Katibu mkuu by all standards hii haijakaa sawa hata kidogo. Haiyumkiniki katika Taifa ambalo populationwise kila kundi kati ya hayo mawili ndani ya jamii lina idadi kubwa ya kutosha tu ya watu katika jamii lakini linapokuja katika utumishi wa umma na teuzi za serikali kundi moja liko overrepsented huku jingine likionekana likiwa na idadi finyu sana, Kwa namna zozote zile hii asilimia ya 80% kwa 20% haiakisi uhalisia wa demography ya wananchi kwa muktadha wa makundi ya imani zao.

Chama cha Mapinduzi kinapaswa kuja na kuwaangalia waislamu machoni kiwaambie, wao wana shida gani kwa nini ni wachache katika teuzi hizi za serikali, wao hawana nini ambacho wenzao wanacho kiasi kwamba kundi jingine likiwa jingi katika nafasi hizo za teuzi kuliko wao? Zimekuwepo hoja kuwa hateuliwi mtu kwa sababu ya dini yake bali vigezo vingine, Tunataka chama cha mapinduzi kiwaambie waislamu kuwa labda hawana elimu, siyo wazalendo, ni mafisadi, ni wavivu sana, Au kiwaeleze sababu zozote zenye mashiko kwa nini wingi wao katika jamii hauakisi uwepo wao katika utumishi wa serikali?

Ndugu katibu mkuu, Chama cha mapinduzi kinaweza kuamua kukaa kimya utadhani hili tatizo halipo, lakini mimi ningependa kukiambia kuwa, uwepo au kutokuwepo kwa tatizo hilo siyo hoja, hoja ni kuwa waislamu wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu na sisi tunaoitakia amani nchi hii, tunaona kuwa hili ni bomu linalosubiri kupasuka kama ama rekodi zisipowekwa sawa au kufanyiwa kazi na serikali.

Ndugu katibu mkuu, Chama chako cha mapinduzi au serikali zake kamwe zisidhani kuwa madai haya ya waislamu yataisha iwapo kila siku wanakaa wanaona teuzi za serikali moja baada ya nyingine anateuliwa mtu wa imani nyingine huku wao wakiambiwa eti watu hawateuliwi kwa dini zao bali vigezo vingine, kwa nini hivyo vigezo viwe kwa wingi kwa watu wa imani moja tu?

3. Udini ni ufa mkubwa sana wa jamii yetu na ni lazima wote tuungane kuupiga vita
Ndugu katibu mkuu, kama kuna ufa mkubwa zaidi katika nchi yetu basi ni suala la udini, hili ni tatizo ambalo hatupaswi kulipiga vita kwa maneno bali kwa vitendo, na katika kulipiga vita tatizo hilo lazima tulipige vita huku kila mtu akiona kabisa kuwa tuna dhati ya kufanya hivyo, vipo viashiria nchini kuwa watu wa imani moja wanawekwa kwenye mizania tofauti pindi wanapofanya mambo fulani yenye kuashiria udini, na mambo haya yanawafanya watu wa dini nyingine wajihisi kuwa ni kutokana na mfumo kuinua kundi fulani ndiyo maana kundi hilo linajihisi kufanya mambo with impunity.

Katibu mkuu nitakupa mfano, Mkuu wa mkoa wa mmoja nchini anatoa kauli kuwa Nchi hii iko chini ya kanisa, hasemi iko chini ya Mungu, anasema iko chini ya kanisa na wala hashughulikiwi na serikali ya chana chsko kwa uchochezi. Waziri mmoja mwandamizi anafanya kampeni katika kanisa kwa kutandika bendera ya chama ndani ya madhabahu, Viongozi wa imani moja wakikemea serikali kwa kauli na maandishi (Japo ni haki yao) hawakamatwi lakini kiongozi wa dini ya Kiislamu anaposimama na kutumia haki yake ya kutoa mapendekezo na maoni yake anakamatwa na kuswekwa ndani bila kufikishwa mahakamani ndani ya muda maalumu kinyume cha sheria.

Ndugu katibu mkuu, katika muktadha huu kwa nini Waislamu wasikiwekee chama chako na serikali yake alama ya kuuliza kuwa huenda vinalea na kuendekeza udini wa imani mmoja nchini?

4. Suala la kuhamisha wahadhiri na watumishi 11 wa Imani moja Chuo cha UDOM na kuleta wengine 11 wa imani nyingine linahitaji uchunguzi
Ndugu katibu mkuu, nilistushwa sana na hili suala kama ambavyo lilielezwa kwa kina kwenye waraka wa Sheikh Ponda.
Nimejiuliza kuwa iweje katika utumishi uhamishe watu kwa mkupuo halafu ionekane wote ni wa imani moja halafu waletwe wengine 11 na wote wawe wa imani moja, hili linatoa picha gani, limebeba ajenda gani, hao waliofanya uhamisho huo walitaka kuachieve kitu gani?

Wazungu wana msemo kuwa, ukiona inatweta kama bata, inatembea kama bata na inalia kama bata basi hiyo ni bata. Inawezekana vipi kwa kanuni zozote zile za nasibu uondoe watu 11 wenye kufuata mrengo wa dini moja sehemu halafu wakati huohuo ulete wengine 11 wa dini nyingine kama maamuzi ya kufanya hivyo hayakusukumwa na udini uliokubuhu katika kufanya maamuzi hayo basi ni kitu gani?. Cha kusikitisha zaidi waraka ukaenda mbele na kusema wazi kuwa wengine kstika wale waliohamishwa walirnda kupewa nafasi za chini kuliko hadhi yao.

Ndugu katibu mkuu, tunakitaka chama chako kifanye uchunguzi au kiilazimishe serikali yake ichunguze na iwaeleze Watanzania ni sababu gani za msingi hatua hiyo ilifikiwa na kwa nini ionekane watu wa dini moja ndiyo wanakumbwa na zoezi la kuondolewa mahali na wakaletwa wengine wote wa imani ya dini nyingine.

Hoja kuwa serikali inaweza kumhamisha yeyote na kumleta yeyote katika utumishi wa umma ni kweli lakini kwa muktadha huu haina mashiko maana inaonyesha kuwa kuna msukumo fulani wa maamuzi ambayo yameacha question marks na kwa kuwa kuna umma hususan wa kiislamu unadhani kuwa kuna nia isiyo njema imesukuma maamuzi hayo, tunakitaka chama cha Mapinduzi kitoe maelezo kwa nini uamuzi tata huo ulifikiwa ili kusafisha hali hii inayoweza kupelekea hisia hasi zinazoweza kupelekea kuvunjika kwa amani.

5. Chama cha mapinduzi na serikali yake kijifunze kwa maandamano yanayotokea marekani kupinga ubaguzi
Huko Marekani kulikuwepo na manung'uniko ya muda mrefu, watu weusi wakilslamika hadharani na sirini kuhusu ubaguzi wa kimfumo dhidi yao, walilamika kuhusu ubaguzi katika uchumi, katika mifumo ya utoaji haki nchini humo, walilamika hadi upataji wa ajira katika serikali ya Shirikisho na hata za majimbo.

Manung'uniko yao yalikuwa yakipuuzwa kwa madai kuwa marekani hakuna ubaguguzi wowote bali ni inferiority complex yao tu na uvivu wao wa kutofanya kazi. Ikawa inatolewa mifano michache kuwa mbona fulani na fulani ni weusi na matajiri, ni wacheza kikapu maarufu, ni wacheza sinema maarufu n. k. Hata hivyo pamoja na kauli hizi donge lilikuwa bado limo katika mioyo ya wamarekani weusi maana wanasema yule avaaye kiatu, yeye ndiye anayeona wapi kinambana. Leo Marekani hali imekuwa tete baada ya wamarekani weusi na wale wapenda haki kuingia mitaani kuonyesha ghadhabu yao juu ya matendo hayo baada ya kifo cha kikatili cha George Floyd kilichosababishwa na ukatili wenye dalili zote za ubaguzi wa rangi.

Ndugu Katibu Mkuu, madai haya ya Waislamu hapa nchini haijalishi ni ya kweli au siyo kweli lakini yapo, madai haya yanahitaji majibu au hatua ya kuyarekebisha ili yasije kuendelea kujenga ghadhabu ya kimya kimya ambayo siku moja ikitoka nje, sisi kama taifa tutakuja kuwa na wakati mgumu sana. Kamwe tusijenge Kiburi kuwa vyombo vya usalama vitawashughulikia wote hao wenye kuleta madai haya. Ndugu katibu mkuu hata katika hivyo vyombo vya usalama kunaweza kukawemo watu walioaminishwa dhana hizo iwapo zitaachwa bila kushughulikiwa na ikitokea hali hiyo Taifa liktakuwa katika sintofahamu kubwa. Wahenga walisema Kinga ni bora kuliko tiba, yatupasa kama Taifa kulitafutia ufumbuzi suala hili badala ya kujidai kuwa halipo.

6. Ni muda muafaka sasa Masheikh walioko jela waachiwe huru bila masharti yoyote
Ndugu katibu mkuu, ni mwaka takriban wa 8 sasa Masheikh wapo jela bila kuhukumiwa na mahakama yoyote, Makosa yao hayajathibitishwa mahakamani, kwa hiyo madai na hoja zilizosomwa na Sheikh Ponda zina. mashiko
Tunakitaka chama cha mapinduzi kiisimamie serikali yake izingatie utawala wa sheria.

Chama kiulize serikali yake, inaendelea kuwashikilia Masheikh hao kwa uhalali upi wa kisheria?. Kama uchunguzi haujakamilika, kama huo uchunguzi haujakamilika miaka 8 utakamilika lini? Je, haki inatendeka kwa hawa nasheikh au kuna namna yoyote ya kuamua kuwakomoa?

Ndugu katibu mkuu hawa Masheikh walikamatwa Zanzibar, kama lengo ni Justice au haki kwa nini ilazimishwe washitakiwe Tanzania bara na di hukohuko Zanzibar walipotenda kosa lolote inalodaiwa walitenda?

Hitimisho:
Ndugu katibu mkuu, yapo madai ambayo waislamu wamekuwa wakidai miaka nenda rudi, na kuna mambo wamekuwa wakiyawekea question mark kama vile teuzi katika awamu hii.

Sasa sisi kama raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaona kuwa haya madai yasipojibiwa huenda yakaitia nchi katika uwezekano wa kuvunja mshikamano wa kitaifa na kuvunja amani huko mbele.

Sasa kwa kuwa watu wa aina yangu tunaipenda nchi yetu, si busara kuacha kutoa mchango wa mawazo katika mambo kama haya hata kama ni tata kiasi gani(controversial). Ndiyo maana kwa muktadha huu tunakitaka chsma cha Mapinduzi kijibu hoja za waislamu ili kutunza huo mshikamano!

Ndugu Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi waislamu wana hoja zijibuni

Missile of the Nation (Kombora hatari kabisa la ulinzi wa Taifa)

Nakala kwa:
1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
2. Waziri Mkuu
3. Mkurugenzi Usalama wa Taifa

Tatizo hamna umoja thus mnaburuzwa,lipeni kisasi October ili kukomesha udhalimu.
 
Hayo ya Inferiority complex unayajua wewe lakini teuzi za 80% watu wa dini moja siyo jambo la kawaida hilo kuna harufu kali ya udini hapo!

Haiwezekani ubague watu kwa misingi ya dini kisha wakihoji uwape majibu ya nyodo, kuita madai yao ni "utoto", " inferiority complex", "hawajasoma" wala haisaidii.

Teuzi za serikalini hazihitaji watu mamilioni, zinahitaji mamia kadhaa na idadi hiyo Waislamu wanayo ya kutosha tu!.

Pia siku hizi waislamu waliosoma ni wengi, hata Nyerere mwaka 1985 kwenye hotuba yake ya kuaga pale diamond Jubilee ailikiri kuwa Waislamu waliosoma waliongezeka sana kulinganisha na mwaka 1961, Sasa kwa nini watu wa imani moja wawe overrepresented kuliko watu wa imani nyingine, kama siyo udini ni kitu gani?
Ndio watu wa aina yako wapewe vyeo kweli? Umejibu nini hapo. Tafuta data ujue unachoandika.
Ponda ana kesi ya kujibu,kuna sheria ya takwimu ilipitishwa bungeni.

Analo hilo
Jibu swali na sio blabla
Wanaotaka kwenda mbinguni wasomee huko na wanaosomea ajira wasomee huko.
Tutasomana tu.
Soma vizuri nilichoandika mwanzo utaelewa tu. Wewe umesoma tu inferiority complex, mengine hujaona
 
Back
Top Bottom