Barua ya Wazi Kwa Comrade Ally Saleh, Uchaguzi Umekwisha, Yaliyopita Si Ndwele, Tugange Yaliyopo na Yajayo, Pelekeni Majina, Muijenge Zanzibar Yenu!

Paskali,Mtu YEYOTE mwenye aKili za kawaida hata Kama Hana Shule kubwa, Ataona maandiko yako siku zote yamejaa kujipendekeza kwa Mkulu ili upate Cheo.Yaani hayana ladha ya ushauri wa kweli.Yamejaa Uhalisia wa kujipendekeza zaidi badala ya ushauri unaojifanya kuutoa.
 
Salaam P. Nimesoma andiko lako hakika limejaa hoja zenye Mantiki katika kutatua sintofahamu baina ya Upinzani na Chama tawala, Bila Shaka wahusika wataupokea ushauri wako na kuufanyia kazi.
 
Haoni hata aibu
 
Sina Shaka Nae Maalim kwenye ili...
 
Mkuu Nsoji go Nvaa, sijasema uchaguzi ulikuwa sawa, nimesema ulikuwa na dosari ndogondogo, ambazo zisinge badili matokeo.
P
Kwako wewe karatasi za kura kuzagaa, baadhi ya wagombea kutopewa ruhusa ya kugombea mapema baada ya kuzuiwa bila sababu,askari polisi kuwa wasimamizi wa uchaguzi badala ya kusubiri kuitwa kwenye tatizo, baadhi ya watu kupiga kura mapema bila sababu inayoeleweka na matokeo ya kura hizi kutotangazwa na kulazimisha ushindi bila kuhesabu kura! Kwako wewe kwa kuwa no sehemu ya wababe unaona ni matatizo madogomadogo kama time ilivyosema! Wengi tulikata tamaa kushiriki chaguzi hizi za kibabe ila uchaguzi huutulidhani mambo yangeenda sivyo yalivyokwenda, siku zote aliyezoea kuonea akisemwa anaona anaonewa
 
Peleka yale majina ya majeshi ya warwanda na wa tanganyika wakaunde serikali.

Msilazimishe maji kuyaita mma.

Ujinga wenu wakuuwa watu kwa sababu yq madaraka ndio unataka leo waingiie kwemye serikali ya kidhalimu iliyofanya na kuratibu mauaji pemba na unguja?

Wewe sindiye ulikuwa ukishadidia piga uwa lakini ccm ishinde. Sasa ushauri huu ni wanini wakati mlilolitaka mmefanikiwa.

Wacha unafiki wenu hizo ngonjera bakia nazo hukohuko tanganyika.

Umefurahia kila baya lilitokea Zanzibar.

Huko kuua,kuteka na kupiga watu ndio kukubalika kwa ccm kwasababu mlijenga vidaraja kwa misaada ya wazungu?
 
CCM , kamati ya maadili na madaraka ya bunge wamekupa kazi ngumu sana kuupamba uongo uwe ukweli na ukweli uwe uongo , haki iwe dhuluma na dhuluma iwe haki . Una kazi tofauti na nilivyokufahamu tulipokuwa na kipindi chako cha kiti moto Kilimanjaro Hotel ukumbi wa Simba Grill . Nikuhurumie tu nitakuumbua vibaya sana .
 
Kwa jinsi ilivyo na inavyotakiwa tuamini ni CCM NA MACCM PEKEE WENYE UWEZO WA KUILETEA NCHI HII MAENDELEO!! WASIO CCM NI WASALITI NA SI WENZETU!!! Hizo kauli ni maarufu na zimeshatimia kwanini wasiotakiwa ama watu wa daraja duni washirikishwe katika mambo makubwa? Wenye akili wako kimya wanawatazama wenye maguvu. TULIPOSHAURI CCM IFUTE VYAMA VINGINE ILI IBAKI PEKEE TULIJUA HAWATAMUDU DEMOKRASIA NA MKONO WA CHUMA UTATUMIKA. JE WALIOTIWA VILEMA NA KUULIWA WAPENDWA WAO TUWAAMBIE TU HAYA MANENO YAKO YANATOSHA? JE INGELIKUWA NDUGU YAKO KAULIWA KATIKA KADHIA HIYO UNGELIANDIKA HIVI MKUU?
TWAPASWA KUUKEMEA UOVU KABLA YA KUPEANA FARAJA VINGINEVYO MIOYO IVUJAYO DAMU ITATUGHARIMU...
 
ACT kujiunga SUK Zanzibar ni fursa kwa chama chao kuwa sehemu ya dola na kukikomaza. It's up to them kama wanataka kukomaa au wanataka uanaharakati.

Fursa kama hii angeipata mtu kama Mbowe hata asingejiuliza mara mbili.
Yani ccm wapumbavu sana, mnamuona Maalim Seif hamnazo mumpe cheo cha kutembea na mkasi?

Hivi yule mama Samia Suluhu ana mamlaka hata ya kumfukuza kazi mtendaji tu wa mtaa?
 
Dikteta amefanikiwa kuwatega hawa wasomi uchwara
 
Si usubiri hata wafanye 40 ya wale waliouliwa kwenye UCHAGUZI.... PASKALI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…