kwenye siasa huwa hatuhitaji water tight evidence kuthibitisha jambo. balance of probability inatosha. Kwa taifa la hovyo kama Tz rushwa na ufisadi sio tuhuma kubwa kama unavyotaka kumaanisha. Vinginevyo kuna majitu mengi tu yangekuwa jela saivi.Tuhuma zozote nzito kama hizi ushahidi mwanana ni muhimu sana
Siasa chafu alizofanya Lisu na team yake dhidi ya team Mbowe yale majeraha kupona sio rahisi
Kuna vidonda vya kawaida na donda ndugu
Bon yai alichofanya ni sahihi ku block kabisa simu nk za wahuni
Tuwe fair Mbowe alichofanyiwa na Lisu sicho kabisaa
Salaam na heshima kwako mheshimiwa Boniface Jacobo Mayor mstaafu na Mwenyekiti wa Kanda ya pwani chama Cha demokrasia na maendeleo CHADEMA.
Kiongozi kabla ya kusema niliyowiwa kuyasema naomba kutambua unao washauri wengi sana wenye vyeo na nafasi kubwa kuliko Mimi ila naomba unipe dakika chache tu kusoma barua hii.
Kiongozi kabla ya uchaguzi mkuu wa chama ulikuwa mtu muhimu sana katika chama na nikiri huo umuhimu wako upo , pengo lako tunaliona ndio maana nimewiwa kuandika barua hii ya wazi kwako .
Kiongozi Kuna matukio mengi sana yametokea nchini ambayo sio kawaida tukose tweet mbili tatu kuyahusu na kuna matukio mengi sana ya kichama ambayo hatukuoni wala kuona mchango wako kwa sasa
Kiongozi naomba nikukumbushe tukio la wewe kurudisha fomu ya kugombea uenyekiti Kanda ya pwani. Wanachama wengi tulikusindikiza kurudisha fomu wengine hata hutufahamu na usisahau hatukukusindikiza kwa sababu ya ukaribu wako na Mbowe tambua hili Kuna wengi tu walipendezwa na Lissu wakati wa uchaguzi na walikuwa wengi tu huenda zaidi ya wafuasi wa mbowe waliokusindikiza . Hivyo tambua tunaokuamini hatukuamini kwasababu yoyote zaidi ya kuwa mwanachama wa chadema na mwenye uwezo mkubwa katika harakati za chama .
Tunatambua umeumia sana kutokana na demokrasia ilivyoamua ila fikiria vizuri sidhani kama mheshimiwa Mbowe anafurahia ukimya wako . Tafadhali ni muda wa kurudi sasa. Tusamehe tuliotoa maneno makali wakati wa uchaguzi wa chama nikiwemo umeniblock kabisa. Uchaguzi umekwisha . Ushapumzika vya kutosha . Pengo lako linakusubiri ulizibe Tafadhali lizibe tusonge mbele.
Nisikuchoshe kwa barua ndefu. Tafadhali rudi kama awali maisha yaendelee
Mwanachama mtiifu wa CHADEMA
Na mwanaharakati wa haki
Assenga
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mwamba alikuwa kiongozi,akiongea watu wanatafakari hata wiki,sasa hivi Kiongozi anaongea saa hiyohiyo watu wanasahauIla mwamba alikuwa na mvuto flan hivi pale CDM.....Yani chama kilikuwa oinaonekana kina standard flan hivi...
Ila Sasa hivi ni vurugu tuu
Kuna wakati unaongea point 💪Mkuu ni vigumu sana kufanya kazi na watu uliowatukana hadharani na kuwasingizia kula Rushwa ya Samia, kwa mfano Lissu amesema si mara moja kwamba Sugu alimshinda Msigwa kwa Rushwa, bila ushahidi wowote, ushahidi unaotolewa ni kwamba Mrema alihongwa bia 10 (bia moja ya kitanzania ni elfu 2 tu, hii maana yake ni kwamba Mrema alihongwa elfu 20), Je tuamini kwamba hii ndio rushwa ya uchaguzi? , hata kama ni kweli , hivi Mrema ni mpiga kura?
Sasa Sugu ni Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa na Msigwa ni Mwanaccm, Sasa unafanyaje kazi na Sugu kwa namna hii katika hali ya Ukweli wa kibinadamu? Unayemtetea Msigwa yuko ccm, tena alihama akiwa kakata rufaa na watu wakijiandaa kuijadili.
Tujifunze kuheshimu viongozi wengine kama sisi tunavyotaka kuheshimiwa, Hakuna Kiongozi anayeweza kuongoza Chama Peke yake kwa kutumia akili zake tu
Haya ni Mapungufu na ni lazima yarekebishwe ili kama chama twende pamoja
Siasa chafu alizofanya Lisu na team yake dhidi ya team Mbowe yale majeraha kupona sio rahisi
Kuna vidonda vya kawaida na donda ndugu
Bon yai alichofanya ni sahihi ku block kabisa simu nk za wahuni
Tuwe fair Mbowe alichofanyiwa na Lisu sicho kabisa
Kwa katiba ya Chadema, anakuwa mjumbe wa kudumu wa kamati kuu ya chama, yeye bado ni sehemu ya chama ni mwanachama. Labda yeye aamue kukimbia wajibu wake.Freeman Anaipenda sana Chadema, Atakuja kuwasaidia wakihitaji msaada wake, hajawahi kuwa na kinyongo
Sina chama cha siasa. Hata hivyo, nina uhuru wa kushauri pale ambapo naona inafaa. Kwa mwenendo huu, SSH kashashinda uchaguzi, CHADEMA ijikite kwenye uchaguzi wa madiwani na wabunge.Yaani nyie maccm mnataka kuifundisha chadema jinsi ya kuendesha chama?
Kama ni kuwafundisha ufisadi sawa, kwa sababu hiyo ndiyo fani mliyobobea.