Ni swala ambalo ni gumu kdg kulizungumzia hum kiundani zaidi lakn kikubwa kilio chetu tunahitaji kimfkie mheshimiwa Rais Ntashkuru kma utakua na msaada na hlo hata kuweza kushare.
Umeumizwa halafu unakingia kifua kufichua uozo uliosababisha mchujo wa kinafiki na upendeleo wa kushenzi?
Nani asiyejua kujiunga na jeshi kunatumika rushwa na kujuana?
Nikuhakikishie, hao wote mkifanyiwa re examination, robo3 ni wazima, ila nafasi zenu zimewekwa kibindoni ajili ya kuzawadia watoto wa wakubwa wadio na sifa, watakaochomekwa kinyemela ama nafasi hizo kuuzwa.
Sasa wewe endelea kufichaficha, mahali ambapo unatakiwa kumwaga mtama ili msaidiwe, maana haukusaidiwa na mamlaka hiyo.
Mara nyingi kumekuwa na upinzani wa kimyakimya rais atoapo maelekezo ya ajira kwa amri.
Wanayapokea maagizo yake kwa shingo upande huku wakiwaza namna ya kufanikisha waliyoyazoea, maana anakuwa kaziba mirija yao ya ulaji.
Mwaka jana tuliona tena tangazo la Mkuu wa majeshi akiagiza vijana waliojenga ukuta wa Mererani wakapewa zawadi ya ajira kisha kurudishwa majumbani, waripoti kwenye chuo cha mafunzo!
Ni nini maana ya mkanganyiko huu sasa, ni nani huyo aliyepingana na amri halali ya CinC kuwarejesha majumbani badala ya kuwapeleka chuo cha mafunzo!
Ajira hiyo ilitangazwa kama zawadi kwenu ni haki yenu vijana mliojitolea kwa nidhamu na jasho kufanikisha miradi iliyopewa jeshi kutekeleza na kupelekea jeshi hilohilo kupewa sifa na kuaminika.
Je walipowapima walipeleka ripoti kwa rais juu ya u unfit wenu na hatua gani zichukuliwe za kuwasaidia?
Maana hiyo ni ajira maalumu ya tamko la rais, hawezi kutokea tu kiongozi hapo katikati akapindisha tamko la rais bila kupeleka taarifa Ikulu.
Sasa wanatumia mbinu za kuwapa alama za unfit kutimiza malengo yao hayo niliyoeleza.
Lalamiko lenu likisongeshwa likamfikia Jpm na likafanyiwa kazi, kisha mkarudiwa kupimwa kwa kutumia majopo mengine ya madaktari, litaumbua myororo mzima wa kifisadi, kisha waliofanya huo unyama washitakiwe na kuwajibishwa bila kujali cheo cha mtu, maana nyie wote hao hamuwezi kuwa ma unfit inapopatikana ajira, lakini kwenye kujitolea mlikuwa physically fit.
Pole sana kijana.
Sent using
Jamii Forums mobile app