Barua ya wazi kwa Sheikh Mziwanda na Dr. Sule: Acheni kutetea dhulma dhidi ya Watanzania wenzenu

Barua ya wazi kwa Sheikh Mziwanda na Dr. Sule: Acheni kutetea dhulma dhidi ya Watanzania wenzenu

Quran inatutaka kabla ya kuzungumza jambo kwanza tulifanyie utafiti wa kutosha
Au masheikh kama kweli wamefanya hayo wanatakiwa watubu. Sio muongozo wa dini.



Katika Qur'an, kuna aya kadhaa zinazosisitiza umuhimu wa kufanya uchunguzi wa jambo kabla ya kutoa uamuzi au kuamini kitu.

Moja ya aya maarufu ni kutoka Surah Al-Hujurat (49:6), ambapo Allah anasema:"Enyi mlioamini! Mkiletewa habari na fasiki yoyote, ichunguzeni kwa makini, msije mkawadhuru watu kwa ujahili, na mkawa wenye kujuta kwa mliyoyatenda."
(Qur'an 49:6)

Aya hii inatoa mwongozo wa kidini kwa waumini kuhusu umuhimu wa kufanya uchunguzi wa habari au jambo lolote kabla ya kuchukua hatua, ili kuepuka kufanya maamuzi mabaya au kuumiza wengine bila sababu. Hii inahimiza kuwa na tahadhari na kufanya utafiti wa kina kabla ya kuchukua hatua yoyote.

AO MASHEIKH WAMEFANYA UTAFITI ?
Hao Masheikh ni wahuni tu wanaotegemea kuvuna kitu toka meza kuu. Huyo Sule ndiyo mhuni kabisa anayetangaza biashara ya pete zake za majini.
 
Sijui kwanini ukiwa upande ule lazima na uzezeta japo hata kidogo tu
Nami nashangaa.🙌🙌🙌

✍️Mit 31:6
Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.

✍️Hab 2:15
Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili kuutazama uchi wao. Pdidy
 
Masheikh 80% wanà uelewa mdogo wa mambo yasiyokuwa ya dini....hawa wapo vyema kukariri tu Quran ila huku kwingine ni weupe mno
Hili Taifa litaendelea kutaabika kwa kuwa na watu kama hawa. Mungu awalaani wale wote washabikiao mauaji ya Roho za wengine. Uchawa wa aina yake . Ukweli usemwe bila ya kujali kuwa aliyetenda anatoka upande gani
 
kukariri Quran ndio inakuwaje ni zaidi ya kila kitu ikiwa mambo ya kawaida tu masheikh wanatia aibu? Tangu lini mtu anaekariri akawa na akili?
Tuwapuuze hawanaga msimamo katika mambo ya Kitaifa, wanajali zaidi maslahi yao binafsi na hawawakilishi maoni na misimamo ya wafuasi wao
 
Ukweli ni kwamba katika Uislam kuna taratibu zilizowekwa katika kuamiliana na watawala. Haifai kuminyamana na watawala. Tumeamrishwa kuwatii watawala katika yasiyo ya haramu na kuwa na subra katika dhulma ya mtawala.

Na haifai kumkosoa mtawala hadharani, anayetaka kumnasihi mtawala amshike mkono au amuandikie kwa siri amnasihi. Umekutana na mtawala uso kwa macho hapo sasa ndio umepata fursa ya kumnasihi, basi mnasihi kwa busara iwapo kama ni kweli unataka kutoa nasaha. Au muandikie. Haifai kumtukana.

Lakini haifai kuwapinga na kuwakosoa hadharani. Sikuambii kuwafanyia uasi ndio kabisa.

Na kuhusu maandamano sijui mapinduzi hayafai. Sisi tumefundishwa kuwa na subra kunako dhulma ya mtawala. Hawawi madhalimu watawala ila kwa sababu ya dhulma za raia.

Dhulma ikidhihiri miongoni mwa watu; kukajaa washirikina wanaoabudu wengine pamoja na Allah au wakawaabudu wengine badala ya Allah, au kukajaa wazinifu, wezi, wadokozi, matapeli, waonevu na wenye kupokonya haki za watu na kadhalika basi Allah atawaoneshea athari ya maovu yao kupitia watawala wao. Watayaona hayo kwa watawala wao. Hivyo wakitaka kuondolewa watawala madhalimu, basi waache wao kwanza dhulma.

Ila migomo, maandamano, uasi na mapinduzi unazidisha shari na uharibifu na kuondoa amani.


Nimeandika haya sio kwa sababu hao "dokta" Sule na Sheikh Mziwanda ni masheikh zangu. Hapana. Allah awaongoze.

Allah atuongoze katika njia iliyonyooka. Allah atengeneze mioyo ya watawala wetu, awaongoze katika njia iliyonyooka, awafanyie wepesi na awape hikma na uadilifu. Allah aidumishe amani tuliyonayo, Yaa Hayyu Yaa Qayyum. Ameen.
Unakumbuka harakati za Sheikh Ponda na Ilunga (Rip)?....Kumbe walikuwa wanakosea kuminyana na utawala wa Ccm ?
 
Usiwe kama kiazi na mjinga wa kupotezea historia, wale wa tuhuma za ugaidi wa Arusha na kwingineko si ilikuwa enzi ya Mzee wa Msoga yule ni dini gani???


Sasa usipayuke tu kisa unaona sa hivi ni sahihi kisayupo mwenzenu na aliepita hakuwa mwenzenu


Serikali ina taratibu zake na inapozifuata tegemea maumivu kwa upande wowote as long as amani itaendelea kutawala na nchi inakaa kwenye msingi sahihi
Mnadharau masheikh kwa kejeli kisha mnataka Waislam wawaunge mkono?

Nani haujui mlengo wa CHADEMA kwenye swala la dini?

Hoja ya Mziwanda ni kuwa mnakuwa hamna consistency kwenye kulaani matukio!!

Wakati masheikh wanakamatwa na kuswekwa ndani kwa dhulma hamkuinuka kisa kiongozi mkuu alikuwa dini yenu
 
Kishki, Mziwanda, "dokta" Sule wote hawajasimama sawa. Huyo Ponda naye hajasimama sawa na ni mwanaharakati tu. Allah atuongoze sisi na wao.

Masheikh waliosimama sawa ni wale walio katika njia ya Salaf
Wepi hao? Salaf ni wema waliotangulia
 
Mnadharau masheikh kwa kejeli kisha mnataka Waislam wawaunge mkono?

Nani haujui mlengo wa CHADEMA kwenye swala la dini?

Hoja ya Mziwanda ni kuwa mnakuwa hamna consistency kwenye kulaani matukio!!

Wakati masheikh wanakamatwa na kuswekwa ndani kwa dhulma hamkuinuka kisa kiongozi mkuu alikuwa dini yenu!
Chadema imeingiaje hapo? Mtoa mada kaandika chama? Au unataka kutuaminisha kuwa kuwa ccm ni cha kiislamu na Chadema ni cha kikristo? Tumeshatoka huko miaka mingi sana aisee! Bado ww tu.
 
Mnadharau masheikh kwa kejeli kisha mnataka Waislam wawaunge mkono?

Nani haujui mlengo wa CHADEMA kwenye swala la dini?

Hoja ya Mziwanda ni kuwa mnakuwa hamna consistency kwenye kulaani matukio!!

Wakati masheikh wanakamatwa na kuswekwa ndani kwa dhulma hamkuinuka kisa kiongozi mkuu alikuwa dini yenu!
Masheikh waliswekwa ndani na mzee wa Msoga, je ni Mkristo? Ni Chadema haohao waliopiga kelele na si CCM. Wakati wa awamu ya JPM ni Chadema haohao waliopiga kelele na kupitia hekaheka nyingi kama kupigwa risasi makamu mwenyekiti, kukamatwa kwa viongozi wao na wemgine kupotezwa kabisa! Iweje awamu hii iwe kosa kwao kukosoa utawala na kudai haki zao!? Huo udini mbona wewe na Masheikh njaa wako ndo mnauleta?
 
Unaweza kuwatofautisha kutokana na hizo kauli zao uislamu unapinga dhulma bila ya kujali hiyo dhulma imefanywa na nani muislamu wa kweli hawezi kuunga mkono dhulma
Kwahiyo kwa kauli za Sulle,mwaipopo na mziwanda nikwamba sio uislamu?
 
Bakwata iwe inawatimua kabisa hao mashehena, wao sio chombo maalumu cha matamko, matamko yote ya kitaifa yawe yanatolewa na Bakwata, kuwaachia mashehena hao ni kuuchafua uongozi wa Bakwata mchana kweupe
Sasa hao si ndio BAKWATA wenyewe?



Halafu BAKWATA = CCM
 
kukariri Quran ndio inakuwaje ni zaidi ya kila kitu ikiwa mambo ya kawaida tu masheikh wanatia aibu? Tangu lini mtu anaekariri akawa na
Acha upumbavu wako wa udini.


Masheikh wanazingua sana ila sababu ni tamaa zao tu


Hao masheikh wa BAKWATA ni CCM
 
Back
Top Bottom