Barua ya wazi kwa Waziri wa Mazingira na NEMC- Kelele mitihani ni tishio la afya za wananchi na Ustawi wa Taifa

Barua ya wazi kwa Waziri wa Mazingira na NEMC- Kelele mitihani ni tishio la afya za wananchi na Ustawi wa Taifa

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Ndugu mheshimiwa Waziri naandika haya kukujuza kuwa. Kwa sasa nchini kiwango cha kelele mitaani kinatisha, ni jukumu la serikali kuchukua hatua ili kulinda Afya za wananchi na ustawi wa Taifa.

Ndugu Waziri, leo hii kwenye vituo vya mabasi, masokoni, mitaani, kelele zimekuwa ni nyingi na tena kubwa kupita kiasi.

Ndugu Waziri, nafahamu ofisini kwako ziko taarifa mbalimbali za Tafiti ya hali ya kelele nchini, zilizofanywa na taasisi mbalimbali za Elimu na utafiti nchini. Na miongoni mwa Tafiti zetu ni ile iliyofanywa na chuo kikuu cha Muhimbili kwa kushirikiana na UDOM mwaka 2019 ikionyesha kuwa zaidi ya asilimia 58 ya wafanyakazi wa viwanda vya nguo nchini WAMEPOTEZA USIKIVU.

Pia Tafiti zikaendelea kusema kuwa maeneo ya Mgahawa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na SUA umevuka hadi kufikia 73dBA ambayo imezidi kiwango cha 55dBA ambayo ndiyo inayotakiwa.

Na tafiti nyingine ikasema kuwa maeneo yanayozunguuka mashine za kusaga kiwango cha kelele kinafika hadi 103dBA ambacho ni kiwango kikubwa sana cha kelele ambacho kinaathiri pakubwa mno uwezo wa kusikia.

Kutumia mtindo wa kupiga mziki mkubwa utadhani Disco siku hizi limegeuka ndiyo mtindo wa matangazo ya biashara.

Ndugu waziri, siku hizi kila anayetaka kutangaza biashara zake basi anatafuta spika kubwa na muziki mkubwa anauweka masokoni, anapita na maspika barabarani au anasimika maspika makubwa mahali na kufungulia muziki mkubwa non stop utadhani yuko ndani ya Disco. Hali hii siyo tu kwamba inaumiza masikio bali inakosesha utulivu kabisa. watoto wanaathirika, wagonjwa wanaathirika na hata raia wa kawaida nao wanaathirika.

ATHARI ZA HIZI KELELE.

Wataalamu wanasema kuwa Sauti inayofikia 75dB inaathiri uwezo wa kufikiri na kufanya kazi. Hii inamaanisha kuwa kwa kushindwa kudhibiti hizi kelele tunatengeneza Taifa la watu wenye uchovu wa kufikiri na hata tija ya utendaji wao wa kazi unashuka. Hii inashusha uwezo wa kuzalisha na hivyo kupelekea cycle ya umasikini kuendelea.

Wataalamu wanasema kuwa kiwango cha kelele kikishafika 90dB hii inaweza kupelekea watu kupoteza uwezo wa kusikia vizuri.

Uchunguzi wangu kuhusu kiwango cha sauti mitaa ya Dar

Kwa kutumia kifaa cha kupima sauti, nimepita katika maeneo ya mkusanyiko wa watu wengi katika soko la Bunju, na Kituo cha mabasi ya Makumbusho. Hapa kiwango cha sauti kinafika kati ya 85dB mpaka 87dB. Maeneo haya yamesheheni spika kibao, Makumbusho kuna Spika ya kutangaza biashara ya kampuni ya Simu ya Yas, Wanapiga DISCO mtindo mmoja, ni makelele ya kufa mtu.

Ndugu waziri hatuwezi kuwa Taifa la makelele. Hakuna mind iliyoproductive inayoweza kuwa bunifu, yenye fikra tunduizi, inayoweza kufanya kazi sawasawa katika mitaa iliyojaa makelele.

Najua Ipo sheria ya kudhibiti Kelele ya NEMC ya mwaka 2004 lakini sheria hiyo haisimamiwi. Serikali za mitaa hazifanyi kazi ipasavyo, na manispaa zinazotoa vibali vya matangazo hazifanyi kazi sawasawa kwenye hii ishu.

Ndugu Waziri na mhusika wa NEMC fanyieni kazi hili.

Nawasilisha!
 
Hiyo hali ilishaanza kudhibitiwa hapa Dar es Salaam lakini akatokea mlevi mmoja akawa anapingana na wenzake kwa sababu ya ulevi wake akidai haiwezekani mtu akanywa bia bila kelele na kudai kwamba kama kuna mtu hataki kelele ahame Dar!
Huyu mtu tunashangaa wenye mamlaka ya uteuzi wamempa vipi madaraka ambayo yamemzidi kimo kutokana na athari ya ulevi uliyopitiliza kiasi cha siku za hivi karibuni amekuwa maarufu kwa kutukana na kukashifu wananchi.
 
Mods rekebisheni kichwa cha habari.
Pamoja na hivyo viongozi wa ovyo wa ccm ndo wametifukisha huku!
Yaani makelele yamekuwa sehemu ya maisha ya Bongo!
 
Hiyo hali ilishaanza kudhibitiwa hapa Dar es Salaam lakini akatokea mlevi mmoja akawa anapingana na wenzake kwa sababu yabulevi wake akadai haiwezekani mtu ukanywa bia bila kelele na kudai kwamba kama kuna mtu hataki kelele ahame Dar!
Huyu mtu tunashangaa wenye mamlaka ya uteuzi wamempa vipi madaraka ambayo yamemzidi kimo kutokana na athari ya ulevi kiasi cha siku za hivi karibuni amekuwa maarufu kwa kutukana na kukashifu watu.
Chalamila ni mtu wa ovyo sana!
 
Hiyo hali ilishaanza kudhibitiwa hapa Dar es Salaam lakini akatokea mlevi mmoja akawa anapingana na wenzake kwa sababu ya ulevi wake akidai haiwezekani mtu akanywa bia bila kelele na kudai kwamba kama kuna mtu hataki kelele ahame Dar!
Huyu mtu tunashangaa wenye mamlaka ya uteuzi wamempa vipi madaraka ambayo yamemzidi kimo kutokana na athari ya ulevi uliyopitiliza kiasi cha siku za hivi karibuni amekuwa maarufu kwa kutukana na kukashifu wananchi.

Kumbe huyo jamaa ndo ametufanya tuishi hivi. Hii ni disaster.
 
Ndugu mheshimiwa Waziri naandika haya kukujuza kuwa. Kwa sasa nchini kiwango cha kelele mitaani kinatisha, ni jukumu la serikali kuchukua hatua ili kulinda Afya za wananchi na ustawi wa Taifa.

Ndugu Waziri, leo hii kwenye vituo vya mabasi, masokoni, mitaani, kelele zimekuwa ni nyingi na tena kubwa kupita kiasi.

Ndugu Waziri, nafahamu ofisini kwako ziko taarifa mbalimbali za Tafiti ya hali ya kelele nchini, zilizofanywa na taasisi mbalimbali za Elimu na utafiti nchini. Na miongoni mwa Tafiti zetu ni ile iliyofanywa na chuo kikuu cha Muhimbili kwa kushirikiana na UDOM mwaka 2019 ikionyesha kuwa zaidi ya asilimia 58 ya wafanyakazi wa viwanda vya nguo nchini WAMEPOTEZA USIKIVU.

Pia Tafiti zikaendelea kusema kuwa maeneo ya Mgahawa kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na SUA umevuka hadi kufikia 73dBA ambayo imezidi kiwango cha 55dBA ambayo ndiyo inayotakiwa.

Na tafiti nyingine ikasema kuwa maeneo yanayozunguuka mashine za kusaga kiwango cha kelele kinafika hadi 103dBA ambacho ni kiwango kikubwa sana cha kelele ambacho kinaathiri pakubwa mno uwezo wa kusikia.

DISCO SIKU HIZI LIMEGEUKA NDIYO MTINDO WA MATANGAZO.

Ndugu waziri, siku hizi kila ansyetaka kutangaza biashara zake basi anatafuta spika kubwa na muziki mkubwa anauweka masokoni, anapita na maspika barabarani na kufungulia muziki mkubwa non stop utadhani yuko ndani ya Disco. Hali hii siyo tu kwamba inaumiza masikio bali inakosesha utulivu kabisa. watoto wanaathirika, wagonjwa wanaathirika na hata raia wa kawaida nao wanaathirika.

ATHARI ZA HIZI KELELE.

Wataalamu wanasema kuwa Sauti inayofikia 75dB inaathiri uwezo wa kufikiri na kufanya kazi. Hii inamaanisha kuwa kwa kushindwa kudhibiti hizi kelele tunatengeneza Taifa la watu wenye uchovu wa kufikiri na hata tija ya utendaji wao wa kazi unashuka. Hii inashusha uwezo wa kuzalisha na hivyo kupelekea cycle ya umasikini kuendelea.

Wataalamu wanasema kuwa kiwango cha kelele kikishafika 90dB hii inaweza kupelekea watu kupoteza uwezo wa kusikia vizuri.

UCHUNGUZI WANGU KUHUSU KIWANGO CHA SAUTI MITAANI DSM

Kwa kutumia kifaa cha kupima sauti, nimepita katika maeneo ya mkusanyiko wa watu wengi katika soko la Bunju, na Kituo cha mabasi ya Makumbusho. Hapa kiwango cha sauti kinafika kati ya 85dB mpaka 87dB. Maeneo haya yamesheheni spika kibao, Makumbusho kuna Spika ya kutangaza biashara ya kampuni ya Simu ya Yas, Wanapiga DISCO mtindo mmoja, ni makelele ya kufa mtu.

Ndugu waziri hatuwezi kuwa Taifa la makelele. Hakuna mind iliyoproductive inayoweza kuwa bunifu, yenye fikra tunduizi, inayoweza kufanya kazi sawasawa katika mitaa iliyojaa makelele.

Najua Ipo sheria ya kudhibiti Kelele ya NEMC ya mwaka 2004 lakini sheria hiyo haisimamiwi. Serikali za mitaa hazifanyi kazi ipasavyo, na manispaa zinazotoa vibali vya matangazo hazifanyi kazi sawasawa kwenye hii ishu.

Ndugu Waziri na mhusika wa NEMC fanyieni kazi hili.

Nawasilisha!
Barua yako ina mashiko tatizo linakuja kwetu sisi wenyewe, mwanzo kulianzishwa msako wa makelele kwenye mabaa na kumbi za starehe wananchi wakaanza kelele maradioni watu kama walikua wanaandamana hivi na Jamaa wakaona isiwe tabu wakatuachia kelele zetu, so atupaswi kulalamika tena.
 
Kumbe huyo jamaa ndo ametufanya tuishi hivi. Hii ni disaster.
Alitakiwa awe mkuu wa wilaya moja wapo kule kwao Iringa au Njombe kwa kule ndiyo mabingwa wa kulewa tokea alfajiri hata watoto wao badalavya kuwapa chakula wao wanawatandika pombe tu ndiyo maana kuna utapiamlo sana japo wana chakula cha kutosha.
 
Alitakiwa awe mkuu wa wilaya moja wapo kule kwao Iringa au Njombe kwa kule ndiyo mabingwa wa kulewa tokea alfajiri hata watoto wao badalavya kuwapa chakula wao wanawatandika pombe tu ndiyo maana kuna utapiamlo sana japo wana chakula cha kutosha.

Yeye analeta comedy kwenye mambo serious, tunaoumia ni sisi wananchi.
 
Maskini wanapenda sana kelele. Kuna bodaboda zinazofungwa mziki zinakatisha mitaani sauti ikiwa juu sana. Unajuliza kama dereva huyo ana akili timamu au ni mwehu. Na unakuta ni usiku. Hafikiri labda kuna watoto wadogo wamelala au hata mgonjwa.

Kelele ni nyingi sana kuanzia spika za matangazo, honi za magari na pikipiki, pikipiki zilizofanyiwa modification kwenye bomba la moshi, wauza movie na kuweka nyimbo kwenye flash kwenye vibanda mitaani. Uko kwenye eneo moja lenye vyanzo zaidi ya 10 vya kelele. Si salama kwa afya ya akili. Hadi unajiuliza kama kuna serikali kweli au wahusika hawajali tu afya za watu.
 
Maskini wanapenda sana kelele. Kuna bodaboda zinazofungwa mziki zinakatisha mitaani sauti ikiwa juu sana. Unajuliza kama dereva huyo ana akili timamu au ni mwehu. Na unakuta ni usiku. Hafikiri labda kuna watoto wadogo wamelala au hata mgonjwa.

Kelele ni nyingi sana kuanzia spika za matangazo, honi za magari na pikipiki, pikipiki zilizofanyiwa modification kwenye bomba la moshi, wauza movie na kuweka nyimbo kwenye flash kwenye vibanda mitaani. Uko kwenye eneo moja lenye vyanzo zaidi ya 10 vya kelele. Si salama kwa afya ya akili. Hadi unajiuliza kama kuna serikali kweli au wahusika hawajali tu afya za watu.

Yaani utadhani nchi hii haina serikali kabisa. Huwezi kuuona Ujinga huu kwenye nchi za watu wanaojielewa.
 
Sio afya ya wananchi tu bali sema afya ya akili ya wananchi inaathiriwa vibaya
 
Hiyo hali ilishaanza kudhibitiwa hapa Dar es Salaam lakini akatokea mlevi mmoja akawa anapingana na wenzake kwa sababu ya ulevi wake akidai haiwezekani mtu akanywa bia bila kelele na kudai kwamba kama kuna mtu hataki kelele ahame Dar!
Huyu mtu tunashangaa wenye mamlaka ya uteuzi wamempa vipi madaraka ambayo yamemzidi kimo kutokana na athari ya ulevi uliyopitiliza kiasi cha siku za hivi karibuni amekuwa maarufu kwa kutukana na kukashifu wananchi.
Kuna mwaka flani akikatazwa kutoa hotuba akiwa amesha lewa, na hii ndio ilimgharimu kipindikile hadi wakamuweka kando
 
Nakazia na kukazia, hapo karume ukipita na boda au kwa mguu unaweza kuzimia kwa kelele, na ukifanikiwa kupita salama basi siku nzima itakuwa mbovu kwa maumivu ya masikio

Wizara fanyieni jazi hili kwa amri haraka sana
 
Back
Top Bottom