Bashe alitupia lawama Bunge kuharibu Kilimo

Bashe alitupia lawama Bunge kuharibu Kilimo

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Waziri Bashe jioni hii akichangia bungeni ameutupia lawama Mhimili wa Bunge kuwa ndio umesababisha kuharibu kilimo na kusisitiza kuwa kamwe Serikali ya Rais Samia haiwezi kufanya kosa hilo.

Pamoja na lawama hizo nzito kwa watunga sheria..Kiti hakijaweza kutoa mwongozo wowote kuhusiana na jambo hili la Waziri kulidharau Bunge, wakati Rais mwenyewe wa nchi Dk. Samia Suluhu Hassan hajawahi kulidharau Bunge wala wabunge kwa kuwa anatambua ni moja ya mihimili ya nchi iliyoko kwa mujibu wa Katiba.

Swali la muhimu. Bashe anapata wapi kiburi cha kulidharau bunge kwa kiwango hicho ilihali Rais Samia mwenyewe anayemwakilisha kwenye wizara ya kilimo hajawahi kutoa kashfa kwa Bunge, ametumia bunge kuwatetea wafanyabishara na kusisitiza kuwa kamwe serikali haiwezi kuwapangia bei ya kuuza mazao yao.

Je Wabunge nao wakiamua kueleza ukweli juu ya makampuni yanayohusika na kuuza mazao ndani na nje ya nchi na mahusiano yao na Bashe yuko tayari kuwajibika?
 
Bashe kuwa na hayo mahusiano sio kosa, kosa lingekuwa kama anawapendelea hao washirika wake na kuacha wengine wateseke, ila kama karuhusu kwa wote basi hio haina shida kabisa
 
Waziri kulidharau Bunge, wakati Rais mwenyewe wa nchi Dk. Samia Suluhu Hassan hajawahi kulidharau Bunge
Rais Samia hajawahi kufanya kosa hilo hata siku moja kudharau Bunge? hiyo kazi wanaiweza Mwigulu, Makamba na Bashe tu
 
Bila shaka na yeye Bashe alikuwa mbunge wakati uharibifu unafanyika

20230113_165617.jpg
 
Wewe ni moja kati ya watu wa hovyo katika nchi hii.

Kilimo kikistawi, utajiri utarudi vijijini, kuwapangia bei, kunakatisha tamaa vijana kuingia katika kilimo na kukimbilia bodaboda.

Nchi hii ajira hakuna, lakini kazi zipo, mwakani kama bei nzuri Kila mtu atarudi shambani, akauze Kenya, Burundi, Rwanda,uganda
 
Waziri Bashe jioni hii akichangia bungeni ameutupia lawama Mhimili wa Bunge kuwa ndio umesababisha kuharibu kilimo na kusisitiza kuwa kamwe Serikali ya Rais Samia haiwezi kufanya kosa hilo.

Pamoja na lawama hizo nzito kwa watunga sheria..Kiti hakijaweza kutoa mwongozo wowote kuhusiana na jambo hili la Waziri kulidharau Bunge, wakati Rais mwenyewe wa nchi Dk. Samia Suluhu Hassan hajawahi kulidharau Bunge wala wabunge kwa kuwa anatambua ni moja ya mihimili ya nchi iliyoko kwa mujibu wa Katiba.

Swali la muhimu. Bashe anapata wapi kiburi cha kulidharau bunge kwa kiwango hicho ilihali Rais Samia mwenyewe anayemwakilisha kwenye wizara ya kilimo hajawahi kutoa kashfa kwa Bunge, ametumia bunge kuwatetea wafanyabishara na kusisitiza kuwa kamwe serikali haiwezi kuwapangia bei ya kuuza mazao yao.

Je Wabunge nao wakiamua kueleza ukweli juu ya makampuni yanayohusika na kuuza mazao ndani na nje ya nchi na mahusiano yao na Bashe yuko tayari kuwajibika?

Hao wabunge nao waeleze ukweli maana Bashe kawaambia ukweli. Isitoshe nani analiogopa hilo bunge la majizi ya kura?
 
mwaka jana miezi kama hii kipindi cha mavuno mkulima aliuza mchele 1300 kwa kg leo hii tunaongelea bei zaidi ya mara mbili, sasa ebu niambie anayeuza bei ya 3500 ni mkulima au mfanya biashara
Mimi unayebishana nae ni mkulima wa mpunga,haiwezekani Bei ya mwisho iwe 3500 halafu mkulima akuuzie buku jero,wakulima hatuishi shomoni tuna taarifa zote za soko,huwa tukiwaachia Sana wachuuzi faida basi ni miambili kwa kilo
 
Back
Top Bottom