Tajiri mpole
JF-Expert Member
- Apr 15, 2018
- 2,890
- 5,632
Nikikuambia kuwa ccm wanatumia mabavu ya vyombo vya dola kuongoza kwa shuruti, sina chembe ya shaka na maelezo yangu. Kutekeleza mipango ya maendeleo ya vitu au watu, ni wajibu wa serikali yoyote, hata wakoloni walifanya hilo. Kwamba vyombo vya dola vimetumika kukandamiza upinzani, hilo halihitaji hata kuishi hapa nchini kujua hayo.
Bashiru acha kuwapangia watu. Mwacheni Bashite atimize ndoto zake. Na mkimkata atakwenda kwa baba yake mzee Membe. Kigamboni pale lazima ashinde uchaguzi mkuu.
Kwani ni lazima afanye kazi mliyoamua nyinyi. Wapeni haki ya kuchagua. Hoja mnazotoa ni manyanyaso kwao.Nikikuambia kuwa ccm wanatumia mabavu ya vyombo vya dola kuongoza kwa shuruti, sina chembe ya shaka na maelezo yangu. Kutekeleza mipango ya maendeleo ya vitu au watu, ni wajibu wa serikali yoyote, hata wakoloni walifanya hilo. Kwamba vyombo vya dola vimetumika kukandamiza upinzani, hilo halihitaji hata kuishi hapa nchini kujua hayo.
Kama mnaamini ni wajibu wa Serikali kutekeleza mipango ya maendeleo na ikatimiza wajibu huo, kuna hoja gani tena ya msingi?
Kwa nchi zinazoendelea kumekuwa na mapungufu makubwa ya kiuongozi, hasa kuhusu matumizi ya kodi na usimamizi wa rasimali za Taifa. Uongozi wa Magufuli umethibitisha kuwa ni imara katika matumizi na usimamiaji, na ndiyo maana sina shaka kuwa Serikali ya CCM itarudishwa madarakani.
Kwamba hata wakoloni walifanya hivyo, ni hoja ya kipuuzi, kwani ukoloni ulifanya hivyo kurahihisha utawala wao tofauti na ilivyo sasa. Mahitaji na mipango ya maendeleo hutoka kwa wananchi kupitia wawakilishi wao toka ngazi za chini. Wananchi waliochagua wawakilishi makini na waadilifu, hakuna shaka maeneo yao yana maendeleo yanayoonekana.
Nisingependa kutoa mifano jinsi vyama vya upinzani vinavyotumia ruzuku (kodi ya wapiga kura) kunufaisha wanasiasa viongozi wa vyama hivyo huku wakitegemea kesho wapewa dhamana ya kuongoza nchi.
Au mnadhani wapiga kura ni wajinga kiasi cha kutokutambua mbivu na mbichi? Labda mnaamini Tume Huru ya Uchaguzi ndiyo agenda ya kuaminisha wapiga kura?
We
Serikali inaweza kuongozwa na chama chochote.
Unaandika maneno mengi, lakini mtu akifuatilia vizuri unachoongea ataona fika ulivyo na uelewa finyu wa mambo. Sasa kama hujui tofauti ya chama na serikali, huoni lazima utajikuta unaongea maneno mengi yasiyo na maana yoyote?
.
Kama ni kujichanganya ni wewe. Nimeacha aya hizo mbili ulizoandika wewe.
Kwa Katiba ya JMT, hakuna mgombea binafsi hivyo mgombea wa Urais ndiye uunda Serikali. Na mgombea Urais huteuliwa na chama na kunadi Sera za chama kama zilivyoanishwa kwenye Ilani.
Awali nilisema Serikali imetekeleza yaliyomo kwenye Ilani kwa sababu ya usimamizi makini wa Chama. Hivyo chama, kwa maana ya wagombea, watapanda kwenye majukwaa ya kampeni wakiwa wamebeba mafanikio yaliyotokana na utekelezaji wa Ilani yake na Serikali.
Je, upinzani unalo lipi la kunadi iwapo katika kipindi chote ni kuibeza Serikali pasipokuwa na Sera mbadala! Upinzani ukipanda majukwaani kudai Tume Huru au demokrasia, wataeleweka?
😃😃😃😃 daah we jamaa umenchekesh kwel nape wa 2010-2015 cio huyu wa sasa kabsa kawa mnyonge hata kuongea hawezi daah magu co mtu mzur kwa kwelDuniaaa, haina huruma eeeh! ×2
Nimejikuta namuimbia Nape kawimbo.
Anapitia kipindi kigumu sana awamu hii. Mara anyooshewe mguu wa kuku hadharani, hatujakaa sawa anapiga magoti kuomba radhi, na Sasa anajificha hata kuchukua fomu.
Nape, ooooh Nape!
Wew humwogopi? Hizo siri zote alizonazo kuhusu zile maiti zilizokuwa zinaelea baharini ni kitu kidogo? Kujua Ben Saanane alienda wapi ni kitu kidogo?. Ni Pompeo tu ndo hamwogopi Bashite maana aliweka wazi kuwa "ananyima watu haki ya kuishi"Hahahaha aibu kubwa sana hii. Wanamuogopa Makonda utadhani ukoma dadeeeki
Kwakweli Magu amefifisha nyota na kuzima ndoto za Nape😃😃😃😃 daah we jamaa umenchekesh kwel nape wa 2010-2015 cio huyu wa sasa kabsa kawa mnyonge hata kuongea hawezi daah magu co mtu mzur kwa kwel
Dah Usiku mwemaWew humwogopi? Hizo siri zote alizonazo kuhusu zile maiti zilizokuwa zinaelea baharini ni kitu kidogo? Kujua Ben Saanane alienda wapi ni kitu kidogo?. Ni Pompeo tu ndo hamwogopi Bashite maana aliweka wazi kuwa "ananyima watu haki ya kuishi"
Kuhusu kutenda haki kwa wagombea wote, Dkt. Bashiru amesema:
”Nadhani kama umemsikiliza Mwenyekiti wetu jana wakati anaapisha baadhi ya viongozi, alisema yeye kama mwenyekiti wa chama hana mgombea, na akaenda mbali kusema Makamu wa Rais, hana mgomnea; akamtaja Waziri Mkuu, hana mgombea; akamtaja Makamu Mwenyekiti, Mzee Mangula, hana mgombea; akanitaja mimi, sina mgombea.”
“Matarajio yetu, viongozi wanaokaa kwenye vikao vya uteuzi wana dhamana kubwa ya kutenda haki kwa wagombea wote. Hata kama ni mkeo, hata kama ni mwanao, hata kama ni rafiki yako mulisoma wote, hata kanma ni tajiri yako kakuajiri – unalinda maslahi ya chama siyo maslahi ya mgombea. Na kwahiyo upo upande wa chama, si upande wa wagombea”
Kuhusu wanaoachia nafasi zao na kuusaka ubunge, Dkt. Bashiru amesema:
"Na ndiyo maana hairuhusiwi mtu anayegombea kushiriki katika vikao. Naomba nitaje jambo ningependa mtusaidie. Kuna baadhi ya wenyeviti wetu wa mikoa; sasa hivi wamefikia watatu -- mikoa mitatu. Wanaopaswa kukaa kwenye vikao vya kamati za siasa za mkoa (ndiyo wenyeviti); Kamati ya Usalama na Maadili (ndiyo wenyeviti); Halmashauri Kuu ya Mkoa (ndiyo wenyeviti). Sasa wameamua wao waache kiti wajadiliwe badala ya kuwajadili wengine. Na wakati wanaomba uongozi walikabidhiwa dhamana ya kusimika uongozi madhubuti wa kukiletea chama ushindi. Sasa wamaemua kuingia kwenye foleni ya kujadiliwa."
Kanuni yetu inasema:
Mwanachama atakuwa na haki ya kugombea nfasi yoyote ya uongozi lakini edapo kugombea nafasi nyingi kutasababisha kuzorota kwa uhai wa chama, hatateuliwa.
"Una haki ya kugombea lakini vikao vikisema wewe unafaa zaidi kuwa mwenyekiti, na ukitoka kwenye uenyekiti mkoa utayumba, sasa unafaa uenyekiti kuliko ubunge, unaweza ukaambiwa kaa kwenye uenyekiti kwa maslahi ya chama na uhai wa chama. Na wanajua hayo hao viongozi wetu."
“Ukishakuwa kiongozi hutakiwi kuwa na tamaa, ndiyo ujumbe Mwenyekiti ametuambia. Unatakiwa kutosheka, na ni moja ya sifa za kiongozi. Tosheka na dhamana uliyopewa na ukamilishe hiyo dhamana, upimwe kwadhamana hiyo – siyo unatangatanga tu.”
“Ni haki yake, ni haki yake; lakini ajue angepimwa vizuri kwa ngazi yake ya ukuu wa Mkoa. Najua baadhi ya wakuu wa mikoa ambao wamekaa kwa muda mrefu na majina yale utafikiri ni cheo yale. Nsa Kaisi watu wengine wangedhani kuna cheo kinaitwa Nsa Kaisi, lakini kwa kwasababu amekaa kwenye nafasi ile na ameitumikia kama Mkuu wa Mkoa.”
“Kuna mtu unakuta ndani ya miaka mitano tu kapata vyeo vikubwa viwili kwa mpigo alafu kabla hajakomaa pale, anataka ubunge. Ni haki yake lakini ni vizuri kujitathmini na kujitafakari.”
Msimamo wake wa kutogomea nafasi yoyote
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Dr. Bashiru Ally Kakurwa ameweka wazi msimamo wake wa kutogombea nafasi yoyote katika Chama hicho kwani ameridhika na nafasi aliyonayo.
“Mimi sigombei na siwezi kugombea, nimeshakuwa Katibu Kuu nagombea cheo gani?, cheo gani cha maana kuliko kazi hii ya kusimamia haki katika Chama” Katibu Mkuu CCM, Dkt.Bashiru
“Ukishakuwa kiongozi hutakiwi kuwa na tamaa ndio ujumbe Mwenyekiti ametuambia, unatakiwa kutosheka ndio moja ya sifa za kiongozi, tosheka na dhamana uliyopewa na uikamilishe hiyo dhamana na upimwe kwa dhamana hiyo sio unatangatanga tu” Dkt. Bashiru Ally
CCM kila kitu wanafanya kwa maslahi ya mwenyekiti na chama, hakuna sehemu utaona wanasema kwa maslahi ya watanzania. A gang of wicked selfish monsters wanajali matumbo yao tu. Nchi iko palepale haiendelei. Africans kazi ipo sana kutoka kwenge umaskini sio leo wala kesho kwa akili za kishenzi hivi