Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Harambee hiyo imefanyika Mkoani Kigoma tarehe 20 Septemba, 2024 ambapo pamoja na mambo mengine, Waziri Bashungwa amemshukuru Baba Askofu wa Jimbo Katoliki la Kigoma Mhashamu Joseph Mlola kwa kumpa fursa hiyo ya pekee kushiriki Ibada ya Misa na kuongoza Harambee katika Kanisa la Kasumo ambalo umisionari wake ulianza mwaka wa 1985.
Viongozi Wakuu waliochangia katika Harambee hiyo ni pamoja na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Doto Biteko, Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, Naibu Waziri wa Maji Eng. Kundo Mathew, Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Eng. Maryprica Mahundi, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Akisoma Risala kwa niaba ya waumini wa Parokia ya Kasumo, Katibu wa Halmashauri ya Walei wa Parokia hiyo Bw. Onesmo Witae ameeleza kuwa hadi sasa wameweza kukusanya zaidi ya Shilingi Milioni 62 kutoka kwa wadau na marafiki wa Parokia hiyo kwa ajili ya ujenzi wa ukumbi na vyumba vya kulala wageni katika Parokia hiyo.