Basi la Africa Raha Express (T 382 DCS) latelekeza abiria sheli

Basi la Africa Raha Express (T 382 DCS) latelekeza abiria sheli

ALT

Member
Joined
Oct 6, 2021
Posts
78
Reaction score
90
Wanabodi,

Kwa ufupi ni route ya musoma-mwanza. Basi tajwa limenoa nanga saa kumi na moja unusu jioni kuelekea mwanza ambapo kituo cha mwisho inapaswa iwe buzuruga stand.

Changamoto ni gari kuharibika, limeharibikia sheli moja kisesa( mtanirekebisha wenyeji sheli inaitwa "wave").

Ameskika konda akisema "abiria shukeni mchimbe dawa chap."

Tukajua anakunywa mafuta safari iendelee, kumbe ni break down. Karibia dakika thelathini ikabidi abiria kuhoji. Kumbe gari imeharibika.

Abiria wana mizigo mizito, wanafikaje buzuruga na eneo sheli hapo ni mbali na vituo vy daladala? Je nauli ya kufika stendi ya buzuruga analipa nani?

Na kwanini isitolewe taarifa ya gari kuharibika?

Ni maswali aliyoulizwa konda, konda hakua n jibu wala hata kuomba samahani. Kilichofuata ni kama alimpigia simu bosi wake amtumie hela mpesa awalipie abiria wafike buzuruga.

Bana wee, konda akawa kama vile kazunguka upande wa pili wa gari, kumbe katoroka.

Wakawatelekeza abiria na kuacha gari wazi.

ABIRIA WAKAENDA POLISI HAPO KISESA

Wamekutwa askari wawili nje, wamepewa stori nzima na tiketi ya uthibitisho. Kufupisha stori afande mmoja kipara aliyeko zamu muda huu kasema," abiria rudini sheli kapigiwa trafiki anakuja hapo, lakini jiongezeni, tumieni akili zenu, mnaweza kuendelea na safari, hao watu wa basi watawasumbua."

HASIRA ZIKAWAKA

Abiria tayari hawana hela, wametelekezwa, wamepeleka shida zao polisi na polisi hawana msaada, je, wakalilie wapi?

Je, polisi na africa raha express wamekula mbinu kuwakomoa abiria?

Ni kwanini africa raha wajiamini namna hii?

Kwanini polisi wanashindwa ku enforce law kama jeshi? Ilhali nguvu zote wanazo? Wanawake na abiria wenye watoto wadogo usalama wao u juu ya nani?

MAMLAKA HUSIKA, TAFADHALI, TOENI ADHABU IWE FUNZO KWA WATU WA NAMNA HII ILI TABIA ZA NAMNA HII ZISIJIRUDIE.

USIKU MWEMA.
 
Nilishawahi kupitia vigezo na masharti kwenye risiti ya bus moja
Ilinishangaza kuona kuwa kumbe gari likiharibika nauli hairudishwi na napaswa kusubiri hadi litengenezwe au pale litakapokuja lingine
Abiria tunachukua tiketi tu kwa mazoea matukio kama haya ni kuwa mpole tu
 
uendeshhaji wa biashara ya mabasi ni mgumu

Sasa ndio ugumu wao mimi kama abiria nilielipa nauli ya elfu kumi( wakati hua ni elfu nane) kwa hoja ya mafuta kupanda unaniusu nini? Huu ni upumbavu. Hii route ina gari nyingi, unavyo mfanyia abiria hivi, my friend, tayari umempoteza. Quality of service offered speaks louder.
 
Sikilizeni, kama bus imeachwa hapo, fanyeni utaratibu wa kuuza matairi, taa, tank ya mafuta, engine, shock absorber, gearbox, vioo, siti, chassis na vyengine wao waachieni funguo tu apo sheli
 
Wanabodi,

Kwa ufupi ni route ya musoma-mwanza. Basi tajwa limenoa nanga saa kumi na moja unusu jioni kuelekea mwanza ambapo kituo cha mwisho inapaswa iwe buzuruga stand.

Changamoto ni gari kuharibika, limeharibikia sheli moja kisesa( mtanirekebisha wenyeji sheli inaitwa "wave").

Ameskika konda akisema "abiria shukeni mchimbe dawa chap."

Tukajua anakunywa mafuta safari iendelee, kumbe ni break down. Karibia dakika thelathini ikabidi abiria kuhoji. Kumbe gari imeharibika.

Abiria wana mizigo mizito, wanafikaje buzuruga na eneo sheli hapo ni mbali na vituo vy daladala? Je nauli ya kufika stendi ya buzuruga analipa nani?

Na kwanini isitolewe taarifa ya gari kuharibika?

Ni maswali aliyoulizwa konda, konda hakua n jibu wala hata kuomba samahani. Kilichofuata ni kama alimpigia simu bosi wake amtumie hela mpesa awalipie abiria wafike buzuruga.

Bana wee, konda akawa kama vile kazunguka upande wa pili wa gari, kumbe katoroka.

Wakawatelekeza abiria na kuacha gari wazi.

ABIRIA WAKAENDA POLISI HAPO KISESA

Wamekutwa askari wawili nje, wamepewa stori nzima na tiketi ya uthibitisho. Kufupisha stori afande mmoja kipara aliyeko zamu muda huu kasema," abiria rudini sheli kapigiwa trafiki anakuja hapo, lakini jiongezeni, tumieni akili zenu, mnaweza kuendelea na safari, hao watu wa basi watawasumbua."

HASIRA ZIKAWAKA

Abiria tayari hawana hela, wametelekezwa, wamepeleka shida zao polisi na polisi hawana msaada, je, wakalilie wapi?

Je, polisi na africa raha express wamekula mbinu kuwakomoa abiria?

Ni kwanini africa raha wajiamini namna hii?

Kwanini polisi wanashindwa ku enforce law kama jeshi? Ilhali nguvu zote wanazo? Wanawake na abiria wenye watoto wadogo usalama wao u juu ya nani?

MAMLAKA HUSIKA, TAFADHALI, TOENI ADHABU IWE FUNZO KWA WATU WA NAMNA HII ILI TABIA ZA NAMNA HII ZISIJIRUDIE.

USIKU MWEMA.
Polisi amewashauri vizuri tu kuliko kusumbuana na wenye basi ni heri wajiongeze maana hapo kwenye icho kituo cha mafuta ni town tu mtu unaendelea tu na safari lakini kama ukiwa huna kazi za kufanya utaendelea kukaa hapo kubishana na konda wakati ata yeye mwenyewe anawaza gari inayofanya anapata kipato imeharibika me nacho washauri ao abiria wapande dala dala wafike buzuruga kuepusha kupoteza muda
 
siwahi kuona mtu waajabu kama wewe abiria ulie panda hilo basi! yaani umesema kabisa yakuwa gari limeharibika halafu unataka likufikishe stand kivipi haujiongezi tu yaani hiyo alfu10000 yako inatosha matengenezo ya hiyo gari subiri gari itengenezwe ndio safari iendelee unajua bei ya hiyo gari

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Kuna wajinga waliwahi kufanya upuuzi kama huu, basi mimi sikuona tabu.
Kwakua kwenye kibegi changu natembeaga na leather man tool, nikakitoa nikafungua side mirror kisha nikaweka kwenye begi nikaita boda huyooooo nikasema nikawaacha abiria wanashangaa tu. Baada ya kufika ofisi ya mtendaji nikawaeleza story ilivyokua kisha nikafungua kesi ya kutapeliwa na nikaacha side mirror pale hadi watakapo peleka pesa yangu ndipo waichukue...😂
 
Labda ulipa
Kuna wajinga waliwahi kufanya upuuzi kama huu, basi mimi sikuona tabu.
Kwakua kwenye kibegi changu natembeaga na leather man tool, nikakitoa nikafungua side mirror kisha nikaweka kwenye begi nikaita boda huyooooo nikasema nikawaacha abiria wanashangaa tu. Baada ya kufika ofisi ya mtendaji nikawaeleza story ilivyokua kisha nikafungua kesi ya kutapeliwa na nikaacha side mirror pale hadi watakapo peleka pesa yangu ndipo waichukue...😂
Labda kama walikua hawajielewi.

Aya kwaio ukasema umetapeliwa nauli au.?
 
  • Thanks
Reactions: ALT
Labda ulipa

Labda kama walikua hawajielewi.

Aya kwaio ukasema umetapeliwa nauli au.?
Pengine wewe ndio haujielewi ndio maana unakubali kufanyiwa ujinga na unachukulia poa. Sie wengine tulisha pinda na sijawai kukubali ujinga aiseeee.....
Kumbuka tunapo badilishana ticket na pesa, tayari huo ni mkataba baina ya mimi na wewe kunitoa point 1 to point 5. Sasa unapo haribikiwa gari lako nikiwa nimefika point 4, then hilo sio tatizo langu na nijukumu lako wewe kuhakikisha mimi ninafika point 5 kama tulivyo kubaliana.
 
Abiria tayari hawana hela, wametelekezwa, wamepeleka shida zao polisi na polisi hawana msaada, je, wakalilie wapi?

Je, polisi na africa raha express wamekula mbinu kuwakomoa abiria?

Ni kwanini africa raha wajiamini namna hii?

Kwanini polisi wanashindwa ku enforce law kama jeshi? Ilhali nguvu zote wanazo? Wanawake na abiria wenye watoto wadogo usalama wao u juu ya nani?
Siku nyingine polisi wakizingua piga kwa DC, RC au IGP, iliwahi kutusaidia siku moja nasi tulitelekezwa
 
  • Thanks
Reactions: ALT
Polisi amewashauri vizuri tu kuliko kusumbuana na wenye basi ni heri wajiongeze maana hapo kwenye icho kituo cha mafuta ni town tu mtu unaendelea tu na safari lakini kama ukiwa huna kazi za kufanya utaendelea kukaa hapo kubishana na konda wakati ata yeye mwenyewe anawaza gari inayofanya anapata kipato imeharibika me nacho washauri ao abiria wapande dala dala wafike buzuruga kuepusha kupoteza muda
Mleta mada ameweka concerns
  1. Kuna watu hawana nauli ya kufika stand
  2. Kuna watu wana mizigo mizito
  3. Mkataba wa abiria na mtoa huduma ni kuwafikisha stand, kama hawajafikishwa basi ni bovu, watafutiwe means ya kufika
 
  • Thanks
Reactions: ALT
Kuna wajinga waliwahi kufanya upuuzi kama huu, basi mimi sikuona tabu.
Kwakua kwenye kibegi changu natembeaga na leather man tool, nikakitoa nikafungua side mirror kisha nikaweka kwenye begi nikaita boda huyooooo nikasema nikawaacha abiria wanashangaa tu. Baada ya kufika ofisi ya mtendaji nikawaeleza story ilivyokua kisha nikafungua kesi ya kutapeliwa na nikaacha side mirror pale hadi watakapo peleka pesa yangu ndipo waichukue...😂

Bravo....😂😂😂, mwaga mboga namwaga nguna
 
Labda ulipa

Labda kama walikua hawajielewi.

Aya kwaio ukasema umetapeliwa nauli au.?

Pengine wewe ndio haujielewi ndio maana unakubali kufanyiwa ujinga na unachukulia poa. Sie wengine tulisha pinda na sijawai kukubali ujinga aiseeee.....
Kumbuka tunapo badilishana ticket na pesa, tayari huo ni mkataba baina ya mimi na wewe kunitoa point 1 to point 5. Sasa unapo haribikiwa gari lako nikiwa nimefika point 4, then hilo sio tatizo langu na nijukumu lako wewe kuhakikisha mimi ninafika point 5 kama tulivyo kubaliana.
Inategemeana ni masaa mangapi yamepita tangu gari kuharibika sheria za sumatra ni kwamba iwapo gari imeharibika inatakiwa abiria wasubili mpaka litengenezwe ndani ya masaa mawili na iwapo masaa hayo yatapita ndio abiria inatakiwa atafutiwe usafiri mbadala sasa wewe unaposema utareta ubabe nakushangaa iwapo itakua chini ya masaa mawili
 
  • Thanks
Reactions: ALT
Back
Top Bottom