Basi la Africa Raha Express (T 382 DCS) latelekeza abiria sheli

Basi la Africa Raha Express (T 382 DCS) latelekeza abiria sheli

Mleta mada ameweka concerns
  1. Kuna watu hawana nauli ya kufika stand
  2. Kuna watu wana mizigo mizito
  3. Mkataba wa abiria na mtoa huduma ni kuwafikisha stand, kama hawajafikishwa basi ni bovu, watafutiwe means ya kufika

Nakazia mjumbe.... Na hiki ndicho kinanifanya nielewe kwanini kiongozi yeyote wa nchi akiamua kufanya upumbavu wowote anafanya kwasababu keshajua wananchi wengi ni misukule. At all, watu hawalingani vipato. Kuvunja mkataba ni kosa kisheria.

Nimekuja kuonesha kosa ili wenye mamlaka wachukue hatua kama funzo kwa wengine ila kuna narrow minded people hata hawaelewi agenda kubwa ni ipi.

Acha kodi ziwekwe kede kede. At all mafuta yapande bei, tunaumia sisi so viongozi wa serikali, tozo za mihamala zinatuua sisi si serikali ambapo wao hadi communication allowances wanapewa.

Wananchi tuzinduke kama kenya hapo tuu muone kama viongozi watafanya upumbavu.

Nawaibia siri, nchi ya demokrasia, nguvu kamili iko kwa wananchi. Amkeni.
 
siwahi kuona mtu waajabu kama wewe abiria ulie panda hilo basi! yaani umesema kabisa yakuwa gari limeharibika halafu unataka likufikishe stand kivipi haujiongezi tu yaani hiyo alfu10000 yako inatosha matengenezo ya hiyo gari subiri gari itengenezwe ndio safari iendelee unajua bei ya hiyo gari

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app

Ndio watanzania hawa, jamani tuwaombee. Kipindi flani niko chuo tunafanya mgomo, kuna watu kama wewe walijikuta wapenda skuli. Wenzao wakasusia pepa, yeye kaenda kufanya.

Akichapwa mboko hatokuja kusahau, lakini pepa alifutwa tukafanya wote fresh paper baada ya ndalichako kama waziri mwenye mamlaka kuingilia kati.

Yaani hujaona kabisa concerns hapa?
 
Inategemeana ni masaa mangapi yamepita tangu gari kuharibika sheria za sumatra ni kwamba iwapo gari imeharibika inatakiwa abiria wasubili mpaka litengenezwe ndani ya masaa mawili na iwapo masaa hayo yatapita ndio abiria inatakiwa atafutiwe usafiri mbadala sasa wewe unaposema utareta ubabe nakushangaa iwapo itakua chini ya masaa mawili

Ndugu, mimi nilikua kwenye tukio. Sumatra(latra) anasema gari likiharibika abiria asipewe taarifa?

Anasema gari akiaribika dereva na konda wakimbie wawatelekeza abiria?
 
siwahi kuona mtu waajabu kama wewe abiria ulie panda hilo basi! yaani umesema kabisa yakuwa gari limeharibika halafu unataka likufikishe stand kivipi haujiongezi tu yaani hiyo alfu10000 yako inatosha matengenezo ya hiyo gari subiri gari itengenezwe ndio safari iendelee unajua bei ya hiyo gari

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
Ri mjusi....ri reptilia
 
Upo uwezekano polisi na LATRA wakaenda kunufaika na hilo tatizo
 
Wanabodi,

Kwa ufupi ni route ya musoma-mwanza. Basi tajwa limenoa nanga saa kumi na moja unusu jioni kuelekea mwanza ambapo kituo cha mwisho inapaswa iwe buzuruga stand.

Changamoto ni gari kuharibika, limeharibikia sheli moja kisesa( mtanirekebisha wenyeji sheli inaitwa "wave").

Ameskika konda akisema "abiria shukeni mchimbe dawa chap."

Tukajua anakunywa mafuta safari iendelee, kumbe ni break down. Karibia dakika thelathini ikabidi abiria kuhoji. Kumbe gari imeharibika.

Abiria wana mizigo mizito, wanafikaje buzuruga na eneo sheli hapo ni mbali na vituo vy daladala? Je nauli ya kufika stendi ya buzuruga analipa nani?

Na kwanini isitolewe taarifa ya gari kuharibika?

Ni maswali aliyoulizwa konda, konda hakua n jibu wala hata kuomba samahani. Kilichofuata ni kama alimpigia simu bosi wake amtumie hela mpesa awalipie abiria wafike buzuruga.

Bana wee, konda akawa kama vile kazunguka upande wa pili wa gari, kumbe katoroka.

Wakawatelekeza abiria na kuacha gari wazi.

ABIRIA WAKAENDA POLISI HAPO KISESA

Wamekutwa askari wawili nje, wamepewa stori nzima na tiketi ya uthibitisho. Kufupisha stori afande mmoja kipara aliyeko zamu muda huu kasema," abiria rudini sheli kapigiwa trafiki anakuja hapo, lakini jiongezeni, tumieni akili zenu, mnaweza kuendelea na safari, hao watu wa basi watawasumbua."

HASIRA ZIKAWAKA

Abiria tayari hawana hela, wametelekezwa, wamepeleka shida zao polisi na polisi hawana msaada, je, wakalilie wapi?

Je, polisi na africa raha express wamekula mbinu kuwakomoa abiria?

Ni kwanini africa raha wajiamini namna hii?

Kwanini polisi wanashindwa ku enforce law kama jeshi? Ilhali nguvu zote wanazo? Wanawake na abiria wenye watoto wadogo usalama wao u juu ya nani?

MAMLAKA HUSIKA, TAFADHALI, TOENI ADHABU IWE FUNZO KWA WATU WA NAMNA HII ILI TABIA ZA NAMNA HII ZISIJIRUDIE.

USIKU MWEMA.
Acha kulia lia kama mtoto hakuna polisi case hapo hayo ni mambo ya madai
 
Kuna wajinga waliwahi kufanya upuuzi kama huu, basi mimi sikuona tabu.
Kwakua kwenye kibegi changu natembeaga na leather man tool, nikakitoa nikafungua side mirror kisha nikaweka kwenye begi nikaita boda huyooooo nikasema nikawaacha abiria wanashangaa tu. Baada ya kufika ofisi ya mtendaji nikawaeleza story ilivyokua kisha nikafungua kesi ya kutapeliwa na nikaacha side mirror pale hadi watakapo peleka pesa yangu ndipo waichukue...😂
Ofisi ya mtendaji kwanza haina mamlaka ya kufungua kesi na kitu ulicho fanya kufungua side mirror za gari ya watu huo ulikua ni wizi ungekutana na watu waelevu ungejutia kitendo ulicho fanya maana tayari ulisha jichukulia sheria mkononi.

Utakuja kulipishwa vioo vya gari yote siku moja, we utasema unadai 10k wao watasema ulifungua vitu vyenye thamani ya 1M na ushahidi ni hiyo side mirror uliyoenda nayo kwa huyo mtendaji asiejielewa
 
Ubaya zaidi hata Sisi Humu JF wengi hatuwezi saidia. Matatizo ya Nchi Yetu Ni Umasikini
 
Kama wanaume mpo hao ng'oeni hizo tairi za nyuma nakuja chap na mteja anayo cash atawapa pesa ya nauli. Huyo mmiliki wa pesa ile pesa ya kuwarudishieni mfike stand akanunulie tairi.
 
Sikilizeni, kama bus imeachwa hapo, fanyeni utaratibu wa kuuza matairi, taa, tank ya mafuta, engine, shock absorber, gearbox, vioo, siti, chassis na vyengine wao waachieni funguo tu apo sheli
Huo ni wizi sasa watapata pesa zaidi ya nauli yao tairi tu za nyuma tu kwa bei ya hasara wanapata milioni,inawatosha kufika stand.
 
Chomeni moto hilo basi lao mkweche iwe fundisho kwa wangese wengine.
Basi la milioni 300 uchome moto kwa nauli isiyozidi milioni.
Boss muungwana anaetegemea akili na sio ndumba kuendesha biashara,fasta hapo angekodi daladala akampa elf 50,abiria wote wangefika stand kuu.
Mizigo mizito utasubiria gari itengenezwe.
 
Wanabodi,

Kwa ufupi ni route ya musoma-mwanza. Basi tajwa limenoa nanga saa kumi na moja unusu jioni kuelekea mwanza ambapo kituo cha mwisho inapaswa iwe buzuruga stand.

Changamoto ni gari kuharibika, limeharibikia sheli moja kisesa( mtanirekebisha wenyeji sheli inaitwa "wave").

Ameskika konda akisema "abiria shukeni mchimbe dawa chap."

Tukajua anakunywa mafuta safari iendelee, kumbe ni break down. Karibia dakika thelathini ikabidi abiria kuhoji. Kumbe gari imeharibika.

Abiria wana mizigo mizito, wanafikaje buzuruga na eneo sheli hapo ni mbali na vituo vy daladala? Je nauli ya kufika stendi ya buzuruga analipa nani?

Na kwanini isitolewe taarifa ya gari kuharibika?

Ni maswali aliyoulizwa konda, konda hakua n jibu wala hata kuomba samahani. Kilichofuata ni kama alimpigia simu bosi wake amtumie hela mpesa awalipie abiria wafike buzuruga.

Bana wee, konda akawa kama vile kazunguka upande wa pili wa gari, kumbe katoroka.

Wakawatelekeza abiria na kuacha gari wazi.

ABIRIA WAKAENDA POLISI HAPO KISESA

Wamekutwa askari wawili nje, wamepewa stori nzima na tiketi ya uthibitisho. Kufupisha stori afande mmoja kipara aliyeko zamu muda huu kasema," abiria rudini sheli kapigiwa trafiki anakuja hapo, lakini jiongezeni, tumieni akili zenu, mnaweza kuendelea na safari, hao watu wa basi watawasumbua."

HASIRA ZIKAWAKA

Abiria tayari hawana hela, wametelekezwa, wamepeleka shida zao polisi na polisi hawana msaada, je, wakalilie wapi?

Je, polisi na africa raha express wamekula mbinu kuwakomoa abiria?

Ni kwanini africa raha wajiamini namna hii?

Kwanini polisi wanashindwa ku enforce law kama jeshi? Ilhali nguvu zote wanazo? Wanawake na abiria wenye watoto wadogo usalama wao u juu ya nani?

MAMLAKA HUSIKA, TAFADHALI, TOENI ADHABU IWE FUNZO KWA WATU WA NAMNA HII ILI TABIA ZA NAMNA HII ZISIJIRUDIE.

USIKU MWEMA.
Nenda kwa DC au RC wa eneo hilo.
 
Mfanyabiashara kumwacha Mteja ananung'unika ni kosa kubwa sana. Unajiharibia biashara yako mwenyewe..

Nina uhakika abiria 50 waliomo kwenye hilo Basi hawatathubutu tena kurudia kupanda mabasi ya Kampuni hiyo..

Wafanyabiashara wengine wanachokifanya, huita Costa mbili na kupatana nao wawasogezee Abiria stand.. Isitoshe Kisesa - Buzuruga siyo umbali mrefu kiasi cha kukimbia Jukumu la kumfikisha Abiria kwenye final destination..
 
Basi la milioni 300 uchome moto kwa nauli isiyozidi milioni.
Boss muungwana anaetegemea akili na sio ndumba kuendesha biashara,fasta hapo angekodi daladala akampa elf 50,abiria wote wangefika stand kuu.
Mizigo mizito utasubiria gari itengenezwe.
Usilinganishe thamani ya basi na utu wa mtu.
Wakichoma moto hilo basi next time mwenye basi atakuwa na akili timamu.
 
Muwe mna angalia na ma bus ya kupanda hilo bus lina onekana tu ni choka mbaya
 
Wanabodi,

Kwa ufupi ni route ya musoma-mwanza. Basi tajwa limenoa nanga saa kumi na moja unusu jioni kuelekea mwanza ambapo kituo cha mwisho inapaswa iwe buzuruga stand.

Changamoto ni gari kuharibika, limeharibikia sheli moja kisesa( mtanirekebisha wenyeji sheli inaitwa "wave").

Ameskika konda akisema "abiria shukeni mchimbe dawa chap."

Tukajua anakunywa mafuta safari iendelee, kumbe ni break down. Karibia dakika thelathini ikabidi abiria kuhoji. Kumbe gari imeharibika.

Abiria wana mizigo mizito, wanafikaje buzuruga na eneo sheli hapo ni mbali na vituo vy daladala? Je nauli ya kufika stendi ya buzuruga analipa nani?

Na kwanini isitolewe taarifa ya gari kuharibika?

Ni maswali aliyoulizwa konda, konda hakua n jibu wala hata kuomba samahani. Kilichofuata ni kama alimpigia simu bosi wake amtumie hela mpesa awalipie abiria wafike buzuruga.

Bana wee, konda akawa kama vile kazunguka upande wa pili wa gari, kumbe katoroka.

Wakawatelekeza abiria na kuacha gari wazi.

ABIRIA WAKAENDA POLISI HAPO KISESA

Wamekutwa askari wawili nje, wamepewa stori nzima na tiketi ya uthibitisho. Kufupisha stori afande mmoja kipara aliyeko zamu muda huu kasema," abiria rudini sheli kapigiwa trafiki anakuja hapo, lakini jiongezeni, tumieni akili zenu, mnaweza kuendelea na safari, hao watu wa basi watawasumbua."

HASIRA ZIKAWAKA

Abiria tayari hawana hela, wametelekezwa, wamepeleka shida zao polisi na polisi hawana msaada, je, wakalilie wapi?

Je, polisi na africa raha express wamekula mbinu kuwakomoa abiria?

Ni kwanini africa raha wajiamini namna hii?

Kwanini polisi wanashindwa ku enforce law kama jeshi? Ilhali nguvu zote wanazo? Wanawake na abiria wenye watoto wadogo usalama wao u juu ya nani?

MAMLAKA HUSIKA, TAFADHALI, TOENI ADHABU IWE FUNZO KWA WATU WA NAMNA HII ILI TABIA ZA NAMNA HII ZISIJIRUDIE.

USIKU MWEMA.
Sitasahau safari yangu kutoka lindi mpaka Dar. Ilikuwa yamateso
 
Back
Top Bottom