Battle: Mwanza (The Rock City) Vs Arusha (A-Town/Chuga)

Battle: Mwanza (The Rock City) Vs Arusha (A-Town/Chuga)

cleokippo

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2014
Posts
2,118
Reaction score
1,797
Kumekuwa na sintofahamu kati ya Majiji haya mawaili yanatotikisa Tanzania ukiachilia Dar.

Majiji haya yamezua gumzo miongoni mwa watu kwa kujaribu kuyashindanisha lakini pamoja na kuyashindanisha kote bado watu hawajapata jibu la moja kwa moja kwamba ni mji gani mzuri na una fursa kubwa za kimaisha kuliko mwingine pamoja na ukuaji wa maendeleo.

Karibuni mchangie
 
Mimi niko Arusha miaka yote maeneo mengine nafanya kutembelea ila kusema ukweli Arusha Bado kuifananisha na mwanza
Tatizo la mwanza ni Barabara na usiku mji uko giza Sana hakuna taa za Barabarani kabisa mwanza. Ila kwenye mambo mengine pako poa
 
Nani hajapata jibu?

Mwanza sio ya kuilinganisha na vimji vya ajabu ajabu kama Arusha.

Mwanza inakimbizana na Dar kwenye kila kitu, miundombinu, mapato, wingi wa watu, uchangamfu, starehe, watoto wazuri, vyuo, nk. Muwe mnasoma hata takwimu/taarifa za serikali zinatolewa kila mara kuonyesha Mwanza is untouchable.

Arusha ilinganisheni na Kahama ama Musoma sio Mwanza ni kuivunjia heshima Mwanza.
 
Hivi Chuga ina maana gani?... Naomba tafsiri yake na uhusiano wake na Arusha.
 
Fact is Mwanza imeizidi Arusha kwa vitu vingi, hata population ya Mwanza ni kubwa kuliko ya Arusha.

Hata kwenye ushindani kati ya NBI na DSM, pia Wakenya hupenda kuweka Mombasa na Mwanza kwani ni miji inayokaribiana, ingawa Mombasa inazidi kidogo Mwanza. Ukweli ni kwamba kwa kila mizania, Mwanza iko juu ya Arusha. Kwa hali ya hewa Arusha ni green city. Hata hivyo Mwanza ni kubwa, Mwanza ina population kubwa na kiuchumi Mwanza iko juu ya Arusha(angalau kwa sasa)
 
Hata kwenye ushindani kati ya NBI na DSM, pia Wakenya hupenda kuweka Mombasa na Mwanza kwani ni miji inayokaribiana, ingawa Mombasa inazidi kidogo Mwanza. Ukweli ni kwamba kwa kila mizania, Mwanza iko juu ya Arusha. Kwa hali ya hewa Arusha ni green city. Hata hivyo Mwanza ni kubwa, Mwanza ina population kubwa na kiuchumi Mwanza iko juu ya Arusha(angalau kwa sasa)
Duh! Hapo sasa itabid nikubaliene na mawazo yenu... maana sion mchangiaj hata mmoja aliyesema arusha inaizid mwanza
 
Back
Top Bottom