Batuli Actress aka Cleopatra Nabisha Hodi

Batuli Actress aka Cleopatra Nabisha Hodi

duh umeniamasisha nianze kukufatilia maana unaonekana unajitambua flani,,,ujue mie nimetokea kuwadharau sana bongo movie...huwezi amini batuli imefikia hatua nikiingia sehemu nikikuta wanaangalia filamu ya kibongo nageuzia mlangoni kwa hasira..ila kusema ukweli nimekupendaje ghafla,,,bongo movie unajua hadi habari za soko la hisa!!!sikuwai kutegemea ilo.


msalimie Malkia nasikia nae ameanza kunusa,,mshaurini aache huo sio ujanja amuulize kiuno bila mfupa.

Asante sana. Malkia ni yupi huyo?
 
Batuli aka Cleopatra,
zamani nilikua napenda sana maigizo ya kitanzania enzi za kina mzee Jengua, Swebe, Muhogo mchungu, Siyawezi na wenzie kina Uledi (igizo la damu nzito), nk.

Tatizo lilianza pale zilipoibuka hizi zinazoitwa Bongo Movie. Yaani watu hawajui/hawawezi kuvaa uhusika, pia wanaojiita wasanii/waigizaji wa hizi filamu naweza kusema kua ni wezi kupitia kazi zao. Ndiyo ni wezi kwa maana kua unakuta filamu imechezwa nzima lakini inakatwa vipande na kuitwa part 1 na part 2 lakini ukiangalia hakuna ulazima huo.

Kituko kingine utakuta filamu ni ya Kitanzania, imechezwa mazingira ya Kitanzania, lugha iliyotumika ni Kiswahili lakini JINA LA FILAMU NI KINGEREZA mfano "fake smile" (waweza eleza ilikuaje mkaiita hivyo badala ya kutumia Kiswahili?).

Natamani yarudi maigizo ya kina Muhogo mchungu kuliko hizi bongo movie. Vinginevyo karibu Jamiiforums.

Asante kwa maoni yako. Yatazingatiwa katika kazi zangu binafsi.

Kama nilivyoandika, jina la Movie zinategemea sana, Story Writer na Producer. Msanii kazi yangu ni kuigiza.

Sina uhakika na mambo ya part 1 & 2 maana hili liko kwa Distributors zaidi pia. Huenda limekaa Kibiashara zaidi.
 
Karibu jf but tunaomba mpunguze kuvaa nguo za nusu uchi...sisi tunataka kazi na si maungo yenu...waambie hao....maana nguo za club ndo wanazivaa kwenye shooting sijui ndo mauzo..mpk ney akawaamba makahaba wenye viwango wako bongo movie...achen

Asante. Umesomeka I hope Wasanii tutazingatia ushauri huu.
 
Mimi sio mtazamaji sana wa bongo movie na sijawahi tazama filamu uliyoigiza, lkn kwa vile umejiunga JF ngoja nitajidi nitazame kazi ulizofanya.

Karibu JF.
 
Hongera kwa kutumia really Username yako.
Japo Me nalionea ungetumia ID nyingine ili uweze kujua watu tunawachukuliaje nyie katika Jamii yetu ya KITANZANIA. Japo utaniuuliza kwani kwa kumia jina hili hutajua?
Utajua lakini sio kama ambavyo ungetumia Jina lingine, wapo watu wengine watasema kuwa wanakufagilia sana kumbe ni wanafiki tu. Kwa Mfano; Mtu ukianzisha Thread "Napenda sana anavyoigiza huyu msanii BATULI wengine watacomment hivi " Aaahhhhh!!!!!!! Yule ni Malaya wa kutupwa".

Yangu ni hayo tu, Karibu na karibia na Uwakaribishe wasanii wenzako ili nao wakaribie katika Jukwaa la The Greater Thinkers.
 
Hongera kwa kutumia really Username yako.
Japo Me nalionea ungetumia ID nyingine ili uweze kujua watu tunawachukuliaje nyie katika Jamii yetu ya KITANZANIA. Japo utaniuuliza kwani kwa kumia jina hili hutajua?
Utajua lakini sio kama ambavyo ungetumia Jina lingine, wapo watu wengine watasema kuwa wanakufagilia sana kumbe ni wanafiki tu. Kwa Mfano; Mtu ukianzisha Thread "Napenda sana anavyoigiza huyu msanii BATULI wengine watacomment hivi " Aaahhhhh!!!!!!! Yule ni Malaya wa kutupwa".

Yangu ni hayo tu, Karibu na karibia na Uwakaribishe wasanii wenzako ili nao wakaribie katika Jukwaa la The Greater Thinkers.

Asante sana. Kama nilivyosema nimejiunga JF kwa ajili ya kujifunza na pia kubadilishana mawazo. Changamoto zinaweza kuwepo na kwangu binafsi ni jambo la kawaida na zinaweza kunisaidia kujijenga zaidi.
 
Back
Top Bottom