BAVICHA: Tumesikitishwa sana na walioenda kuapa, ni kitendo cha usaliti, hujuma na hakiwezi kuvumilika. Wataka hatua kali zichukuliwe

John Pambalu anaROMOKWA tu.

Kilichopo mbona KIWAZI jamani.

Halima J.Mdee ameikata MIZIZI KONGWE ya STATUS QUO...yaani ile MBELEKO MGONGONI mwa mh.Mbowe.

Yaani kule "kubebana".
 
Mbona nyie viongozi wenu wameingia madarakani kwa kura feki na kuiba kura Nani kawaajibisha? Si ndo kwanza mnawatetea?. Leo CCM wanamuona Halima kakosea wakati chanzo Cha yote Ni MWENYEKITI WA CCM NA NEC YAKE.

Mimi simlaumu HALIMA na sintokuja kumlaumu kamwe.
Nitamlaumu Magufuli na NEC yake hao ndo chanzo
Unazidi kujichanganya, real criminals wanawazidi akili, badala ya kuwawajibisha, mnawatetea tena kwa nguvu zote, so sad!
 
Chadema haiishiwi majembe, kama huyo Mdee aliokotwa jalalani mwambieni ajue wataokotwa wengine wawe zaidi yake.

Chadema ni wapenzi na wanachama, sio hao wajuaji waliojiona wameota mapembe.
 
Kumfukuza Halima James Mdee kutakuwa HAVOC kwa CHADEMA.

Halima ndiye mpambanaji WA KWELI ALIYEWAVUTA WANAWAKE KUIPENDA CHADEMA.
 
Ukimtimua tu HALIMA MDEE.

Yale maneno yenu ya KUTHAMINI MCHANGO WA WANAWAKE na dhima yenu ya KUISIMAMIA demokrasia yatakuwa ni DEBE TUPU.

Chadema ACHENI MFUMO DUME.
Chadema ACHENI MFUMO DUME.
 
Huyu mwenyekiti anafokafoka tuuu hata hajui cha kusimamia. Umoja wa vijana wanatakiwa kuwasilisha mapendekezo kamati kuu kwa baraka. Yeye anaitangazia dunia, je kamati kuu ikikataa ku adopt mapendekezo watakwenda mahakamani.????? Anachofanya huyo dogo ni insubordination kwa kamati kuu, yeye ndiyo afukuzwe
 
13m x 60 months+90m ( v8)+ 300m ( kiinua mgongo)

Jumla hapo ni 1.170 billion kwa miaka 5 hapo hatujaongelea zile laki 3 per day during a bunge sessions wala ma posho ya kamati kadhaa hasa kama ile ya PAC ambayo imemuwezesha Mtoto wa Mwandiga kuishi eneo moja na kina Bakhresa, Sofia Simba, n.k

Aache mzigo wote kwa ajili ya 'heshma aliyojijengea?

Wee ungeacha kusema ukweli?
Halima hivi alishindwaje kulinda heshima aliyoijenga kwa jasho na damu miaka zaidi ya 15 akiwa mbunge. Hata kama ni hela mshahara wa miaka yote alikuwa anapeleka wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…