BAWACHA kuwapeleka Mahakamani wabunge 19 waliofutwa uanachama CHADEMA

BAWACHA kuwapeleka Mahakamani wabunge 19 waliofutwa uanachama CHADEMA

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) limesema litakwenda mahakamani kufungua kesi iwapo wanawake 19 waliofukuzwa katika chama hicho wataendelea kutambulika kama wabunge wa Chadema.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Jumamosi Aprili 24, 2021 mweka hazina wa Bawacha, Catherine Ruge amesema watachukua hatua hiyo iwapo wabunge hao wataendelea kuwepo bungeni na kwamba wapo tayari kuuthibitishia umma kuwa walifukuzwa Chadema.

Amesema wanamtaka Spika wa Bunge, Job Ndugai kujitokeza hadharani kuwaeleza Watanzania kama kweli ofisi ya Bunge haikupokea uthibitisho wa Chadema wabunge hao kufukuzwa uanachama.

"Hatutaendelea kuona katiba inaendelea kuvunjwa kwani ofisi ya Bunge inafahamu kwamba wabunge hao wamepoteza sifa za kuwa wabunge."

"Ni jambo la dharau kuona chama kinasema kimewavua ubunge wanachama wao eti naibu spika anakataa na kusema hana taarifa..., na si kweli kama Bunge halina taarifa ya kuvuliwa uanachama hao wanaoitwa wabunge wa Chadema hii ni dharau kubwa," amesema Catherine.
 
Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) limesema litakwenda mahakamani kufungua kesi iwapo wanawake 19 waliofukuzwa katika chama hicho wataendelea kutambulika kama wabunge wa Chadema.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Jumamosi Aprili 24, 2021 mweka hazina wa Bawacha, Catherine Ruge amesema watachukua hatua hiyo iwapo wabunge hao wataendelea kuwepo bungeni na kwamba wapo tayari kuuthibitishia umma kuwa walifukuzwa Chadema.

Amesema wanamtaka Spika wa Bunge, Job Ndugai kujitokeza hadharani kuwaeleza Watanzania kama kweli ofisi ya Bunge haikupokea uthibitisho wa Chadema wabunge hao kufukuzwa uanachama.

"Hatutaendelea kuona katiba inaendelea kuvunjwa kwani ofisi ya Bunge inafahamu kwamba wabunge hao wamepoteza sifa za kuwa wabunge."

"Ni jambo la dharau kuona chama kinasema kimewavua ubunge wanachama wao eti naibu spika anakataa na kusema hana taarifa..., na si kweli kama Bunge halina taarifa ya kuvuliwa uanachama hao wanaoitwa wabunge wa Chadema hii ni dharau kubwa," amesema Catherine.
Kwanini halmashauri kuu isikae na kupitia rufaa zao na kuhalalisha maamuzi ya kamati kuu?
Huu mchezo Chadema mnauchelewesha wenyewe.
 
Kwanini halmashauri kuu isikae na kupitia rufaa zao na kuhalalisha maamuzi ya kamati kuu?
Huu mchezo Chadema mnauchelewesha wenyewe.
Na ikizikataa ndio wataenda Mahakamani ambako Mahakamani watapiga full stop zoezi zima.

Amandla...
 
Confused somehow, hao wanawake walishafukuzwa lakini Chadema nao kuna mambo siwaelewi, uchaguzi wa Bawacha kujaza hizo nafasi zao utafanyika lini? zile rufaa za hao wanawake nazo zitasikilizwa lini?

Hao wanawake sasa hivi wamebakiwa na defence moja tu ya tumekata rufaa, na hii defence japo ni potofu ndio inayotumiwa mpaka na speaker kule bungeni, sijui kwanini Chadema hawataki kuumaliza huu mchezo.
 
uchaguzi wa bawacha umeshafanyika? na je kwann nafasi ya mwenyekiti ni kaimu na sio mwenyekiti kamili kama hawawatambui akina mdee?
Mkuu Nambisa, kuna kitu kinaitwa 'procedure ' ndio maana hata CCM kwa sasa hawana MWENYEKITI TAIFA ila wana Makamus. Kutokuwepo Mwenyekiti Taifa wa Chadema haihalalishi litabuliwa kwao.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Jumamosi Aprili 24, 2021 mweka hazina wa Bawacha, Catherine Ruge amesema watachukua hatua hiyo iwapo wabunge hao wataendelea kuwepo bungeni na kwamba wapo tayari kuuthibitishia umma kuwa walifukuzwa Chadema.
Chadema ni chama cha kihuni,kila mtu anaongea
Hao wabunge wamekata rufaa kwenye baraza kuu,na rufaa yao haijasikilizwa,kihere here cha kwenda mahakani kinatoka wapi?
 
Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) limesema litakwenda mahakamani kufungua kesi iwapo wanawake 19 waliofukuzwa katika chama hicho wataendelea kutambulika kama wabunge wa Chadema.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Jumamosi Aprili 24, 2021 mweka hazina wa Bawacha, Catherine Ruge amesema watachukua hatua hiyo iwapo wabunge hao wataendelea kuwepo bungeni na kwamba wapo tayari kuuthibitishia umma kuwa walifukuzwa Chadema.

Amesema wanamtaka Spika wa Bunge, Job Ndugai kujitokeza hadharani kuwaeleza Watanzania kama kweli ofisi ya Bunge haikupokea uthibitisho wa Chadema wabunge hao kufukuzwa uanachama.

"Hatutaendelea kuona katiba inaendelea kuvunjwa kwani ofisi ya Bunge inafahamu kwamba wabunge hao wamepoteza sifa za kuwa wabunge."

"Ni jambo la dharau kuona chama kinasema kimewavua ubunge wanachama wao eti naibu spika anakataa na kusema hana taarifa..., na si kweli kama Bunge halina taarifa ya kuvuliwa uanachama hao wanaoitwa wabunge wa Chadema hii ni dharau kubwa," amesema Catherine.
A good move to expose the hypocrisy
 
Ccm watafanya uchaguzi mwezi huu mwishoni na nafasi ni ya Mama Samia. ila kwa bawacha wameitisha uchaguzi tatizo nafasi ya mwenyekiti wameweka kaimu mwenyekiti sio mwenyekiti kamili
Mkuu Nambisa, kuna kitu kinaitwa 'procedure ' ndio maana hata CCM kwa sasa hawana MWENYEKITI TAIFA ila wana Makamus. Kutokuwepo Mwenyekiti Taifa wa Chadema haihalalishi litabuliwa kwao.
 
Back
Top Bottom