BBC Dira ya Dunia: Zari athibitisha kuachana rasmi na Diamond

Leo ndio nimegundua kua hela sio kila kitu.na mapenzi sii pesa,isipo kua kwa maskini pekee pesa ndio mapenzi.
 
Zari athibitisha Wema Sepetu ndiye amevunja mahusiano yake na Diamond

Unazikumbuka picha za Wema Sepetu na Diamond Platnumz zilizosambaa wakiwa wamekumbatiana kwa mahaba wakati wa sherehe ya kumkaribisha Maromboso au ‘Mbosso’ iliyofanyika mwezi uliopita katika hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam?
Basi tukio lile ndio limesababisha Diamond kuweza kupigwa chini na mama watoto wake, Zari The Bosslady.
Akiongea katika kipindi cha runinga cha Dira ya Dunia ya BBC Swahili, Zari amesema, “Tulikuwa tunajaribu kuona we can move from hiyo sikendo ya kupata mtoto. So we can move forward lakini vitu kama hivyo leo unasikia hivi unaona vile sijui kukumbatiana huko na maex kwenye public vitu vya kunidhalilisha, kunifanya niwe very disrespect na watoto wangu unaona tu like it’s just not right.”

Zari ameongeza kuwa Diamond hakuwahi kumueleza chochote kuhusu picha hizo na wala yeye hakuwahi kumuuliza kwa kuwa aliona haina maana kwake.
^^Bongo5^^
 
Mie kwa maoni yangu hata kama hujabahatika mapenzi ni matamu sana hata wale ambao hawajabahatika na baadhi kujiapiza sitaki kupenda tena bado hurudi tena ndani ya mapenzi.

Of course ni starehe kama starehe zingine
 
Huyu dada kelele nyingi sana, labda ndio kawaida yao wakiachwa au kuacha, kama mwanaume naelewa kwanini Diamond hajapiga makelele wala nini..
 
Money can't buy everything..
 
Duh mwanamke yuko vizuri kimaisha yaani watoto kasema hata baba asipotake CARE yy atatacare
No dogo atapigwa hela ndefu kisomi tu, nyie subirini hapa yule mwanamke hachomoki bure ashajua wapi atampatia timming, Diamond ajiangalie sana sasa hivi maana nikikumbuka ile action ya kusubiria X wake yuko mahututi fasta kamuacha domo madale akakimbilia hospitali kumdai Ivan mirathi .
Ule ukakamavu si wa dunia hii
 
Rayvanny alikuwa BBC, Zari naye BBC hapo hapo kuna tukio la uzinduzi wa album ya Diamond. Bado naamini hizi ni kiki tu na sidhani kama kuna kuachana.

aisee..., ujinga huu
 
Matunzo ya watoto vipi? Ile nyumba ya sauz siwamechuma wote wanapiga pasu au? Naona kuna mtu anataka kupelekwa kwa pilato
 
Hili limama sijui likoje ndio ukamtangaze mwenzio bbc? Ovyo!
 
Ila inauma kujifanya umemwacha mwanaume halafu hata kukutumia SMS ya sorry hajakutumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…