Mahakama ya Ubelgiji imeiamuru serikali ya nchi hiyo kuwalipa fidia wanawake watano waliochukuliwa kwa lazima kutoka katika familia zao katika enzi ya ukoloni wa Ubelgiji nchini DR Congo.
Wanawake hao, ambao sasa wana umri wa miaka 70, walichukuliwa kutoka kwa mama zao walipokuwa watoto wadogo na kupelekwa katika vituo vya watoto yatima chini ya mpango wa serikali.
Mahakama imesema serikali ilikuwa na "mpango maalumu wa kuwatafuta na kuwateka nyara watoto waliozaliwa na mama mweusi na baba mzungu."
Siku ya Jumatatu majaji walisema, “ulikuwa ni uhalifu dhidi ya ubinadamu” na utekaji nyara huo ni "kitendo cha kinyama cha mateso."
Serikali ya Ubelgiji mwaka 2019 iliomba radhi rasmi kwa waathiriwa 20,000, waliotenganishwa kwa nguvu na familia zao nchini DR Congo, pamoja na Burundi na Rwanda.
DR Congo ilitawaliwa na Ubelgiji kama koloni kutoka 1908 hadi 1960.
Baba wengi wa kizungu walikataa kuwatambua watoto wao wa rangi mchanganyiko au kukiri kuwa ni watoto wao, na watoto hao pia hawakupokea utaifa wa Ubelgiji moja kwa moja.
Kwa hivyo walichukuliwa kwa nguvu na kupelekwa katika vituo vya watoto yatima vinavyosimamiwa na Kanisa Katoliki, ambapo mara nyingi walipitia unyanyasaji.
2017, kanisa katoliki liliomba msamaha kwa waathiriwa. Na 2019, serikali ya Ubelgiji iliomba msamaha kwa kuhusika kwake.
Wanawake hao, ambao sasa wana umri wa miaka 70, walichukuliwa kutoka kwa mama zao walipokuwa watoto wadogo na kupelekwa katika vituo vya watoto yatima chini ya mpango wa serikali.
Mahakama imesema serikali ilikuwa na "mpango maalumu wa kuwatafuta na kuwateka nyara watoto waliozaliwa na mama mweusi na baba mzungu."
Siku ya Jumatatu majaji walisema, “ulikuwa ni uhalifu dhidi ya ubinadamu” na utekaji nyara huo ni "kitendo cha kinyama cha mateso."
Serikali ya Ubelgiji mwaka 2019 iliomba radhi rasmi kwa waathiriwa 20,000, waliotenganishwa kwa nguvu na familia zao nchini DR Congo, pamoja na Burundi na Rwanda.
DR Congo ilitawaliwa na Ubelgiji kama koloni kutoka 1908 hadi 1960.
Baba wengi wa kizungu walikataa kuwatambua watoto wao wa rangi mchanganyiko au kukiri kuwa ni watoto wao, na watoto hao pia hawakupokea utaifa wa Ubelgiji moja kwa moja.
Kwa hivyo walichukuliwa kwa nguvu na kupelekwa katika vituo vya watoto yatima vinavyosimamiwa na Kanisa Katoliki, ambapo mara nyingi walipitia unyanyasaji.
2017, kanisa katoliki liliomba msamaha kwa waathiriwa. Na 2019, serikali ya Ubelgiji iliomba msamaha kwa kuhusika kwake.