Beatrice Mwaipaja pole sana ushuhuda wako ni mzito lakini hatimae utashinda kwani Kristo alishinda

Beatrice Mwaipaja pole sana ushuhuda wako ni mzito lakini hatimae utashinda kwani Kristo alishinda

kitu ambacho sikuelewa ni hiki, anasema kuna mchungaji mmoja ambaye ni mwanamke, alikuwa kiongozi mkubwa wa TLP pale Makambako na Mbeya, huyo alikuwa na imani ya kishetani na aliwaingiza wao. ni nani huyo?

kama waliingia kwenye imani hiyo, na dadake huyo akarudi kumshukuru na kuungana na imani hiyo, alishoaondoka? nyimbo anazoimba yupo chini ya huyo mungu wake na imani potofu au alishaokoka sasa?

binafsi nawajua walivyoanza hao mabinti, hali ya umasikini wanayoisema ni kweli, alipokuwa anaanza kabisa, Martha alishawahi kuja kanisani kwetu, alikuwa mwembamba, mweusi, anayeonekana kama ametoka uwanja wa fisi fulani hivi, nguo alizovaa ilikuwa kasketi ka mtu masikini kale ka sagulasagula mitumba na ka tshirt keupe ka mtumba sidhani kama hata kufua alikuwa amefua. maana ilionekana ni kauka nikuvae. alikaribishwa akaimba wimbo wake hata kabla hajarekodi. kama ni Mungu aliwainua, kweli Mungu anajua kuinua watu (kama nimjuavyo Mungu), ila shida inakuja, imekuwaje baada ya kupata pesa tayari wanavaa nguo za kubana, anazunguka na binti anayevaa taiti chafu, na wanazunguka naye, na kuna kashfa ya usagaji ambayo yeye hataki kujitenga nayo. si afukuze huyo binti ili kuondoa matope anayorushiwa? kwani huyo binti ana nini cha ziada hadi anasafiri naye kongo na kwengine na yote yanayosema juu yake? kwa nini tusiamini, na kwanini hamsaidii mdogo wake?OK tuseme mdogo wake alimchukulia ndoa au vyovyote (though wote walikuwa na ndoa na kwa wanyakyusa kulala na shemeji ni kawaida tu), basi amkumbuke mama yake ambaye alishakuwa hadi kichaa na aliwasaidia kuwakuza kwa shida hadi wakafika hapo.
Kumbe Wanyaki kulala na shemeji ni kawaida?
 
Gospel music industry ya Tz asilimia 90 imeshavamiwa na Ibilisi. Ndio maana niliacha kuwafatilia toka 2010. Gospel zangu ni Gaither vocal Band, Doen Moen, Carrie Underwood, Cece winans. Period.
Kwamba Shetani anakiogopa Kiinglishi?🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom