Ben Saanane aliniunganisha na wauza kemikali za migodini kutoka India, nikawa napeleka Msumbiji migodini. Leo simpati

Sijafuta namba yake ya simu hadi sasa..japokua sikua mtu wa siasa tulielewana...tulikutana sinza akapenda mastory yangu ya town...tukapeana namba
Sijui yaliyomkuta ila ninaamini MUNGU sio Mwanadamu....
 
Mrangi anajifanyaga kitengo, yaani kufungua kijiwe cha shoe shine pale posta, na kufanya kazi kwa miaka mingi, basi, akifika mtaani na visimu vyake feki, anawatisha
mrangi ndugu yako anakuita huku
 
Hamna mtu anaweza kumtunza mda wote huo,jamaa walishammaliza kitambo.
 
Mrangi anajifanyaga kitengo, yaani kufungua kijiwe cha shoe shine pale posta, na kufanya kazi kwa miaka mingi, basi, akifika mtaani na visimu vyake feki, anawatisha
😆 umeniuaaa

Ova
 
Pole sana.
Kwa namma jinsi matukio haya yalivyotokea ya utekaji nchini toka kwa bwana yule hadi sasa yote yanafanana na kwa ushuhuda wa survivor sativa mimi naona hawa waanga waliobaki ambao bado hakuna taarifa zao wamekwisha fariki tena kwa vifo vibaya sana.
Watakuwa waliwapeleka kwenye mbuga na kuwatupa huko Simba au fisi wawamalizie kuondoa ushahidi.
Ni kumuachia Mungu tu hapo..kuna watu ni mashetani wanaoishi jamani.
 
Muulize Bashite alikuwa anawasiliana na Ben ili wazungumze kuhusu nini? Alikuwa anafanya juu chini akutane na ben ,siku mbili kabla ya kukutana Ben akapotea.
Mkuu nadhani swali umelielewa! Kama hujalielewa naweza kufafanua zaidi. Lakini, kama umelielewa na unatumia bandiko hili kulipuuza tuendelee na mjadala.
 
Chanzo cha kuuawa kwa Ben ni kuchallenge Phd ya "MTU FURANI'. ,hayo mengine ni camouflage.
Hayo unayajua wewe,hata huko chamani kwake alikua na maadui.
Wanajua vizuri yuko wapi,mi sina chama ila muache uongo.
 
Hayo unayajua wewe,hata huko chamani kwake alikua na maadui.
Wanajua vizuri yuko wapi,mi sina chama ila muache uongo.
Zitto alishamaliza kazi kwenye uchunguzi wa nani aliyemteka Ben au haujaangalia Bunge? Kwa kifupi waliomteka Ben na kumuua ni watu wa TEETH ,ingekuwa mtu tofauti na wao angeshakamatwa kitambo ,hauwezi kufanya tukio lolote la uhalifu bila kuacha trace.

Mtu yeyote akiuawa ukifuatilia nyuma huko utakuta kwamba kuna mtu anahusika kwa kifo cha huyo mtu ,na polisi ndiyo wanaanzia hapo na wanambana mpaka anaeleza ukweli na anaenda kuleleza alimpomzika kwahiyo ingekuwa Mbowe au chadema wana husika wangekuwa washakamatwa kitambo sana.
 
Mkuu nadhani swali umelielewa! Kama hujalielewa naweza kufafanua zaidi. Lakini, kama umelielewa na unatumia bandiko hili kulipuuza tuendelee na mjadala.

Nimelielewa na ndiyo maana nimekujibu ,mtu wake wa karibu alikuwa Bashite ,na ndiye aliyepewa maelekezo ,ndiyo maana nikakwambia muulize bashite anajua kila kitu hadi maagizo aliyopewa na "MTU FURANI" baada ya kupigwa za uso kuhusu Phd Feki yake ya maganda ya korosho.

Vaa Picha kwamba Ben ni mwanao ,ungetetea genge la wauaji wa mwanao au siasa inakuondolea UTU? Huyo aliyetoa amri yuko wapi?
 
R.i.P Classmate...😥
Pole sana mkuu...🤝
Sasa..... hua unamkumbuka mke wake hata kwa chochote kitu kutokana na wema alio kutendea Ben Saanane..??
 
Vaa Picha kwamba Ben ni mwanao ,ungetetea genge la wauaji wa mwanao au siasa inakuondolea UTU? Huyo aliyetoa amri yuko wapi?
Kuna asilimia kubwa umelielewa swali vema. Lakini, kitendo cha kutokuja na maelezo ya kutosha kuhusu ushahidi na kumalizia bandiko lako kwa kuamsha hisia za hizuni kwa Watanzania sote tupendao amani, kinapunguza Objectivity yako katika kupata ukweli hasa wa wahalifu hawa ni akina nani!

Mkuu kwa heshima kubwa, tuendelee na mjadala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…