Tetesi: Ben Saanane kuna biashara gani unafanya na ubalozi wa Sahara Magharibi na Kundi la TASSC?

Lile swali kuhusu ile .mu.su. uliyokuwa umepewa ili umshughulikie Zito hivi umelijibuje kamanda. Ni hilo tuuu.
 

Yapi hayo yanayotokea CHADEMA? Si uyaseme na kwa uzuri anzisha uzi wake, utajibiwa tu!

Lakini ulichokifanya hapa ni sawa na kuchanganya nyama na mlenda na kuwatengea watu wale!!
 
Huyo Saanane mambo ya Chadema tu yamemshinda sembuse mambo mengine ya juko nje. Kama ni mchambuaji mzuri aanzie na chadema kwanza. Kwa sababu huwezi.ukakimbilia kujenga masuala ya utaifa kwanza wakati masuala ya ndani tu yanatushinda
 
Safi Ben Saanane wewe unapiga propaganda huku zinakuingizia pesa, wafundishe na nyumb.u wenzio waropoke ki maslahi kama wewe.
KATAA KUWA NYUMB.U
 
Kuna wajinga wanaweza kuuza nchi kwa pesa ndogo sana.
 
Mkuu...hapa hushangazwa sana pia na makamarade wenzetu wa shaksiya ya kiwango cha kina Komrade Ben S.....yale wanayoyasema wala hayastaajabishi...kabisa, kabisa, kabisa!
..kinachostaajabisha ni yale ambayo, yanastahili kusemwa, kutolewa ufafanuzi, kuyakiri ktk kweli yake, kunyamaziwa ...!
....namna hii, lazima tukiri kuwa harakati za kuinusuru, kuilinda, na kuiendeleza, Tanzania huru, (naam, Tanzania huru!) kwa kutegemea vijana wasomi wanasiasa,wakiwemo wenye upeo wa juu wa kiwango cha kina Ben, zimefitiniwa na fitna za kila aina! (Ukanda, ukabila, jinsia, udini, "utafutaji pesa", ukibaraka...nk....nk)
...lkn sawia na walivyonusurika kina Shadrack, Meshack, na Abednego wa ktk biblia, watanzania, wenye tafakari huru,na wanyoofu kiuadilifu, watanusurika (kwa maana halisi ya kunusurika!)
 
Ben amewashinda tabia CCM wamuache tu afanye kazi yake hawamuwezi.
 
Meza ya mazungumzo maana yake ni nini? Kwamba sasa Moroco wanaikalia Sahara Magharibi "kidogokidogo", au unalenga kusema kitu gani? Kwahiyo meza ya mazungumzo ina maana yoyote kuliko matokeo ya mazungumzo yenyewe? Au ndio maana mnasema hata Burundi wako katika meza ya mazungumzo kama ilivyokuwa Zanzibar ya Jecha?
 
Kuna mambo ya menivutia kwenye huu utetezi.

1. Anaye jitetea ni Saanane na mwenyekiti wa harakati ya sahara magharibi Shao.

2. Reference ya misimamo ni mwl Nyerere, ila alijutia kufanya biashara ya diamond na de-beer makaburu. Pamoja na kujutia si biashara ilifanyika?

3. Mchambuzi mkubwa hivi mpaka anapata consultancy haelewi kinachoendelezwa na watawala wa SA ya sasa tulivyo jinyima na kuacha fursa nyingi za taifa hili kwa ajili yao. Kweli nimeamini kunawatu wanatumia moyo kufikiri badala ya akili.

Na washawsha!
 
Algeria ina bifu na Morocco? Hawa wote sio waarabu na pia dhehebu lao ni suni?
 
Tuangalie pia Tanganyika na Zanzibar malalamiko tupu. pia mfn mzuri uchaguzi mkuu mwaka jana. .... Safari ni ndefu sana ya watu kuacha hili jitu linaitwa UNAFIKI.
 
Jamani mnamsingizia Ben Saanane, hana uwezo wa kuvuruga ziara yoyote! hata ya profesa Lipumba tu, kuhusu kutumika hiyo iko wazi kila siku anashinda mitandaoni kumtukana Magufuli kwa sababu ya hela mbuzi anayolipwa na chadema iliyonunuliwa na fisadi lowasana kuhusu kujifagilia kufanya consultancy labda anafanya consultancy ubalozi wa nyumba kumi [HASHTAG]#bensaananeAchaSiasaZaMajiTaka[/HASHTAG]
 
Punguza munkari, kisha fanya tafakari...wakielewana kama dalili zinavyojionesha?....kura ya maoni ikiangukia upande wa yale ambayo Morocco inayang'ang'ania?
....kuwa mhalisia kivitendo, leo hii unaisaidiaje Polisario, ktk harakati zake kivitendo, ktk mazingira ambayo harakati za kijeshi zimesimama, na wanazungumza?
....kisha siasa za Zanzibar, na Burundi, ulizoziingiza hapa, zinashabihiana kivipi?
...kwa wafuasi wa siasa koko za kukinzana ktk nchi yetu, inaelekea kuna upande unataka tumia suala la ziara ya mfalme wa Morocco, na mahusiano yanayoimarishwa kama bakora dhidi ya wapinzani wao...lkn bahati mbaya ktk hili hii bakora ni dhaifu kwenye mambo yao sawia na kutumia ubua mkavu wa mtama ulioliwa na mchwa, kumpigia mtu mzima...utaishia mtia vumbi na ubua kuvunjika..."hii ( ya Mgogoro wa Sahara magharibi) si silaha inayofaa ktk kukabiliana kwenye siasa zenu koko na za kujishusha" buddy!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…