Benaco Ngara: Madereva wa Malori wa Tanzania, wamejichukulia sheria mkononi kuzuia Malori yote kutokea Rwanda kuingia nchini

Unafikiri nini sasa huyo jamaa afanye? Anunue ventilator au achimbe kaburi?
Ushauri wako please.
 
Mbona chato ipo karibu na Joni yuko pale kwanini asiwasiliane na ndugu yake Paulo kwamba haya mambo siyo
 
Tusishangilie uhuni,kila mtu akiamua kujischukulia sheria mkononi mwaka,hapa patakuwa hapatoshi,tunatakiwa kulaani kwa nguvu zote uhuni huo,wahuni sio serikali ,ni serikali ndio inatakiwa itoe maamuzi.
 
kwani rwanda wagonjwa wameisha?
Wamepona 129.
Active case 132.
tofauti yao na yetu ni ipi?
Si wangeendelea kukaa ndani
Sent using Jamii Forums mobile app
 

Tanzania ni nchi huru, siyo kila raia anakubaliana na maamuzi ya rais wetu, wapo wanaosema tuwaige nchi jiraninkama yenu, yeye kaona (kama kiongozi) njia tunayo pitia ndiyo nzuri. Jambo amablo ni zuri kwa kiongozi kusimamia unacho kiamini.

Hata nyie banyamulenge, maamuzi mlioyofikia ya kujifungia ndani, ni maamuzi yalio amuliwa na rais wenu kwa niaba yenu. Kwakuwa bado huu ugonjwa upo tu sana, mwisho wa siku njia iliyotumiwa na mmoja wetu, itakuwa bora kuliko ya mwingine.

Hata hivyo, mambo yanayo husu Internal Affairs yetu, tuachie wenyewe iwe mbaya au nzuri, ila siyo kibali cha nyie banyamulenge mtunyanyasie raia wetu au mtumie mwanya huo kujinufaisha kwa kuwapa ajira raia wenu wa malori kwa kuminya wakwetu.

Nafikr ni wakati sasa, baada ya Korona kuisha tu, kupiga marufuku malory yenu na nyie kuingia kufuata mizigo. Nchi zingine malory yao hayaji huku.
 
Unafikiri nini sasa huyo jamaa afanye? Anunue ventilator au achimbe kaburi?
Ushauri wako please.

Mkuu kununua ventilator labda awe Mo au Manji maana bei yake si mchezo. Kuanza kuchimba kaburi atajichosha si unajua mazishi husimamiwa na serikali na watu wasiozielewa kumi?


Hapo kwa msimamo wa serikali yetu anatakiwa kuwa mobile tu - (to keep fingers crossed).

Kwa maana serikali imeamua wa kufa afe wa kupona apone.
 
Tusishangilie uhuni,kila mtu akiamua kujischukulia sheria mkononi mwaka,hapa patakuwa hapatoshi,tunatakiwa kulaani kwa nguvu zote uhuni huo,wahuni sio serikali ,ni serikali ndio inatakiwa itoe maamuzi.

Mkuu hawa ni madereva tu ambao viwango vyao vya elimu labda unavijua.

Somo liliopo hapa:

Palikuwa na unyanyasaji, bila shaka kwa muda mrefu, bila shaka bila usaidizi. Bila shaka wakatambua kilichowaponza ni unyonge wao. Ndiyo maana wakaona hawana namna ya kuomba mapinduzi yaani mabadiliko.

Mkuu ni hivyo hivyo tulivyopata uhuru.

Madereva wako vizuri.

Mamlaka zinapopuuza na kukalia haki za watu wake ni vyema zikajua ni suala la muda tu.

Palipo na nia pana njia!
 
Hawa madereva wa Tanzania wakamatwe na kutiwa ndani kwani Rwanda iko sahihi kulinda wananchi na nchi yake.
 
Mbona chato ipo karibu na Joni yuko pale kwanini asiwasiliane na ndugu yake Paulo kwamba haya mambo siyo

Taabu ni kuwa Joni kapambana na Corona kimkanda mkanda siku 45 hatoki mtu nje. Sasa kumshawishi aridhie kuletewa Corona na wapiga nyungu nadhani ndipo ngoma ilipo.

Labda hapo sasa inahitaji kina Mbatia akili kubwa na SMS za usiku wa manane.
 
Pale jirani anapowafukuza watoto wa mwenzie ambao hawataki kuoga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…