Bendera mpya ya Syria yapandishwa Leo katika ubalozi wa nchi hiyo Mjini Moscow Urusi

Sir John Roberts

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
12,835
Reaction score
23,584
Haya mambo kiukweli yananichanganya Bado sijaelewa picha inayochezwa hapa.
Leo katika Hali inayoonesha kuwa Urusi imeutambua rasmi uongozi wa mpito wa waasi wa Syria imepokea mabadiliko ya bendera ya taifa hilo katika ubalozi wa nchi hiyo huko Moscow Urusi na bendera hiyo mpya kupandishwa na ya zamani kuteremshwa.

Kwa wanaojua vizuri masuala ya kidiplomasia ni mpaka nchi mwenyeji aridhie balozi ndio mambo mengine yaendelee. Wakati huo huo Assad aliyekua Rais wa Syria nae yupo urusi akiwa kapatiwa hifadhi ya kibinadamu.
Acha tuone mbele kitatokea nini.
 
Mrusi kashajua Assad kapigwa mpaka kakimbia.

Mrusi anajua kuwa ana base za kijeshi Syria na bado anazitaka, hivyo ni muhinu aendeleze mahusiano na serikali mpya.

Mrusi amekubali ukweli kwamba, kwenye diplomasia hakuna rafiki wa milele wala adui wa milele, kuna interests za nchi tu.

Hivyo ndivyo chess linavyochezwa.
 
Hilo eneo ilipopandishwa bendera SIO Russia bali ni Syria. Hivyo Russia HAWEZI kwa namna yoyote kuwazuia Wasyria kufanya chochote kwenye ardhi yao ili mradi tu hawavunji makubaliano ya "The Vienna Convention".
 
Mtazamo wako unaheshimiwa
 
Hilo eneo ilipopandishwa bendera SIO Russia bali ni Syria. Hivyo Russia HAWEZI kwa namna yoyote kuwazuia Wasyria kufanya chochote kwenye ardhi yao ili mradi tu hawavunji makubaliano ya "The Vienna Convention".
New Syrian Government Flag raised over Syrian embassy in Russia . Haya soma kwa kiingereza labda utaelewa
 
New Iraq,Afghanistan,Lyibiais coming
 
Mkuu mwenye macho haambiwi tazama, sasa ni wazi kwamba waliochukua nchi Syria ndio wenye ubavu wa kupambana na Israel Assad alikuwa tepetepe, Assad alikuwa hana majibu alipokuwa akishambuliwa na mazayuni sasa wanaume wameishika kambi subiri mziki uanze.,

Ivi wewe huoni kwamba Assad amekuwa laini sana kupinduliwa? Iran walirudisha majeshi yao na jeshi lilokuwa linamlinda Assad pia walitokomea makusudi hakuna ata mzinga mmoja uliolia. Wacha bendera ipandishwe juu mkuu
 
Hilo eneo ilipopandishwa bendera SIO Russia bali ni Syria. Hivyo Russia HAWEZI kwa namna yoyote kuwazuia Wasyria kufanya chochote kwenye ardhi yao ili mradi tu hawavunji makubaliano ya "The Vienna Convention".
Haya hiyo kutoka Sky News labda utaamini kwa sababu ni chombo cha habari kutoka nchi za western
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…