habari ndugu zangu. Mimi ninamiliki nyumba mbili mabibo dar. Eneo ni zuri na barabarani kabisa, nahitaji kubomoa hizi ili nijenge ghorofa Moja floor tatu kwaajili ya apartments. kwakua eneo ni kubwa eneo litakalo baki ntafanya parking ya biashara. I am sure this is a good businesses.. Je Kuna anaejua kama hii itakubalika kwa bank?
Kajaribu CRDB kama una hati au leseni ya makazi
Kaka nadhani kuna mambo mengi yakuangalia kabla ya kufikia huko unakofikia,
1. Kwa harakaharaka, kwa nyumba kama hiyo unayosema unahitaji si chini ya milion 500 kuisimamisha
2. Kuwa na nyumba ya kuweka Dhamana sio guarantee ya bank kukupa mkopo, cha muhimu wanaangalia utarudishaje huo mkopo, namaanisha hivi una njia gani nyingine (kazi, Biashara) halalin ambayo inakupa kipato kitakacholingana na mkopo unaotaka?
3. kwa soko lililopo una uhakika unaweza kulipa deni kwa muda muafaka?
ni Kweli ninahitaji 500 m, mimi ni mfanyakazi na kipato cha kazini hakiendani na mkopo huo. Soko lililopo ni la uhakika kwa Sasa ninavyumba 14 na napangisha 50. I have a good business proposal
Hata mm nina shida kama yako mkopo wa 500 mln kwa hesabu ya haraka ya calculator utalipa kwa miaka 9 kwa sh 10 mln @ mwezi kama jumla billion 1, je return zako zitamudu hayo marejesho ? km chini ya hapo itakuwa zaidi ya miaka 15
kupata hata mil 800 inawezekana shida ni kwamba kwa hiyo hela unayotaka marejesho utakwama tu ndugu maana kurejesha 10m Kila mwezi itakusumbua sana.mwenzio nina mil 40 NMB narejesha kwa mwaka mmoja..hilo rejesho linanitoa jasho..na biashara ilivyo ngumu..sasa mpaka hiyo nyumba ikamilike marejesho utakua unatoa wap?hebu nenda crdb maana hata mimi nlishaisikia hiyo ya marejesho kwa miaka 30 unaweza kupata maelezo kwa kina..nimekutamani na mpangp wako mzuri..Mungu akufanikishe lengo lako litimie!
Jamani naomba ufafanuzi kwa wenye uzoefu na zitto kabwe foundation niliiona huku kwenye jf nikajaza fomu Yao ya kutaka mkopo sasa ninatakiwa nilipe tag 84000nipate mkopo ni kweli? Naomba mnishauri naogopa utapeli
Wacheki Kenya commercial bank(KCB) Wana mikopo mizuri ya ujenzi
mkuu ulifuta nilichokushauri mbona nimerudi sijakiona?
Cheki na Covenant Bank for Women (CBW) ni benki inayokuja kasi, mimi nimechukua mkopo hapo last week.