TANZIA Bernard Kamilius Membe afariki dunia
Musiba atakuwa na smiling face siku ya leo.
Lakini Shangazi bado yupo na anadai zile 2B+
Atanyolewa tu in any way.
Deni lipo pale pale tena sahivi ndio mbaya maana tunajua marehemu alikataa kusamehe, Msimamizi wa Mirathi hataweza wala hatakuwa na uwezo wa kufanya vinginevyo.

Mirathi ya Marehemu Membe inaweza ikawa na kesi nyingi kama ya Marehemu mzee Regnald Mengi, tusubiri mivurugano
 
Bush lawyer, Membe alishamaliza kesi mwenyewe kilichobaki ni mirathi ya wanufaika, endeleeni kudanganyana tu.
Defamation ni personal matter, hakuna mtu anaeweza mdai Musiba zaidi ya Membe ata kama mahakama imetoa hukumu; aliekusudiwa kulipwa hayupo tena.

Si usubiri uone badala ya kupiga kelele za chuki.

We unadhani Musiba akifungua kesi ya appeal na mdai hayupo kuna kesi tena hapo; wakati ni personal matter.

Hilo deni halipo tena technically
 
Kazi ya Msimamizi wa mirathi ni kukusanya madeni ya marehemu na kulipa madeni anayodaiwa na kugawa Mali za marehemu kwa haki.

Ningekuwa ni mtoto wa Membe hizi ndio pesa sahihi za kula pisi Kali za mjini.
Hiyo yawezekana lakini hata huyo msimamizi akipata hiyo pesa itakuwa ni ndogo kutokana na makato ya lodi ya "Inheritance tax" na hii ni kwenye makaratasi na si uhalisia.

Itakatwa sana kwa sababu zingine ikiwa ni pamoja na madeni kama marehemu anayo kutegemea na mahakama itavoona.

Ila kwa dalili hizi yaonyesha wazi kuwa uwezekeno wa Musiba kulipa hizo pesa ambazo itasemwa hana (huenda wakamshauri ajitangaze kafilisika) haupo na huenda pia akashauriwa kujitangaza kuwa ni "bankrupt".

Kwa kuwa hili suala lina zogo basi litamalizwa kiaina.

Hakuna mkate mgumu mbele ya chai.

Nchi hii kuna watu (Mazee wa DS) waiongoza kwa mtindo wa kipekee sana.

Weye fanya mambo yako ila usiingie kwenye 18 yao.
 
Mfahamu walau kwa ufupi Bernard Kamilius Membe, aliyepata kuwa waziri wa mambo ya nje katika awamu ya 4.

1. Bernard Kamilius Membe alizaliwa tarehe 9 Novemba, 1953, Rondo, Chiponda, katika Mkoa wa Lindi, akiwa ni mtoto wa pili kati wa watoto saba (7) waliozaliwa katika familia ya Mzee Kamillius Anthony Ntachile na Mama Cecilia John Membe.

2. Kwa kabila, Bernard Membe ni Mmwera, na kama ilivyo desturi ya Wamwera, watoto hutumia jina la ukoo wa Mama. Hivyo watoto wote saba wa familia hii ya Mzee Kamillius wamekuwa wanatumia jina la upande wa mama yao, Cecilia, yaani Membe.

3. Huyu ni mseminari kwelikweli kwani kwa asilimia kubwa alipata elimu yake huko Seminarini kama ifuatavyo
1962 – 1968: Elimu ya msingi katika shule ya msingi ya Chiponda, Lindi.
1969 – 1972: Elimu ya Sekondari, (O-level) Namupa Seminary, Lindi
1973 – 1974: Kidato cha tano na sita (A-level) Itaga Seminary, Tabora.

4. Mwaka 1975 akiwa na miaka 22 tu aliajiriwa serikalini katika idara ya Usalama wa Taifa. Kutokana na kazi hii ndipo jina la Jasusi Mbobezi wakati akiingia kwenye siasa likaibuka.

5. Ukisikia wanamuita Mwana diplomasia basi ujue Membe ni kweli amepiga shule kuhusu masuala ya mahusiano ya Kimataifa. Elimu yake ni kama ifuatavyo;
1981 – 1984: Alipata Shahada ya kwanza katika tasnia ya Sayansi katika maswala ya Siasa na mahusiano ya kimataifa (Bachelor Political Science and International Relations)
1985 – 1989: Aliendelea na ajira yake serikalini katika katika ofisi ya rais
1990 – 1992: Alipata Stashada ya Uchumi, Mahusiano ya Kimataifa na Sheria za Kimataifa (Masters- Economics, International Relations and International Law)
1993 – 1994: Alirudi serikalini kuendelea na kazi kama mchambuzi za mambo ya ulinzi na usalama

6. Ni miongoni mwa wanausalama mahiri kuwahi kuwa nao nchini. Amepitia kozi mbalimbali za kijasusi ndani na nje ya nchi. Kwa kifupi ni jasusi msomi. Mwaka 1978, Ndugu Membe alipata Mafunzo ya sheria za Jinai na usalama wa nchi, nchini Uingereza.

7. Mwaka 2000, aliingia Bungeni baada ya kuchaguliwa na wananchi wa jimbo la Mtama, kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

8. Mwaka 2005, Bernard Membe alichaguliwa tena na wananchi wa Jimbo la Mtama kuwawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano. Tofauti na kipindi cha nyuma, Bernard Membe alianza muhula wa pili wa Ubunge, Januari 2006, kama ‘front bencher’ baada ya kuteuliwa na rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani.

9. Hata hivyo miezi michache baadae, yaani January 2007, rais Jakaya Mrisho Kikwete alimteua Bernard Membe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa baada ya aliyakuwa anashikilia wadhifa huo - Dr Asha Rose Migiro - kuteuliwa na Katibu Mkuu Baraza la Umoja wa Kimataifa na kuwa Naibu Katibu mkuu wa baraza hilo. Bernard Membe amehudu katika nafasi hiyo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa tangu 2007 hadi 2015, akiwa ni Mtanzania wa pili kushika wadhifa huo kwa miaka mingi mfululizo, akitanguliwa na Rais Kikwete ambaye alidumu katika Wizara hiyo kwa miaka 10 mfululizo.

10. Mwaka 2015 alichukua fomu za kugombea Urais lakini alishindwa na John Pombe Magufuli.
Mwaka 2020 aligombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya ACT Wazalendo baada ya kufukuzwa CCM lakini hakufua dafu. Baadae alirejea tena CCM.

Bernard Membe enzi za Uhai wake alibahatika kuwa na watoto watatu tu ambao ni; Cecilia, Richard na Denis.
 
Wazuri hawafi, alisema Mzee Makamba, RIP Membe, kila nafsi itaonja mauti, na duniani tu wapita njia tu mambo ya kujipiga kifua na kujiona mungu mtu ni ujinga tu ,wanadamu yatupasa tuwe wanyenyekevu, kuna watu wengine tena watu wazito wanashangilia vifo vya wenzao,hata kama mtu humpendi kwa jadi yetu sisi Waafrika hatupaswi kushangilia kisa tusiompenda kaondoka kwa hiyo sasa ndio muda muafaka wa kulamba asali. RIP brother Membe Mungu akuondolee adhabu ya mauti,sote tu wakosaji kutokana na tamaa za kidunia ambazo hutujaza kiburi na kuona hakuna wengine zaidi yako mwenyewe.
umeandika vizuri ila kwa sasa watu wanamihemko watarudi tena baadaye kwako ila hii kauli Mzee Makamba utamtesa mpaka anaenda kaburini.
wakati mwingine mtusamehe sisi watu wafupi huwa hatukubali kushindwa na inafika wakati tunaendeshwa na mihemko bila kujua dharau zinakuwa nyingi na hali ya kukomeshana atanijua mimi ni nani!
kipo cha kujifunza yote poleni wafiwa na MWENYEZI MUNGU awape moyo wa kuvumilia matamshi na maandishi yatakayowakwaza huku mkikumbuka maisha ya siasa ndivyo walivyo kukiwa na sherehe za shangwe kwa ushindi wowote uliopata lakini pia wako walioumizwa pia hivyo tuwape nafasi ili mwisho wa siku tufikie equilibrium kwa wote tukimtukuza MWENYEZI MUNGU kuwa yeye ndiye mwenye haki siku zote na mwingi wa huruma.
poleni wafiwa natumaini muda si mrefu watatangaza taratibu za Msiba
 
Is just a coincidence or it related to the case mentioned above☝️☝️☝️☝️?

Kuugua ghafla asubuhi ya leo na kufa hapohapo?

Jamani ni maswali tu. I am just curious.
Hiyo itakuwa ni BP au fatal heart attack. Hakuna la ajabu hapo hasa ukizingatia kuwa alikuwa kwenye 60s.

Siku hizi vijana wadogo wa 45 wanazimika kwa presha na heart attacks sembuse 60s huko?

Au unafikiri majasusi wenzake wamemzidi mahesabu?
 
Kwa kufuatilia maelezo yako yanaonesha kuwa huenda ni kweli jamaa anahusika?!
Mungu pekee ndo anaejua,
Deni lipo pale pale tena sahivi ndio mbaya maana tunajua marehemu alikataa kusamehe, Msimamizi wa Mirathi hataweza wala hatakuwa na uwezo wa kufanya vinginevyo.

Mirathi ya Marehemu Membe inaweza ikawa na kesi nyingi kama ya Marehemu mzee Regnald Mengi, tusubiri mivurugano
Sasa mvurugano upi?Kaacha mke na watoto watatu tu,ambao mama yao ni mmoja.Wala hata hawataendelea na hili dai.
 
Kama Taifa tunatakiwa tutoke kwenye siasa hizi za chuki zilizozalishwa baada ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015. Baada ya Uchaguzi ule na John Pombe Magufuli kuingia madarakani, kulitokea uhasama mkubwa sana kati ya watu waliokuwa wanamuunga mkono na wale waliokuwa wanapingana na staili yake ya utawala.

Leo Baada ya kutangazwa kwa Kifo cha Bernard Camilius Membe, unaona kabisa limeibuka kundi la watu humu JF ni kama wanahanikiza furaha yao kwa kifo cha Membe. Watu hao ambao wanajificha nyuma ya kuonesha furaha kwamba Cyprian Musiba hatalipa tena hela alizotakiwa kumlipa Membe, lakini kwa undani unaona kinachowafurahisha zaidi ni kuona mmojawapo wa wapinzani wa Magufuli naye Kafariki.

Wakumbuke kwamba ni wao waliokuwa wanasema wakati wa msiba wa Magufuli kwamba "hakuna atakayeishi milele" na Leo ni ushahidi mwingine kwamba hakuna atakayeishi milele.

Watu wafanye maridhiano dhidi ya nafsi zao!!
Hakuna mtu anashangilia kifo cha mtu ila ktk hili ni SoMo kwetu hasa wale waliopo ona Magufuli amefariki wakaona ndio muda wakumnanga na kumsema yote wamesema kumbe njia ni moja kwangu ni mvua imeanza japo wengi hawato amini. The list I well known by unknown. Hangaikeni na pelekeni mashauri Mengi juu ya Hayati Magufuli ila mwisho sote ni waja wake na sote tutarejea. Hayati hana kosa na kama anakosa basi ccm ndio wajijuwe makosa yake ni kwa kukitetea chama na sera za chama ambazo ndio sababu ya chama. Chama kina sera je mlitaka sera yakula nchi while watu hawana kitu ama ujenzi wa Taifa? Je mlitaka chama cha mapandikizi na kulitesa Taifa na kugawana vyoe au chama chenye kusimamia haki na kuleta heshima kwa kila Mtanzania, je mlitaka chama cha undugu au chama cha watu wote... Tafakarini kabla yakuinua midomo na kumsema vibaya Hayati. Asante
 
Haya mie nalia
FsdPCyrWIAIeVqk.jpg
 
Back
Top Bottom