Bernard Kamilius Membe niliyemfahamu, Taifa limepoteza mtu!

Bernard Kamilius Membe niliyemfahamu, Taifa limepoteza mtu!

Bernard Kamilius Membe Waziri wa zamani wa Mashauri ya Kigeni nchini Tanzania, Mwanachama wa chama cha Mapinduzi, na mhudumu wa hadhi ya juu wa Idara ya Usalama wa taifa na "nusu" padre ambae taifa la Tanzania na ulimwengu wa kijasusi utaendelea kumkumbuka daima.

Historia ya Membe inaanzia mbali kidogo toka kusini mwa Tanzania katika kijiji cha Rondo hadi mikono salama ya useminari, chini ya ukasisi wa Namupa Seminari. Bernard Kamilius Membe kijana wa kati mwenye uso angavu akiketi dawati la Tatu kutoka kulia, alikuwa mtoto mwenye akili isiyo ya kawaida akiwa mbele ya watoto wenye vipaji shuleni hapo, Kasisi Mariano anamueleza Bernard kama kijana wa mfano kwa nyakati hizo ambaei hakuwa wakusimamiwa kila jambo,

Hayo ni ya Namupa Seminari, lakini sifa zake zinazidi hadi alipojiunga na shule ya upadre kule Itaga Seminari katika mapito yake kielimu, Kanisa katoliki Useminari wa Itaga wanajiuliza hadi leo ilikuwaje kijana huyu mtawa akaacha utume wa upadre na akaibukia ofisi ya rais tena kitengo nyeti cha kuchakata marundo ya taarifa za nchi toka kila pande ya nchi.

Bernard Membe kutoka Darasa la awali hadi High School yani upadre, hakuna mahali panapotaja mapungufu yake kiakili darasani wala hakuna tukio lolote la utovu wa nidhamu la kukumbukwa, iwe katika mitiahani, michezo, uongozi shuleni ama sifa yoyote mbaya toka kwa wakufunzi wake. Pengine hii ndio sifa kuu iliyompendeza Mkuu wa majasusi Tanzania kumchukua. Kwaujumla alikuwa ni mwanafunzi wa vipaji maalumu kwa mtazamo wa kikatoliki kabisa ambae kanisa lilimtarajia kumtawaza kama padre wake,

Mwaka 1978 Membe aliingia kwenye ajira rasmi ya serikali akihudumu Ofisi ya Rais Idara ya Usalama wa Taifa kitengo cha uchambuzi wa taarifa za kijasusi, Kazi hiyo amehudumu kwa miaka kumi na mbili tu hadi 1989 na kisha akaenda masomoni katika chuo cha Johns Hopkins Marekani, alikosomea Diplomasia katika Uhusiano wa Kimataifa kutoka 1990 hadi 1992 akarejea nchini na akahamishiwa Wizara ya Mashauri ya Kigeni na kwenda Ottawa Canada kuwa mshauri wa Kibalozi kutoka 1992-2000,

Korido za Ujasusi zinaeleza kuwa, Utumishi wake ndani ya Idara ya Usalama ulikuwa wa kutukuka na ameacha kumbukumbu yake nzuri hasa katika medani ya Ujasusi unaovuka mipaka, mfano akiwa masomoni Johns Hopkins, alikuwa ni mmoja ya maafisa waliofanya vizuri katika masomo ya vitendo yaliyofanyikia London katika idara ya Ujasusi ya Scotland Yard (Polisi ya Uingereza) na kupewa tuzo maalumu ya Banquets ikitolewa na the greater wa Scotland Yard Sir Kenneth Newman. Nje ya Diplomasia, Membe alichukua kozi muhimu ya Forensic Criminology.

Mwaka 2000 aliingia kwenye siasa akawa Mbunge wa Jimbo la Mtama, nakisha tarehe 17/10/2006 hadi 1/11/2007 aliteuliwa kuwa naibu Waziri wa Nishati na Madini, na kisha 1/12/2007 mpaka 2015 akawa Waziri kamili wa Mashauri ya Kigeni. Katika kipiti cha utmishi wa Bernard Membe ndani ya Wizara taifa lilipitia migogoro mikubwa ya Kidiplomasia na mataifa ya kigeni na yeye kwa nafasi yake alitatua, Mathalani Mgogoro na Malawi wa Ziwa Nyasa, Mgogoro na Rwanda, Mgogoro na Kenya, Mgorogoro na Uingeraza, Mgogoro na ummoja wa nchi wa Hisani wa Maendeleo za Ulaya, mgogoro wa Comoro, Afrika Magharibi nk. Haya yote yalitukia katika uongozi wa Bernard Membe katika Wizara namba mbili ya kidiplomasia inayohusika na mashauri ya Kigeni.

Baada ya kustafu utumishi, Membe alifanya kazi binafsi za ushauri wa kiusalama Nchini Uturuki kwa rafiki yake mkubwa Recep Tayyip Erdoğan Rais wa Uturuki, Nchini Zimbabwe kwa rafiki yake mkubwa Jenerali Mnanagwa rais wa Zimbabwe, nchini Malta kwa rafiki yake mkubwa Joseph Muscat Waziri mkuu wa zamani wa Malta nk. Lakini kubwa zaidi, Bernard Membe, ndie mwanaccm pekee ambae hakumuogopa Rais Magufuli pamoja na utawala wake wote wa mkono wa chuma, alimpinga hadharani hadi kufukuzwa ndani ya ccm, kwakusimamia msimamo wa haki ya kisiasa ndani ya ccm. Baada ya Magufuli kufariki na Rais Samia kushika madaraka, Membe alirejea CCM kwa uchangamfu uleule bila kutetereka .

Tumuenzi Membe kwa ujasiri na uthubutu wake, Tumuenzi kwa malezi yake mema kwa vijana, Vijana wengi wamepita katika mikono ya Membe, amelala akijivunia kulea na kukuza vijana ambao sasa wanalitumikia taifa kwa weledi mkubwa.

Nina msiba mzito, Nina historia ndefu na Hayati Membe, tutasimuliana kadiri Mizimu ikinijaalia...! Pumzika kwa amani Bernard Membe

Na Yericko Nyerere.

View attachment 2619873
Tujisifa twa kuokoteza. Hamna kitu hapo. Hajafikia hata 1% ya shujaa wetu.
 
Msibani mtu anakuwepo masaa 24 ?!!!!

Hebu tuwe na utamaduni wa kusifia mazuri wafanyayo wengine.....
Ishia hapo hapo , na tunapoelekea mtakubali shoo, uzuri tunaeleka kubaki kizazi cha waliovurugwa mtatukubali, ngoja wazee wenu wanaowapa kiburi washushe mvi chini
 
Bernard Kamilius Membe Waziri wa zamani wa Mashauri ya Kigeni nchini Tanzania, Mwanachama wa chama cha Mapinduzi, na mhudumu wa hadhi ya juu wa Idara ya Usalama wa taifa na "nusu" padre ambae taifa la Tanzania na ulimwengu wa kijasusi utaendelea kumkumbuka daima.

Historia ya Membe inaanzia mbali kidogo toka kusini mwa Tanzania katika kijiji cha Rondo hadi mikono salama ya useminari, chini ya ukasisi wa Namupa Seminari. Bernard Kamilius Membe kijana wa kati mwenye uso angavu akiketi dawati la Tatu kutoka kulia, alikuwa mtoto mwenye akili isiyo ya kawaida akiwa mbele ya watoto wenye vipaji shuleni hapo, Kasisi Mariano anamueleza Bernard kama kijana wa mfano kwa nyakati hizo ambaei hakuwa wakusimamiwa kila jambo,

Hayo ni ya Namupa Seminari, lakini sifa zake zinazidi hadi alipojiunga na shule ya upadre kule Itaga Seminari katika mapito yake kielimu, Kanisa katoliki Useminari wa Itaga wanajiuliza hadi leo ilikuwaje kijana huyu mtawa akaacha utume wa upadre na akaibukia ofisi ya rais tena kitengo nyeti cha kuchakata marundo ya taarifa za nchi toka kila pande ya nchi.

Bernard Membe kutoka Darasa la awali hadi High School yani upadre, hakuna mahali panapotaja mapungufu yake kiakili darasani wala hakuna tukio lolote la utovu wa nidhamu la kukumbukwa, iwe katika mitiahani, michezo, uongozi shuleni ama sifa yoyote mbaya toka kwa wakufunzi wake. Pengine hii ndio sifa kuu iliyompendeza Mkuu wa majasusi Tanzania kumchukua. Kwaujumla alikuwa ni mwanafunzi wa vipaji maalumu kwa mtazamo wa kikatoliki kabisa ambae kanisa lilimtarajia kumtawaza kama padre wake,

Mwaka 1978 Membe aliingia kwenye ajira rasmi ya serikali akihudumu Ofisi ya Rais Idara ya Usalama wa Taifa kitengo cha uchambuzi wa taarifa za kijasusi, Kazi hiyo amehudumu kwa miaka kumi na mbili tu hadi 1989 na kisha akaenda masomoni katika chuo cha Johns Hopkins Marekani, alikosomea Diplomasia katika Uhusiano wa Kimataifa kutoka 1990 hadi 1992 akarejea nchini na akahamishiwa Wizara ya Mashauri ya Kigeni na kwenda Ottawa Canada kuwa mshauri wa Kibalozi kutoka 1992-2000,

Korido za Ujasusi zinaeleza kuwa, Utumishi wake ndani ya Idara ya Usalama ulikuwa wa kutukuka na ameacha kumbukumbu yake nzuri hasa katika medani ya Ujasusi unaovuka mipaka, mfano akiwa masomoni Johns Hopkins, alikuwa ni mmoja ya maafisa waliofanya vizuri katika masomo ya vitendo yaliyofanyikia London katika idara ya Ujasusi ya Scotland Yard (Polisi ya Uingereza) na kupewa tuzo maalumu ya Banquets ikitolewa na the greater wa Scotland Yard Sir Kenneth Newman. Nje ya Diplomasia, Membe alichukua kozi muhimu ya Forensic Criminology.

Mwaka 2000 aliingia kwenye siasa akawa Mbunge wa Jimbo la Mtama, nakisha tarehe 17/10/2006 hadi 1/11/2007 aliteuliwa kuwa naibu Waziri wa Nishati na Madini, na kisha 1/12/2007 mpaka 2015 akawa Waziri kamili wa Mashauri ya Kigeni. Katika kipiti cha utmishi wa Bernard Membe ndani ya Wizara taifa lilipitia migogoro mikubwa ya Kidiplomasia na mataifa ya kigeni na yeye kwa nafasi yake alitatua, Mathalani Mgogoro na Malawi wa Ziwa Nyasa, Mgogoro na Rwanda, Mgogoro na Kenya, Mgorogoro na Uingeraza, Mgogoro na ummoja wa nchi wa Hisani wa Maendeleo za Ulaya, mgogoro wa Comoro, Afrika Magharibi nk. Haya yote yalitukia katika uongozi wa Bernard Membe katika Wizara namba mbili ya kidiplomasia inayohusika na mashauri ya Kigeni.

Baada ya kustafu utumishi, Membe alifanya kazi binafsi za ushauri wa kiusalama Nchini Uturuki kwa rafiki yake mkubwa Recep Tayyip Erdoğan Rais wa Uturuki, Nchini Zimbabwe kwa rafiki yake mkubwa Jenerali Mnanagwa rais wa Zimbabwe, nchini Malta kwa rafiki yake mkubwa Joseph Muscat Waziri mkuu wa zamani wa Malta nk. Lakini kubwa zaidi, Bernard Membe, ndie mwanaccm pekee ambae hakumuogopa Rais Magufuli pamoja na utawala wake wote wa mkono wa chuma, alimpinga hadharani hadi kufukuzwa ndani ya ccm, kwakusimamia msimamo wa haki ya kisiasa ndani ya ccm. Baada ya Magufuli kufariki na Rais Samia kushika madaraka, Membe alirejea CCM kwa uchangamfu uleule bila kutetereka .

Tumuenzi Membe kwa ujasiri na uthubutu wake, Tumuenzi kwa malezi yake mema kwa vijana, Vijana wengi wamepita katika mikono ya Membe, amelala akijivunia kulea na kukuza vijana ambao sasa wanalitumikia taifa kwa weledi mkubwa.

Nina msiba mzito, Nina historia ndefu na Hayati Membe, tutasimuliana kadiri Mizimu ikinijaalia...! Pumzika kwa amani Bernard Membe

Na Yericko Nyerere.

View attachment 2619873
Yaani mtu akiwa mteja wako tu akifa Taifa limepoteza mtu? Acheni huo ujinga. Membe hakuwa na ukubwa au mchango mkubwa wa taifa zaidi ya kuwa alikuwa tu kiongozi.
 
Lakini usisahau naye Membe kapitia kipindi kigumu sana cha mateso ma kubwa sana kiuchumi , alifungiwa accounts zake na mali zake akaishi maisha magumu sana mpaka akaanza uza magenereter ya nyumbani kwake ili aishi, ni kipindi kigumu sana kwa binadamu yoyote kukipitia cha kudhalilishwa na kuaibishwa kwnye jamii, hivyo hata kama alifurahia kifo cha Magu , kama kwa binadamu yoyote siamini kama asinge smile kama angepita news za kifo hicho kwa jinsi alivyo pitishwa kwenye matatizo hayo makubwa , hata wewe unge smile vile vile kama ungekua wewe na ndio manaa hata wewe kwenye kifo hicho ume sema "Mungu fundi"
Kuhusu ku tosamehe , nani asamehe mtu aliye chafua na kuhakikisha ana filisika ? ni kitu kigumu sana ,Membe hakua malaika ila alikua binadamu aliye pitishwa kwenye changamoto kubwa sana kwa hao hao wenye uchu wa madaraka pia .
Mali za Membe karibu 95% ni za kiharamia,alistahili kufilisiwa,acha aende huko alikomtanguliza Magufuli
 
Mali za Membe karibu 95% ni za kiharamia,alistahili kufilisiwa,acha aende huko alikomtanguliza Magufuli
Ok, ila pia wengi ambao labda nao una waona wapo na unawakubali mali zao ina weza kuwa nazo ni hivyo hivyo .
 
Back
Top Bottom