Bernard Membe apokelewa rasmi ACT–Wazalendo. Atoa ahadi kemkem endapo watashika madaraka

Bernard Membe apokelewa rasmi ACT–Wazalendo. Atoa ahadi kemkem endapo watashika madaraka

Kuna mmoja alisema ccm sio baba yake wala mama yake leo analamba miguu ya jiwe

Na hata Ukimchunguza ' Kiumakini ' kabisa huyu Mtu Mkuu utagundua ya kuwa ana ' CV ' Kali ya Serikalini, Foreign na hata alipokuwa Idarani pia.
 
Maalimu Seif alifukuzwa kwa tuhuma za kuutaka uraisi wa Zanzibar na msimamo wake wa Serikali tatu. Utakuwa umezaliwa juzi na wala hufuatilii dulu za kisiasa za nchi hii au wewe Mnywaranda.

Rudi usome tena nilichoandika. Membe hajafukuzwa kwa msimamo wa kiharakati, ni kwasababu ya tamaa na kujiona ana wanachama wengi nyuma yake, hauwezi kulinganisha na sababu zilizomfukuzisha Maalim
 
Ila kweli hata mbunge mmoja wanaweza wasimpate kama Zitto hagombei,hata akigombea naona wazi uchaguzi huu CCM watatumia mabavu kupora majimbo yote

Umeanza vizuri sana Maelezo yako na nikaanza Kukuona ni ' Mwerevu ' ila ulivyomalizia hapo mwishoni nimegundua una ' Upopoma ' mwingi tu!!!
 
Lowassa alijitoa CCM kwenda kujaribu bahati ya urais. Kilichompeleka upinzani ni TAMAAM YA URAIS.

Membe AMEFUKUZWA CCM sababu ya kudai haki za kikatiba. Kinachompeleka upinzani SIO URAIS bali ni kutafuta HAKI.

Yaani na Wewe unaamini na unaaminishwa kabisa eti kuwa Bernard Membe ana Sifa kabisa za kuja kuwa Rais wa JMT Mkuu? Nimeshakudharau!
 
Rudi usome tena nilichoandika. Membe hajafukuzwa kwa msimamo wa kiharakati, ni kwasababu ya tamaa na kujiona ana wanachama wengi nyuma yake, hauwezi kulinganisha na sababu zilizomfukuzisha Maalim

Unaandika utopolo tu,wasiokuwa na msimamo wote wameomba msamaha. Kuutaka uraisi kwa njia ya kidemokrasia ni uroho wa madaraka? Basi hata huyo Yesu wa Lugola ni mroho wa madaraka ndiyo maana alichapisha form moja tu.

Acha kukariri wewe Banyamulenge.
 
Unaandika utopolo tu,wasiokuwa na msimamo wote wameomba msamaha. Kuutaka uraisi kwa njia ya kidemokrasia ni uroho wa madaraka? Basi hata huyo Yesu wa Lugola ni mroho wa madaraka ndiyo maana alichapisha form moja tu.

Acha kukariri wewe Banyamulenge.

Sawa mzee, basi Membe anatufaa sana
 
Nilipokuwa nasoma shule ya bweni A level, kuna jamaa alikuwa akilazimisha sana awekwe kwenye timu ya shule kwenda UMISETA.

Hiyo ni kwasababu alijiona ni maarufu kwa jina lake na alipenda sana kusifiwa.

Alifikia kufanya shopping ya vifaa vya michezo na akawa amejiandaa kwelikweli.

Alilobby huku na kule kwa mwalimu wa michezo na walimu wengine wakawa wanamuonyesha wanamuonea huruma, lakini kumbe walikuwa wakimwangalia tu akihangaika.

Jamaa alikuwa na tabia ya kukosa maadili ikiwemo tabia ya kutoroka kwenda vijijini kupata ulabu.

Lakini siku wachezaji wote wanapanda basi la kwenda kwenye UMISETA yalipotajwa majina yote kwenye orodha jina la jamaa halikutajwa na akawa "very disappointed".

Michezo ya UMISETA ilipokwisha alijikuta anakubali ukweli kwamba hakustahili kwenda huko.

Nimeishasema humu mara nyingi kwamba kiufundi na kimfumo haiwezekani kwa Bernard Membe kuwa raisi wa nchi hii.

Na hali hiyo inazidi kujidhihirisha.

Ni bahati mbaya sana hapa Jamvini ( JamiiForums ) Watu ' Intelligent ' na ' Visionary ' kama Wewe huwa hamueleweki na ile ' Mipopoma ' Mkuu.
 
Yaani na Wewe unaamini na unaaminishwa kabisa eti kuwa Bernard Membe ana Sifa kabisa za kuja kuwa Rais wa JMT Mkuu? Nimeshakudharau!
Lissu na Membe wote hawatokuja wawe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...

Huku bara sijaona wa kumtikisa Mh. Rais ila kwa upande wa visiwani kutakuwa na mchuano mkali mno kwa bwana Mwinyi..
 
usajili pekee wa maana waloufanya ACT ni maalim seif maana huyu ana wafuasi wake direct bt huyu maembe hana lolote zaidi ya kubwabwaja na kujimwambafy
 
Halafu Jamaa mwili wake unakibaridi utadhani ni mtu anayesimamia samaki na kutoa samaki kwenye majokofu pale bandarini Kwa ajiri ya kuwauzia wateja wa madale, kumbe ni jasusi wa ACT

Tena kama kuna Mtu ambaye anaenda ' Kuwamaliza ' mazima kabisa ACT-Wazalendo ni huyu ' Mgeni Adui na Wakala ' waliyempokea kwa Nyodo.
 
Mara awasalimie UWT mara aishukuru kamati kuu ya CDM. Hivi ata alijua yupo kwenye mkutano wa chama gani kweli.
 
Kwa vyovyote vile naona hesabu haziko upande wa Membe

Kuna swali nimekua najiuliza toka hizi harakati zake za kwenda ACT zianze. Hivi kwanini hakuondoka 2015 na Lowassa aje aimarishe huo upinzani halaf Lowassa agombee uRais

Mbona aliacha miaka 5 yote mpinzani wake ajisimike vizuri chama/dola??

Majibu ni mawili tu 1:Hana nia ya dhati na 2:Sio strategist mzuri

Na majibu yote hayo manaake ni moja tu. Hafai

Hongera sana kwa kuwa Mmoja wa JamiiForums Members ambaye uko ' very Intelligent ' halafu pia ni ' Analyst ' mzuri sana. Nimekukubali Mkuu.
 
Back
Top Bottom