Uchaguzi 2020 Bernard Membe hana kabisa mvuto!

Kule kahama kahutubia watoto na wabodaboda shinyanga haendi Tena nasikia anakimbilia tarime
 
Lissu akienguliwa heri mbowe, nyalandu au Zitto ,Membe hana mvuto kabisa
Lissu aenguliwe kwa sababu zipi? UVCCM na Tume yenu ya Uchaguzi iliyowekwa MFUKONI na Rais hamjambo kwa propaganda.
 
Before ilikuwa twende na Membe kachero mbobezi leo hana mvuto.

Hii dunia iache tu hata huyu wanamshabikia kwa kale kamsemo tu kuwa.....
Hao ndio CCM Mkuu mchana bundi usiku popo... vuli tumbusi, kiangazi fisi!!! Jana twende na Membe, leo kalegea hana hoja!!!
Najiuliza tu;

Alivyokuwa kule waliishi nae pasi kuujua ulegevu wake? (Kama ndivyo kuna walegevu wangapi humo ndani mwao!?)
 
Mange Kimambi yalimkuta haya .... dada hatutakuangusha ... wengine wakatengeneza home made gas-mask ...siku ya siku barabara nyeupeeeeeee... wakarudi ooo tumeshinda wameandamana wao badala yetu .... 😂
Wewe ulikuwa wapi siku hiyo ?

Maana kuna takataka huwa zinaona mambo fulani huwa yanawahusu watu fulani tu, mwisho wa siku kila mtu anasomeshwa namba kwa wakati wake huku wengine wakimwangalia tu.
 
Lakini pia Kikwete na Lowassa.... Walisaidiwa sana na vyombo vya habari.... mitandao ya watu kwenye chama na serikali kujijenga kisiasa.....Na kwa kuwa tayari walikuwa kwenye system Kama viongozi .....iliwasaidia Sana kujijenga ..... kila chombo Cha habari ulikuwa ni kusifia tu....Mpunga pia ulitumika Sana kusaidia hilo...Lowassa Aliingia mpaka kwenye nyumba za ibada kujitangaza....wengine hiyo platform hawajapata..... ndio maana wanaonekana hawana mvuto.....Lakini kwa Membe.....mwili uko upinzani .....akili iko CCM.....kwa kifupi nafsi yake inakataa yeye analazimisha.....Nina uhakika 2025 atarudi nyumbani.
 
... kwa post hii, lengo la mleta uzi Nyani Ngabu linaelekea kutimia! Wapelekee mgawanyiko miongoni mwao!
 
... Nyani Ngabu kachochea tayari; naona fitna zimeanza! Kwa utaratibu huu, wapinzani sahauni kushika dola!
 
... Nyani Ngabu kachochea tayari; naona fitna zimeanza! Kwa utaratibu huu, wapinzani sahauni kushika dola!
Namjua huyu Nyani anavyopenda kuchochea....lakini kwenye uzi huu katoa maoni yenye tija.......kiukweli alichochagua Membe kuongea huko Zanzbar na Pemba hakiendani na mgombea uraisi wa chama kilicho na dira nzuri kama ACT......Hatahivyo, kampeni bado hazijaanza.....Nahisi chama chake kitamfunda
aanze kutema madini.......
 

Kwani hutaki masheikh wanaoozea jela bila haki watoke? - Hilo kwako ni jambo dogo?

Au kwa kuwa ni Masheikh kwa hiyo you don't care, wangekuwa ni mapadri ungesema the same? au hujali tu kwa sababu hawa ni waislamu?

Hili la kuachia masheikh, Lissu mbona analizungumzia pia kwenye ziara zake za kutafuta wadhamini huko mikoani?
 
Sawa. Lakini si jambo kubwa
hilo mgombea uraisi. Kwa uzoefu wake hadhira ya JF ilitegemea ajikite kwenye kero na issue kubwa za kisera....
 
Sawa. Lakini si jambo kubwa
hilo mgombea uraisi. Kwa uzoefu wake hadhira ya JF ilitegemea ajikite kwenye kero na issue kubwa za kisera....
Huyu jamaa hata 2015 alikuwa anakuzwa Sana, Ila Hana sera zozote jukwaani. Sikushangazwa alivyo flop Zanzibar
 
Mimi binafsi siamini kama kweli Membe amekuja Upinzani kwa ajili ya Kuleta mageuzi,maana vile anaongea inaonesha hana nia ya dhati kutoka ndani, sana sana utamsikia,Mimi ndio mnogeshaji,Niguse ninuke Mbona alishaguswa na hakunuka? Nitatimba nchi nzima [emoji41] Mgombea urais labda rais wa lindi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…