Bernard Membe mbona yupo kimya sana?

Bernard Membe mbona yupo kimya sana?

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Jasusi wa zamani wa TISS, Mwanadiplomasia na waziri mstaafu Benard Membe yupo kimya Sana awamu hii.

Membe ni jasiri aliyemtikisa Magufuli na kukosoa utendaji wake tangu mwaka 2016 mwanzoni. Namnukuu"Rais Magufuli asitudanganye eti kapunguza matumizi ya serikali kwa kuunganisha wizara mbalimbali, alichokifanya ni sawa na kupunguza mifuko huku idadi ya mayai ikiwa ileile, yaani kahamishia mayai ktk mifuko michache na sio kuyapunguza mayai. Kama anadai kapunguza wizara ngoja tuone bajeti yake ya Kwanza mwaka huu 2016". Benard Membe.

Alipotoa kauli hiyo alitukanwa Sana na UVCCM ya kipindi hicho. Baada ya hapo alinyamaza kimya na kuibuka baadae na kudai atampinga Rais Magufuli kwa njia ya uchaguzi ndani ya chama 2020. Hawakumvumilia na badala yake alifukuzwa na kuhamia ACT. Aligombea Urais na kuambulia kura chache mno, kura si zaidi ya 60,000.

Je, jasusi huyu yupo wapi mbona hasikiki? Anautazama vipi utawala huu?
 
Alikua online 5 mins ago on Tapatalk nadhani atakuja kuleta mrejesho
 
He deserves the Nobel piece prize if he did this. That monster (jiwe) was evil.
Sijui hapa neno Jiwe ( anayehusishwa ni Mtu ) ameingiaje kutokana na Comment yangu.

Kufafanua zaidi hapo nimemaanisha kuwa assignment ya Kukomboa Pesa zake zilizokwama Dubai kisha Kenya zilifanikiwa tarehe hiyo tajwa ya 17 Machi, 2021.

Mtakaohisi otherwise mtakuwa Morons.
 
Majasusi waliopikwa vizuri huwa na tabia ya kufanya kazi zao kimya kimya bila kelele, kwangu mimi anabakia mtu pekee ndani ya ccm kumtikisa mwendazake enzi zile!

Mimi binafsi sina deni nae, kazi aliyotumwa na kitengo ameifanya vyem!

Lakini kumbuka ukiona kobe kainama ujue anatunga sheria!
 
Mkuu Mightier naona kama kuna kitu unajaribu kukiongea. Hebu weka nyama kidogo.
Ahsante
Kufafanua zaidi hapo nimemaanisha kuwa assignment ya Kukomboa Pesa zake zilizokwama Dubai kisha Kenya zilifanikiwa tarehe hiyo tajwa ya 17 Machi, 2021.

Mtakaohisi otherwise mtakuwa Morons
 
Assignment ipi
Kufafanua zaidi hapo nimemaanisha kuwa assignment ya Kukomboa Pesa zake zilizokwama Dubai kisha Kenya zilifanikiwa tarehe hiyo tajwa ya 17 Machi, 2021.

Mtakaohisi otherwise mtakuwa Morons
 
Jasusi kama jasusi
Kufafanua zaidi hapo nimemaanisha kuwa assignment ya Kukomboa Pesa zake zilizokwama Dubai kisha Kenya zilifanikiwa tarehe hiyo tajwa ya 17 Machi, 2021.

Mtakaohisi otherwise mtakuwa Morons
 
Nasikia Kwenye magrupu ya whatsapp huwa anatuma vibonzo, ila hajibu message😁
 
Back
Top Bottom