Nataka Sana kuamini Bernard Membe ana kitu 'interesting'anakuja nacho lakini nashindwa.
Nionavyo Mimi story ya Bernard Membe itaishia kule kule ilipoishia ya Lowasa na Mrema na wengine.
Nashindwa kabisa kumtazama Bernard Membe kama 'mtu mwenye master plan'
Ya kumtoa Magufuli au hata kuleta Tu demokrasia ya kweli achilia mbali plan ya kukamata madaraka.
Makosa ya Bernard Membe ndo makosa ya Lowasa ..ndo makosa ya Chadema na kina Mrema na wengine.
Well said!
Ili mwanasiasa akubalike kutawala nchi hii, katika ngazi ya Urais, kwa sasa na kipindi kirefu kijacho, ni lazima akubalike na CCM, kwa sababu ni chama cha siasa ambacho kimejijenga kitaasisi na siyo kama kampuni ya mtu binafsi.
Nailinganisha CCM na vilabu vya mpira wa miguu vya Yanga na Simba. Kushindwa kwa vilabu hivyo kuwa mabingwa hutokana na fitina za ndani kwa ndani au kuhujumiana. Ikitokea hivyo, ndipo vilabu vya watu binafsi, km Azam huibuka kuwa washindi.
Hadi sasa, mgombea Urais nchini ataendelea kubebwa na chama kuliko sifa zake binafsi. Chama chenye kuweza kumbeba mwanasiasa, kwa sasa kuwa Rais, ni CCM.
CCM imeota mizizi ndani ya wapiga kura. CCM ni kama Yanga na Simba ambayo haijalishi nani anaiongoza maana kiongozi huyo anaweza kuondolewa madarakani wakati wowote na hivyo vilabu vikabaki kama vilivyo. Historia ya vilabu hivyo na CCM inathibitisha hoja yangu.
Mwaka 2015, Rais Magufuli asingekuwa Rais leo kama angegombea kupitia chama kingine maana uwezo na nguvu ya kisiasa aliyokuwa nayo Lowassa, akiungwa mkono na Sumaye, Marehemu Kingunge na wanasiasa wengine wakongwe na mashuhuri. Pamoja na kwamba Lowassa alikuwa na nguvu nyingine ya vyama vyama upinzani, bado hakufanikiwa kuchaguliwa.
Nje ya CCM, kwa sasa, mwanasiasa ni kama samaki nje ya maji. Si Membe au "Mwembe" mwenye uwezo wa kumwondoa Magufuli madarakani bila kuungwa mkono na CCM. Na CCM ikiamua Magufuli aendelee kutawala milele, itawezekana. Itawezekana kwa sababu zaidi ya WaTz 75% ni CCM na hivyo ikipitishwa kura ya maoni ya kumpa Magufuli Urais wa milele, itashinda.
Rejeeni kura ya maoni ya demokrasia ya vyama vingi, 1992, ambapo zaidi ya 85% ya kura zilitaka nchi ibaki ya utawala wa chama kimoja cha siasa. Ni busara ya Baba wa Taifa, Tanzania sasa ni nchi ya utawala wa vyama vingi vya siasa. Lakini, wanasiasa hawajaheshimu, katu, busara hiyo ya Baba wa Taifa kwa kuanzisha vyama vya mifukoni.
Angalau vyama vya upinzani vya awali, km NCCR-Mageuzi, vilikuwa ni vyama kweli vya siasa kwa sababu vilisimamia Itikadi iliyovianzisha na viongozi wake walikuwa wanasiasa walikomaa, kwa kuwa waliibukia kutoka CCM, chungu cha kupika wana siasa. Lakini kilicho wazi kwa sasa hivi ni kuwepo kwa vyama vya siasa vinavyoongozwa na viongozi wachumia tumbo na wenye uchu wa madaraka.
Chama cha siasa cha wachumia tumbo ni kama CHADEMA. Chama hiki ni dhahiri kinaongozwa na viongozi wa aina hiyo. M/Kiti wake ni mjasiriamali wa kisiasa. Ushahidi ni pale alipompokea Lowassa na kumsimamisha kuwa mgombea wa Urais akiamini angeshinda na chama chake kuunda Serikali, nafasi ambayo ingempa nguvu kubwa kifedha. Hata vile chama kilifanikiwa kupata viti vingi vya ubunge na kujihakikishia ndonge nono la RUZUKU. Hakuna shaka ndonge hilo ndilo linalokisambaratisha chama kwa sababu limethibitiwa na mwenye chama - mlafi na mroho wa fedha hata ofisi ya chama hajengi. Akiulizwa pesa iko wapi anakuwa mbogo na kuwajeruhi waulizao.
Vyama vya viongozi wenye uchu wa madaraka ni hivi vilivyoanzishwa hivi karibuni na wanasiasa waliokosa nafasi za kuongoza vyama vyao vya awali. Chama kama ACT-Wazalendo kinaongozwa na mwanasiasa mwenye uchu wa madaraka kwa kauli na vitendo vyake. Kwamba alifukuzwa CHADEMA kwa kuonesha nia ya kuutaka Uenyekiti, kulimuibua ACT-Wazalendo ambako alitumia uwezo wake kifedha kuwa mwenye chama. Ati yeye si M/Kiti wala Katibu Mkuu wa chama, vyeo vikubwa kwenye chama chochote. Yeye ni Kiongozi Mkuu wa chama, du! Sasa anaungana na mlafi mwingine wa madaraka (kumbukeni alipoteuliwa Makamu wa Rais Zanzibar alitulia kabisa, akaridhika), akiamini wataweza kushinda na kuongoza Zanzibar. Anaamini ikitokea hivyo yeye atapewa madaraka makubwa kwenye Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Kwa hoja zangu hizo bado hakuna mwanasiasa, nje ya CCM, atakayeongoza Tanzania.
Membe anajisumbua bure, hana nguvu ya kisiasa kama Lowassa, Sumaye au marehemu Kingunge. Awapigie magoti ya kuomba msamaha wajumbe wa vikao vikuu vya chama.