Bernard Membe: Tanzania diplomasia imeshuka awamu hii. Tutatengwa na majirani wakiona hatufuati vigezo vya WHO kupambana na COVID19

Bernard Membe: Tanzania diplomasia imeshuka awamu hii. Tutatengwa na majirani wakiona hatufuati vigezo vya WHO kupambana na COVID19

Vitu vingine vinatia hasira!! Miiko gani tumejitenga nayo? Kuna chuki Kali sana dhidi ya Tanzania isiyokuwa na sababu!! Kinachowakasirisha zaidi ni kutuona tunadunda na tunaendelea na shughuli zetu!! Walitazamia tufe kwa maelfu na haijawa hivyo!! Inawauma sana!!!
Rais wetu Dr Magufuli mamilioni ya watanzania tunakushukuru sana kwa uongozi wako katika kipindi hiki ambacho vinginevyo tungepita kwenye ugumu sana!! Tukikushukuru watanzania ikutoshe maana hao mabeberu na vibaraka wao hatutegemei kama wanaeeza kukiri uongozi wako imara japo nafsini mwa o wanajua hivyo! Mungu yuko upande wetu ndio maana matazamio yao hayajafanikiwa!!
Maendeleo ninayoyaona kayaleta JPM ni kutufanya watanzania tuishi kama Hayawani! Utawala wake unavunja Katiba hakuna kuhoji, vyombo vya habari vime- compromise, Bunge lime- compromise, Mahakimu waliowenge wanafuata maelekezo badala ya taaruma yao na hivyo kuifanya Mahakama kuonekana kama nayo ime- compromise, Viongozi wa Serikali za Mitaa hawakuchaguliwa na Wananchi, kukitokea majanga ya asili Serikali badala ya kuwafariji na kuwasaidia Wananchi inawakejeri, no salary increment, no employment, na wakulima wa Mazao ya biashara wanayauza kwa bei ya hasara. Maendeleo makubwa sana aliyoyafanya JPM ni kuvisababishia mateso makali sana Vyama halisi vya upinzani.
 
Mtumwa wa fikra utamtambua tu!! Hata akiwa na uwezo namna gani bado hawezi kujiamini!! Tunaishi kwa kodi zetu pamoja na kwamba mabeberu wametupora sana!! Wanakasirika sana kuona ofisi namba moja haiingiliki!!
Matrilioni ya deni la taifa yametoka wapi? Kodi zetu ndiyo zinazo ongeza deni la taifa? Pamoja na mahaba yako kwa namba moja, tumia akili kidogo. Kilangila.
 
Membe hana hoja sasa ni miiko ipi ambayo hatufati kama mikono kila sehemu ndoo zipo tena ni mandate kuwa n hizo ndoo na sanitizers kila Mabus na gari za mbali lazima unawe kabla hujaingi, Barakoa watu wanavaa hawa na pia mtaani kuna gari zinapita kutoa elimu kwa wananchi juu ya hili janga juzi nimeshuka stand fulani cha kwanza nilipewa sanitizer ni nawe na mgambo wa jiji yani mlangoni tu pale hawawalitaka nini Jamani?? Ni lazima tujifunze kuishi na huu ugonjwa hatuwezi never kujifungia na anaetaka kujifungia hakuna alie mzuia afanye ivo, Sasa ivi Trump aliekuwa anapigia debe lockdown leo Analalama kuwa baadhi ya Senators wa state wanahujumu kwa kuchelewa kufungua state zao ili watu wachape kazi , Boris Johnson anasema watu nilazima tujifunze kuishi na corona na pia badala ya slogan ya stay home sasa ni Take precautions na Chapa kazi, Hawa watu kama Membe au zito nadhani kuna mategemeo yao walitaka either ipigwe totally lockdown watu wakose chakula waje kulalamikia serikali au itokee vifo vingi pia waje kulalamikia serikali au uchumi ushuke sana waje kuilalamikia serikali, Sasa Mheshimiwa Rais amewa outsmart na mambo yanaenda smoothly hao majirani wafahamu tunategemeana waendelee tu kuvimba kichwa na hizo borders sisi ni wakubwa kuliko wao na wanatuhitaji zaidi waendelee kutumiwa tu ili sisi tuonekane hatuchukui hatua na international communities dawa yao inachemka hata mzee hizo virtual meetings zao apotezee tu hawana la maana la kujadili yani measures zinakuwa imposed US leo uzilete third world countries kweli? Ili usifiwe na WHO sijui ivi upuuzi mtupu kenya amekuwa mlamba miguu wazungu kila analo ona anabeba leo wakenya walikuwa wanakufa njaa eti wako lockdown that's pathetic
 
Kwani madereva kutoka Tanzania tu ndio wanakagulimwa Kenya? Hata wao madereva wao au raia wao wakija kwetu tunawapima mbona? na huu utaratibu hutumiwa na kila nchi, sasa kipi cha ajabu hapa.

Kuhusu kufunga mipaka kwani Zambia wamefunga mipaka kwa ajili ya Tanzania? Huu utaratibu wakufunga na mipaka na kuweka nchi lockdown ulitumiwa na nchi nyingi baada ya korona kuingia na hata hivyo bado korona inaendelea kuwasumbua, sasa ikiwa serikali yetu imeamua kutokuweka nchi lockdown na kutokufunga mipaka nini kosa lake?

Sababu kila nchi inahiari ya kuchagua njia yake ya kupambana na corona kwa kufuata utaratibu au muongozo wa WHO, sasa ni utaratibu upi sisi hatujaufuata? ikumbukwe WHO hailazimishi nchi kufungia watu wake ndani au kufunga mipaka.

Taratibu naona hii vita ya corona inageuka na kuwa vita ya kiuchumi, kuna nchi zimefungia watu ndani shughuli za uchumi zimesimama kakini maambukizi bado yanaendelea wakati sisi Tanzania hatujafungiwa ndani maambukizi tunayo lakini kazi tunafanya na tunazalisha na kujenga uchumi wetu, hii inaweza kuwakera baadhi ya watu.

Kwa hali inavyoendelea sasa dunia inaweza kujikuta inapambana na corona na njaa hasa hizi nchi zetu za Africa na hapo ndipo media za nje zitaacha kuripoti idadi ya watu wanaopata corona na kuanza kuripoti watu wanavyokufa kwa njaa na utapia mlo na hapo ndipo Afrika na Dunia itatambua kwa nini Mh. Raisi aliamua kuacha watu wafanye kazi huku wakichukua tahadhari huku mwili ukijitengenezea kinga wenyewe dhidi ya covid.
 
Nimesikilza
Kwa makini mahojiano hayo,yalipangwa na DW na ni bias kabisa
Nasema hivyo kwa sababu eti ni Watanzania tu pekee ndio tutaathirika wakati hata Zambia wataathirika tena pakubwa kuliko sisi watanzania kwa sababu asilimia 70 %ya mizigo ya Zambia inatoka Tanzania
Ukiwa Tanzania tuu utadanganywa sana wafanyabiashara wa Zambia baada ya kuweka VAT kwenye transit goods waliondoka na kuanza kutumia msumbiji na Durban na magari mengi maroli ya Tanzania yaliokua yanabeba huku kwa wateja wao yapo kule hata yule mount meru mtanzania alieshika soko la mafuta Zambia anapokea mafuta Tanzania na Msumbiji...Zambia mizigo mingi wananunua SA na maagent wa SA wapo Zambia tofauti ya baadhi ya bidhaa ya Zambia na SA kwa bei unakuta ni 10,000Tsh kwa caton endeleeni kulishana matango pori Mkongo ndio anatutegemea sisi sio Mzambia ndio maana Zambia wanapata faida kwa kutoza gharama kubwa kwa gari za mizigo zinazopita Zambia...
 
Hizo jumuia za kimataifa hazina hata muda wa kuhangaika na watu.
Wao wenyewe wanakufa kama sisimizi.
Tusiombe tufike huko, kutengwa na jumuia ya kimataifa na majirani pia
Screenshot_20200513-004356.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Diplomat wetu No. 1 Jiwe
Diplomati wetu no. 2 Prof. wa Jalalani ambae ndio mshauri No.1 wa Jiwe.
Juzi juzi hapa
1 Tumemsikia Odinga na alichosema
2. Tumemsikia Ramaphosa na alichosema ( SADCC)
3. Tumesikia EAC walichosema kuhusu ushiriki wetu kwenye mkutano (virtual) wa kujadiri janga la COVID19
Kama kawaida yetu tumewatukana na kuwaita kuwa ni vibaraka wa mabeberu. Walichotaka wao ni mazungumzo.
4. WHO tumewasikia nao tumewaita mabeberu.
Baada ya yote hayo tukiambiwa na mtanzania mwenzetu alikubuhu kwenye diplomasia tunamtolea nje kwa maneno makali. Hivi tunataka kuprove nini?
 
Hata Sukari wanatutegemea?
Nimesikilza
Kwa makini mahojiano hayo,yalipangwa na DW na ni bias kabisa
Nasema hivyo kwa sababu eti ni Watanzania tu pekee ndio tutaathirika wakati hata Zambia wataathirika tena pakubwa kuliko sisi watanzania kwa sababu asilimia 70 %ya mizigo ya Zambia inatoka Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu akikosa hoja utamjua tu!! Siwezi kukulaumu kwa matusi maana ndivyo ulivyolelewa!! Pole!! Matusi hufanya kazi mbili tu: 1. Hufunua moyo wa mtu jinsi ulivyo mchafu. 2. Hufunua namna mtu alivyolelewa toka utotoni!! Pole! maana unaaonyesha kuwa wewe ni mhanga wa malezi mabovu!! Nitakuwa punguwani nikikulaumu!!!
Sijakytukana, nimekuuliza swali, hivyo jibu swali.
 
kwamba ukidaiwa na China ndio nini? hivi hata unaelewa unachozungumza?

hata putin alishawahi kusema USA is weak nation protected by technology, sasa hio muscle unaongelea ni ipi, infact haijui ata inalipaje madeni yake zaidi ya kuchapisha tu noti mpya ambayo itatuathiri wengine wote tunaotumia USD as foreign reserve
 
hata putin alishawahi kusema USA is weak nation protected by technology, sasa hio muscle unaongelea ni ipi, infact haijui ata inalipaje madeni yake zaidi ya kuchapisha tu noti mpya ambayo itatuathiri wengine wote tunaotumia USD as foreign reserve
sasa hata kama ndio hivyo huwezi kuiweka kwenye kapu moja na tz, ndio ilikuwa hoja yangu, vitu anavyofanya Trump na matamshi yake dhidi ya China na WHO, Tz haiwezi kuiga simply haina huo ubavu.
 
sasa hata kama ndio hivyo huwezi kuiweka kwenye kapu moja na tz, ndio ilikuwa hoja yangu, vitu anavyofanya Trump na matamshi yake dhidi ya China na WHO, Tz haiwezi kuiga simply haina huo ubavu.

Kwahio we unataka tuwanyenyekee ama? lazima heshima iwepo , kila kitu kifanyike uku tukujua tunafaidi nchi yetu kama hawataki basi kwan Korea waliwezaje kupewa heshima yao na wanaongozwa na dikteta,
 
Kwahio we unataka tuwanyenyekee ama? lazima heshima iwepo , kila kitu kifanyike uku tukujua tunafaidi nchi yetu kama hawataki basi kwan Korea waliwezaje kupewa heshima yao na wanaongozwa na dikteta,
Sijasema unyenyekee, tread carefully, unajua wananchi Korea wanaishi maisha gani?
 
Back
Top Bottom