Akihojiwa na DW, waziri wa zamani wa mambo ya nje mheshimiwa Bernard Camilius Membe amesema katika awamu hii ya utawala wa Magufuli, diplomasia imeshuka mno.
Membe anaonya kwamba, tanzania awamu hii inajiendeshea mambo kivyakevyake nje ya utaratibu wa jumuia ya kimataifa.
Akoingelea suala la korona, Membe amedai kuwa Tanzania haiheshimu na imejitenga na miiko ya shirika la afya WHO.
Chanzo: DW
=====
Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje, Bernard Membe amezungumzia uhusiano wa Kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na nchi za jirani katika kipindi hiki cha mlipuko wa #COVID19
Amesema kwasasa nchi zipo katika mapambanao dhidi ya #CoronaVirus na dio maana nchi kama Zambia zinafunga mipaka yake na kuzuia watu waziende ikiwa ni njia ya kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo kutoka sehemu moja
Amesema "Kama Zambia wamefunga mpaka wake na kuzuia magari yasipite, huo ni mkakati na hatua ya kuzuia maambukizi ya #COVID19 na ndio maana inatakiwa tufanye mambo haya kwa pamoja kwa pande zote mbili"
Aidha, kuhusu kupimwa kwa Madereva wa Tanzania wanaotaka kuingia Kenya, amesema kidiplomasia ni kwamba nchi za jirani zina wasiwasi sana kwamba Tanzania inaweza kuwa inapeleka ugonjwa huu kwenye nchi fulani
Ameeleza "Wasiwasi huu unaweza kuwa unakuja baada ya kuona pengine hatufungamani ni vigezo vya WHO ambavyo vimewekwa na dunia nzima vinavifuata labda mpaka pale tutakapofungamana na vigezo vya WHO wanavyofuata wenzetu"
Ameongeza "Kwa na mna Tanzania inavyoshungulikia jnaga kama hili tutatengwa, majirani watatutenga na kutengwa ni kwa namna hii ya kufunga mipaka na kidiplomasia tunasema mtengano huu unatumiiza na kututesa zaidi sisi kuliko majirani"
Amemalizia kuwa ni kweli diplomasia imeshuka kwasababu awamu hii haijengi kwenda na dunia inaangalia zaidi matatizo ya ndani na ina athari zake hasa tukipata janga hili na ndio maana tunasema diplomasia imeshuka sana