Bernard Membe: Tanzania diplomasia imeshuka awamu hii. Tutatengwa na majirani wakiona hatufuati vigezo vya WHO kupambana na COVID19

Nimesikiliza dw mchana huu mzee wa diplomasia kafunguka duuu...

Sent using Jamii Forums mobile app

Mashabiki na Wakereketwa wa CCM ya Jiwe Naona radio zote za nje mtaziita za MABEBERU.
Hii jioni BBC wanasema Madreva 25 wa Tanzania wamepimwa na kukutwa Wana Covid-19 na WAMEZUIWA kuingia Kenya.
Kwa hiyo BBC ni MABEBERU na Kenya wanatumiwa na Mabeberu....Nonsense!
 
Jidanganye kuna Beira Msumbiji na Welvisbay Namibia

Unajua Mafisccm wengi wanaongozwa na Ushabiki wa kijinga na wala hawajui hata Jiografia ya Africa& Dunia yote.
Mtu kufikiri eti Zambia ikifunga mpaka na Tanzania itakosa Bandari ya kupitisha bldhaa zake ni upuuzi mtupu!
 
Unajua Mafisccm wengi wanaongozwa na Ushabiki wa kijinga na wala hawajui hata Jiografia ya Africa& Dunia yote.
Mtu kufikiri eti Zambia ikifunga mpaka na Tanzania itakosa Bandari ya kupitisha bldhaa zake ni upuuzi mtupu!
Tena hili tukio la corona kupuuzwa na magufuli ndio wake up call yao

Ninavyowajua waZambia watabadili port sema waKongo ndio wataumia kidogo halafu na wao watahamia Namibia
 
Membe amesahau wakati wake ambapo Tanzania ilikuwa imetengwa na Kenya na Uganda kwenye maamuzi hasa kwenye ujenzi wa treni za "standard gauge". Alipokuja Magufuli kila kitu kilibadilika. Bomba la Mafuta likapita kwetu. Standard gauge inajengwa kuunga nchi za Uganda, Rwanda, Burundi, Congo. Ile ya kuotokea Kenya kwenda Uganda imekufa. Sasa utasemaje diplomasia imekufa. Je wewe ulishindwa nini kutetea haya. Ulitengwa na mikutano ulikuwa huendi. Sasa hapa mwenye kushindwa kidiplomasia ni wewe au marehemu Mahiga! Ulitumia diplomasia kupata pesa ya kujenga kiwanda cha simenti kwetu, lakini ukaziweka zote mfukoni! Unataka uraisi ili ukope na kuweka mfukoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…