Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,296
- 122,540
Anayevuma kwa sasa ni Tundu Lissu tu.
Na si kwamba anavuma kwa sababu ana sera bora na anazinadi kwa ustadi!
La hasha.
Anavuma tu kwa kelele kelele anazozipiga akiwa huko kwenye mizunguko yake ya kutafuta wadhamini.
Sasa ikija kwa Bernard Membe, si ajabu ukimwuliza Mtanzania wa kawaida barabarani kuwa jana au leo Membe alikuwa wapi, sidhani kama kuna mtu ataweza kukuambia.
Kwa Lissu hali ni tofauti kabisa. Majuzi ile alikuwa Ikungulyabashashi. Juzi alikuwa sijui Arusha au Kilimanjaro. Jana alikuwa Iringa au Morogoro....
Sasa huyo ‘jasusi mbobezi’ yeye yuko wapi?
Hata vile vijembe vyake dhaifu kule Twitter naona hatoi tena.
Isije akawa keshaguswa na sasa ananuka!
Jamaa ni dhaifu sana. Siasa naona haimkubali. Haiba yake haiendani na mikikimikiki na mashamsham ya kisiasa.
Na si kwamba anavuma kwa sababu ana sera bora na anazinadi kwa ustadi!
La hasha.
Anavuma tu kwa kelele kelele anazozipiga akiwa huko kwenye mizunguko yake ya kutafuta wadhamini.
Sasa ikija kwa Bernard Membe, si ajabu ukimwuliza Mtanzania wa kawaida barabarani kuwa jana au leo Membe alikuwa wapi, sidhani kama kuna mtu ataweza kukuambia.
Kwa Lissu hali ni tofauti kabisa. Majuzi ile alikuwa Ikungulyabashashi. Juzi alikuwa sijui Arusha au Kilimanjaro. Jana alikuwa Iringa au Morogoro....
Sasa huyo ‘jasusi mbobezi’ yeye yuko wapi?
Hata vile vijembe vyake dhaifu kule Twitter naona hatoi tena.
Isije akawa keshaguswa na sasa ananuka!
Jamaa ni dhaifu sana. Siasa naona haimkubali. Haiba yake haiendani na mikikimikiki na mashamsham ya kisiasa.