Bernard Membe yupo kweli?

Bernard Membe yupo kweli?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Anayevuma kwa sasa ni Tundu Lissu tu.

Na si kwamba anavuma kwa sababu ana sera bora na anazinadi kwa ustadi!

La hasha.

Anavuma tu kwa kelele kelele anazozipiga akiwa huko kwenye mizunguko yake ya kutafuta wadhamini.

Sasa ikija kwa Bernard Membe, si ajabu ukimwuliza Mtanzania wa kawaida barabarani kuwa jana au leo Membe alikuwa wapi, sidhani kama kuna mtu ataweza kukuambia.

Kwa Lissu hali ni tofauti kabisa. Majuzi ile alikuwa Ikungulyabashashi. Juzi alikuwa sijui Arusha au Kilimanjaro. Jana alikuwa Iringa au Morogoro....

Sasa huyo ‘jasusi mbobezi’ yeye yuko wapi?

Hata vile vijembe vyake dhaifu kule Twitter naona hatoi tena.

Isije akawa keshaguswa na sasa ananuka!

Jamaa ni dhaifu sana. Siasa naona haimkubali. Haiba yake haiendani na mikikimikiki na mashamsham ya kisiasa.
 
Hivi Magufuli nae anatafuta wadhamini au? Mbona hata hajaanza na tarehe za kurudisha fomu inakaribia naomba kwa anaejua anielekeze plz!
 
Anataka kumtoa madarakani bwana yule ....wa chama kile...

Eti membe naye ni mpinzani anaogopa kulitaja jina la mtu anayepambana naye na pia chama anachoshindana nacho anaogopa kukitaja jina
Hapo ndo ujue hakuna lolote!
 
Ninawasiwasi yupo anasuka mipango ya kumsaidia mwinyi kimyakimya huku akiwalaghai ACT kuwa yupo pamoja nao. hawa majasusi sio watu wa kuwaamini. Linapokuja swala la "maslahi ya taifa" huwa wanamisimamo yao...
Huyo jasusi bado hajaonja joto ya jiwe ya kuwa upinzani!

Siku atayopewa msukosuko atarudi mwenyewe CCM bila kupenda.
 
Membe anaweka maslahi ya Taifa mbele siyo yake binafsi

Na hakuna maslahi makubwa kwa nchi zaidi ya kusaidia juhudi za kumng'oa Magufuli madarakani october 28 ,maana Magufuli ni sehemu kubwa ya kikwazo cha maendeleo ya kweli nchini hususan kwenye suala la fundamental freedoms za wananchi!

Kwa hiyo Membe yuko behind the scene anafanya hiyo kazi kwa weledi mkubwa sana
 
Isije akawa keshaguswa na sasa ananuka!
Wewe ni Ngabu kweli, Sisi kwetu Jina Ngabu linamaanisha, ni mtu ambaye Kwa Wakati Fulani, njaa imemshika,bahati Nzuri pengine akakutana na mtu akampatia karanga za kutafuna, Wakati wakiachana tu na huyo mtu aliyemgea karanga, Mbele yake akamwona mtu ambaye naye ananjaa, huyo mtu akataka kuomba karanga Ili ale, matokeo yake aliyeombwa, akaztupia zote mdomoni mwake akimwambia Yule jamaa aliyeomba kuwa, nimemaliza karanga na mdomo umejaa karanga asiweze hata kuongea vizuri, hiyo ndio inaitwa amezi Ngabu
 
Back
Top Bottom