Betting ni biashara inayolipa, mpaka radio zimeamua kuachana na malengo ya msingi zimehamia huku. TCRA mpo kimya tu

Betting ni biashara inayolipa, mpaka radio zimeamua kuachana na malengo ya msingi zimehamia huku. TCRA mpo kimya tu

RADIOs na TVs ila RADIOs Sana sana. Yaani ukifungua tu unakutana na tangazo la kamari. Kama zamani ilikuwa matangazo ya waganga wa kienyeji.

Sasa hivi Radio zimeamua zichezeshe zenyewe michezo hii. Hii biashara inaonekana kulipa sana.

Sijui tunatengeneza kizazi cha aina gani? Ukifungua hapa ni betting ukifungua chochote ni kamari tu. Watoto wanaokua wanajifunza nini?

Kwa maslahi ya kipato na kodi tunaharibu kizazi kijacho na cha sasa?

Yaani radio kwa siku. Content ni 20% ila BETTIN ni 80% where are we heading to?
Hatari hatari hatari sana
 
Hapo mwanzo hz redio zlikua znapokea matangazo kutoka kwny makampun ya kubeti mfano tatu mzuka, biko n.k

Kheeee badae hz redio zkaona mh mbona hawa watu wa makampun ya kubeti wanapiga hela

Ghafla zkajikuta nazo zinageuka na kua kampun za kubeti
Clouds fm wanaita mchongo pesa
Efm wanaita mshindo milionea,toboa kiulaini
Wasafi fm wanaita chota mihela

Kibaya zaidi wanapromote mpaka kero yan kila baada ya dakika 5 wanakwambia weka buku utashinda daaah mpaka kero

Yan wanaboa kinoma mi sku hz sisikilizi hzo redio labda mara moja moja sana. Nkifungulia redio natune 92.5 Hitz fm Dar es salaam. Hii radio inapiga mziki mwanzo mwisho. Hakuna cha matangazo wala nn

Zaman kdogo kulikua na stations nyng znazopiga mziki asbuh mpaka usku ila sku hz nazo zmeanza matangazo mfano 102.5Fm, 98.9Fm n.k
 
EFM ndio waliooanza na MSHINDO
Clouds wakaiga na MCHONGO
Wasafi wakaingia kichwa kichwa na WASAFI BET... wakaona haitoshi wakaja na CHOTA MIHELA...

Jinsi wanavyopromot hadi aibu... Yaani ni njaa ndio yazidi...
Tena hao wasafi FM ndo wanakera mno siku hizi, kiasi kwamba hata sports arena imepoteza mvuto, wanatumia muda mwingi kuchambua chota mihela badala ya mpira, wachambuzi wamegeuka mapromota wa kamari.
 
Mi nasikiliza Radio Maria tuu,hakuna hayo makero
 
Tena hao wasafi FM ndo wanakera mno siku hizi, kiasi kwamba hata sports arena imepoteza mvuto, wanatumia muda mwingi kuchambua chota mihela badala ya mpira, wachambuzi wamegeuka mapromota wa kamari.
Alafu hao hawajui hata kuprogram mambo yao... Kuna wakati wanasahau wanadhani wapo kwenye kipindi cha kamari na si michezo tena...

Mpaka wamejishusha thamani wachambuzi wao...
 
Najiuliza. Redio zetu. Siku nzima zinachambua mpira, udaku n.k.
Hazizungumzii kilimo, maji, elimu, usalama n.k.
Wamemtumbukiza Mama.
Hivi Greyson Msigwa. Unapokimbizana na kapu la minoti. Sahihi kweli. Fuata taratibu za kibenki
 
Wanahabari wa siku hizi wanakosa content ya kuwasilisha.
Wengi wa wanahabari hawa sio professional made,
Walaji nao wa kizazi kipya wanavutiwa sana na udaku badala ya hard news.
Tv na radio stations zinaendeshwa na soko liliko.
Sisi tulioishi tangu zamani ndio tunaona utofauti huu.
 
Tafuta odds 1.20, three times a week..kila mkeka weka laki tano tano..faida ni laki 3 kwa @ wiki..Jiulize kama mangi dukan anapata faida ya 5000 ktk mauzo ghafi ya vocha za 100,000/= na hayo sio mauzo ya sku 1.
Tatizo huwa zinachana hata utafute 1.02 hiyo ni labda under 5.5.....game inaisha 5-1 😆😆😄 mi nimefanya sana sema labda uzisome game na ubeti mara moja kwa wiki..

Labda una hiyo 500K unastake 1.2 faida ni 100K kwa wiki na kwa mwezi ni 400K profit out of 500K. Ukiwa na 1mil. Unamake 800K monthly sema ni Big risk bado na kwa mtu asiye kuwa na subira asicheze hii afanye shughuli nyingine😁
 
Back
Top Bottom